Baada ya kupatikana Viongozi wa VIWAWA ngazi ya Jumuiya ndogo ndogo na kanda, na Baadaye wakapatikana Viongozi wa Kigango cha Mbweni, Mt. Rafael na Jumapili iliyopita tukahitimisha kwa kuwapata Viongozi wa Kigango Mama cha Boko.
Hii ilikuwa ni safari ndefu yenye Maombi kwani tunaelewa viongozi Bora ndiyo dira ya vijana wetu kwa kipindi kijacho cha miaka mitatu..
Shukrani nyingi kwa Kamati tendaji za Walei Vigango vyote kwa usimamizi mzuri walioufanya, na viongozi wetu walichaguliwa kuanzia jumuiya mpaka Kigango ni jukumu lenu kuona mashirikiano kati yenu yanakuwa mazuri na tunawajenga vijana wetu katika ustawi wa kiroho na kimwili.
Jumapili hii ndiyo tunawachagua Viongozi wa Parokia ambao ndiyo kiunganishi kati yetu, ni jambo kubwa lahitaji maombi sana ili Roho Mtakatifu atuongoze kuwachagua wale ambao watakiongoza chama chetu na kutufikisha katika malengo yetu.
hili ni jukumu la viongozi wote wa Vigango na mnatakiwa kufika Parokiani Boko saa 4 asubuhi tayari kwa maandalizi ya Uchaguzi.
Tunawatakieni kila la kheri katika uchaguzi huo na Roho Mtakatifu awaongoze........Mapendo sana....
Thursday, March 7, 2013
Historia ya Makanisa Zanzibar
1800 – 1900
WAKATOLIKI, MAKUNDI YA WAKIRISTO WASIOPENDA MIKUTANO ASMI, VITA AU GHASIA (QUAKERS) NA UJUMBE WA VYUO VIKUU KWA AFRIKA YA KATI ( UMCA)
Baada ya Wareno kurudi nyuma Wakiristo kidogo tu Wakigoa
ndio waliobakia Zanzibar.
Wakiristo
hawa hawakuwa na kanisa la kufanyia Ibada lakini waliweza kuifanya hai jumuia
yao kwa kwa kuifanya ibada zao kibinafsi. Baadae katika miaka 1800 makundi ya
watu wa wamagharibi yalianza kujumuisha wamisionari na wachungaji wamisionari
waliokuwa wakipita pita mara chache na wachungaji katika meli bandarini. Katika
mwaka 1844 wamisionari wa kikiristo zaidi wa kudumu waliwasili Afrika mashariki
kwa kupitia mchungaji wa kilutheri Joseph Krapf na wafuasi wawili ambao
walifanya kazi kwa ajili wa Jumuia ya kimisheni ya kanisa la kiingereza (English
Church Missionary Society). Wakifanyakazi, Mombasa, walitembelea Zanzibar na
miaka michache mbeleni walitoa kamusi bora kabisa la Kiswahili lakini hawakuwahi
kuanzisha kanisa ndani ya visiwa hivyi.

Ukuwaji
wa harakati dhidi ya utumwa ndani ya Uingereza ulishajiisha raghba ya
wamisionari wakiristo, ikikuzwa na hotuba ya David Livingstone aliyoitoa mwaka
1857 akiomba Uingereza kupeleka wamisionari na wafanyakazi Afrika. David
Livingstone alilingania kwamba mwisho wa utumwa utakuwepo tu kupitia “ biashara
na ukiristo”. Baadae Livingstone alitumia siku nyingi tu Zanzibar ambao
alipatiwa nafasi ya kutumia nyumba ya Sultani.
Hotuba zake zilipelekea kuundwa kwa ujumbe wa Vyuo Vikuu
kwa Afrika ya Kati (UMCA). Ujumbe wa Vyuo Vikuu kwa Afrika ya Kati ulikuwa ni
mashirikiano baina ya kitivo na wanafunzi waliopitia vyuo vikuu vya Oxford and
Cambridge, ambao baadae tu waliungana na mashabiki kutoka vyuo vikuu vya Durham
na Dublin. Katika mwaka 1860 walimchagua Charles Mackenzie kama ni “Askofu wa
Afrika ya kati” na ilipofikia mwezi wa Oktoba wa 1860 alikuwa njiani kuelekea
huko Afrika ya Kati.
Lengo la ujumbe wa vyuo vikuu kwa Afrika ya kati (UMCA)
lilikuwa ni kufikisha dini ya kikiristo kwa watu wengi sana waliokuwa Afrika ya
Kati, kuzunguka ziwa Nyasa, ambalo Livingstone alilizungumzia kwa ufanisi. Kwa
ajili hiyo, baada ya kufika Afrika Kusini Askofu Mackenzie na wafuasi aliokuwa
nao walisafiri kwa boti mpaka mto Zambezi na baadae hadi mto shire kuasisi
ujumbe wa mwanzo wa ujumbe wa vyuo vikuu kwa Afrika ya Kati katika Afrika katika
sehemu iliyojulikana kama Magomero.
Wakati ujumbe huu na eneo lake ulichukuana na jina na ari
ya jumuia mama, Ujumbe huu ulishuhudia kushindwa kwa aina yake kutekeleza
malengo yake. Maradhi na njaa na ukame uliwakumba wamisionari wa mwanzo na
kupelekea kufa kwa askofu. Kundi hili lililazimika kuondoka katika eneo hilo
ndani ya kipindi
cha miaka mitatu kwa sababu eneo hilo lilikuwepo mbali sana
na upatikanaji wa bidhaa kutoka nje na vituo vya mawasiliano, eneo hilo halikuwa
na mazingira mazuri ya kiafya kwa wale ambao hawana uzoefu na mazoea na hali ya
hewa ya hapo na pia eneo halikuwa na utulivu wa kisiasa. Askofu mpya, George
Tozer, kwanza alijaribu kuupeleka ujumbe maili 200 mafikio ya mtiririko wa mto
kuelekea eneo la muanuko lakini hata hivyo eneo hilo mara tu liligundulika kuwa
halikuwa na mazingira mazuri ya kiafya na kwa hiyo lilihamwa kwa miezi hivi tu.
Wakichukua bidii za makusudi, ili kutorejea makosa
yaliyopita viongozi wa ujumbe wa Vyuo Vikuu kwa Afrika ya Kati (UMCA)
waliangalia uwezekano wa kituo au eneo jengine ambalo litatumika kuweza kufika
kati kati ya Afrika. Maeneo mbali mbali yalifikiriwa kutumika kama Kisiwa cha
Johanna, maeneo katika mwambao wa Afrika Kusini lakini kwa bahati Zanzibar
ilikubalika kutumika kutokana na muundo mzuri wa njia za mawasiliano,
upatikanaji mzuri wa bidhaa za chakula na wingi wa upatikanaji nguvu kazi bora.
Ujumbe wa Vyuo Vikuu kwa Afrika ya Kati (UMCA) uliobakia uliwasili Zanzibar
tarehe 31/08/1864.

Ruhusa iliyotolewa na Sultan Majid kwa Wafaransa hawa
kuanzisha duka ndani ya Zanzibar ilitafsiriwa kama ni juhudi za Sultani za
kuweka “ uwiano wa nafasi kubwa waliokuwa nao Waingereza Zanzibar kwa
kuwakaribisha wapinzani wao wakuu wa kizungu.” Ikiwa ushindani wa kisiasa ndio
uliompelekea Sultan Majid za kukaribisha pamoja matawi tofauti ya wamisionari
wakiristo hata hivyo matokeo hayakuwa hayo kwani kwa upande wa wamisionari hawa
hakukuwa na msuguano wowote. Mahusiano yao mazuri makundi hayo mawili ya
wamisionari ulitokana na ukweli kwamba Ujumbe wa Vyuo Vikuu kwa Afrika ya Kati
wa kianglikana (UMCA Anglicans) ulikuwa ni ujumbe wa watu watukufu ambao wenye
mafunzo ya kikatoliki ya kiengereza (Anglon Catholic Learnings)
Wamisionari
wakifaransa walikuwa makini kuepuka matatizo yoyote Zanzibar “kwa kutambua
uhalisia wa maisha ulivyo ndani ya nchi ya kiislamu ya Zanzibar, Wafaransa
kuanzia 1862 wafuasi wa Holy Ghost Order, waliamua kujikita katika maeneo maalum
kama ya elimu, shughuli za uchungaji kwa jumuia ndogo ya mjini ya magoa
wakatoliki na huduma za afifu na walifungua hospitali ya mwanzo iliyopendekezwa
na Sultani ya kizungu. Kwa hili waliojenga maoni mazuri kwa warabu.
Juu ya ukarimu wa watu wa Zanzibar, Wazanzibar hawa kidogo
hawakuwa na azma yoyote kufuata imani ya wageni hawa wapya. Wamisionari wa
kikatoliki walilielewa hili lakini waliamini
kwamba
kundi kubwa la wafuasi wapya wa dini hii ya kikiristo litaweza kupatikana masafa
machache kuvuka mlango bahari wa Zanzibar huko Tanzania Bara.
Walipeleka ujumbe mdogo Bagamoyo katika mwambao wa Tanzania Bara katika mwaka
1868 na kwa sehemu kubwa walitumia nafasi walizonazo Zanzibar kama ni makao
makuu ya kuzidisha harakati zao Tanzania Bara. Harakati hizi ikiwemo ujenzi wa
“ Hospitali ya Kifaransa” ndani ya Bagamoyo.

“ Hospitali ya Kifaransa” ndani ya Zanzibar ilijengwa
mkabala na jengo la watawa. Hospitali ilimalizwa kujengwa na kuanza kazi
kufikia mwaka 1890. Kipindi hicho wakatoliki walien delea kutumia uhusiano
mzuri na majirani zao wa Zanzibar, wakipata ruhusa ya kujenga kanisa la
mtakatifu Joseph katika mwaka 1894. (Cathedral of Saint Joseph in 1894). Jiwe
la msingi la kanisa
hili kuu liliekwa tarehe 10 Julai 1896. Misa ya mwanzo katika kanisa hili kuu
jipya iliendeshwa na Askofu Allegeyer katika usiku wa krismas 1898.
Kadri
ya wakati ulivyokuwa ukienda, hospitali hii ya Zanzibar ilipungua umuhimu wake
na jengo hilo likafanywa kuwa ni skuli. Hii ilikuwa ni skuli ya kitawa ya
mtakatifu Joseph (St. Joseph Convent School).
Wamisionari wa Ujumbe wa Vyuo Vikuu kwa Afrika ya Kati
(UMCA) hawakuzubaa katika kipindi hichi. Akianzia kwanza kuishi katika nyumba
Mambo Msiige, katika eneo la Shangani, ambapo haikuwa mbali na ujumbe wa
Kifaransa, Muingereza mchapa kazi shupavu alianzisha ustawi wa majengo
ya ukubwa wa kuvutia na ya aina tofauti. Kwanza walinunua sehemu ya ardhi ya
kilimo Kiungani pembezoni mwa mji wa Zanzibar Kaskazini. Ujenzi wa “bweni kwa
ajili ya vijana watumwa walioachiwa huru” uliendelea katika eneo hilo kufikia
mwaka 1866. Karibu ya hapo mava sehemu ya kuzikia ilianzishwa, na hadi leo mava
hii inayo baadhi ya mabaki ya wakiristo wa mwanzo wa Zanzibar.
Baadae ilinunuliwa ardhi nyengine katika mwaka 1873, ardhi
hii ilikuwa karibu na kitovu cha mji ambalo ni jengo kubwa zima la mjini ambalo
liliwahi kuwa uwanja wa soko kongwe, ambapo watumwa walikuwa wakiuzwa, Mara
wito ulitolewa wa fedha kusaidia ujenzi wa kanisa katika eneo hilo ambao uovu
huo wa biashara ya utumwa ulifanyika. Huu ulikuwa mwanzo kanisa kuu la kristo
(Christ Church Cathedral).
Mwaka uliofuata Ujumbe wa Vyuo Vikuu kwa Afrika ya Kati
(UMCA) walinunua ardhi ya kilimo Mbweni kusini mwa mji karibu na bahari.


Jiwe la msingi la kanisa kuu la ujumbe wa Vyuo Vikuu kwa
Afrika ya Kati (UMCA Cathedral)
liliekwa
mwaka 1873 katika siku ya siku kuu ya krismas katika eneo la mjini. Uwanja wa
soko kongwe ulianza kujazwa majengo ya ujumbe wa Vyuo Vikuu kwa Afrika ya Kati.

“Jumba la Mkunazini” lilijengwa katika mwaka 1875 na kanisa
mara baada ya kujengwa jumba la kunazini lilihamisha makao makuu yake kutoka
Mambo Msiige na kuwa Mkunazini. Zahanati
ilijengwa
katika mwaka 1877, hatimae iligeuzwa kuwa hospitali yenye kutoa huduma kamili
katika mwaka 1893. Skuli ya Mtakatifu Mon`ica, nyumba ya kasisi mkuu na Askofu
ilijengwa katika uwanja wa soko kongwe. Jengo hilo la skuli ya Mtakatifu Monica
bado mpaka leo linatumika kama ni hostel/dahalia Mtukufu Monica.

Mwenye kustahiki sifa ya mafanikio haya ilikuwa hakika ni
kanisa kuu la kristo. Mradi usio wa kibiashara ambao ulisimamiwa binafsi na
Askofu wa tatu wa Ujumbe wa Vyuo Vikuu kwa Afrika ya Kati Edward Steere,
utabakia kuwa moja ya mifano ya kuvutia na bora wa usanifu majengo ndani ya
Afrika uliofanywa na wakiristo wa mwanzo.














Theodore Buft aliamini kwamba biashara na ukiristo ilikuwa
ndio njia ya uongofu na kuweza kuweza kuelimika.
Watumwa na Waliobadili Dini

Lakini juu ya hivyo, wingi wa wakiristo hawa wapya na
mahitaji yao maku bwa yalikuwa ni changamoto kwa raslimali na subira ya
wafadhili wao. Wakiangalia demografia wamisionari waliona njia pekee ya
kuwahudumikia wakiristo wapya ni kuanzisha chimbuko la Padri wa kiafrika.
Kwa hivyo wote wakatoliki na waprotestanti walifanya bidii
kuwajumuisha makundi ya kienyeji shughuli na mambo ya kanisa na hii yote
ilipelekea kujua na kufunza mtumishi bora kwa ajili ya kuendesha shughuli za
kidini.
Kwa Zanzibar harakati zote hizi zilikuwa katika eneo la
Kiungani ambapo kwanza ilianzishwa “dahalia kwa watumwa vijana walioachiwa huru”,
na baadae “Chuo cha Mafunzo ya ualimu cha Mtakatifu Andrew” na baadae “Chuo cha
kidini/theolojia” kila moja kati ya hivyo kilijaribu kuwafunza na kutathmini
matokeo ya vijana wa kiafrika. Kiasi cha wanafunzi 50 kwa kipindi kimoja cha
wakati waliishi na kusoma Kiungani. Mitaala ilisisitiza heshima, elimu, imani
na michezo. Wanafunzi wazuri walifanywa kuwa walimu na wanafunzi bora kuliko
wote walifanywa kuwa mapadri.


Serikali ya Zanzibar ilitoa stempu mwaka 1963 kuadhimisha
historia ndefu ya uvumilivu wa kidini Zanzibar.

Picha hizi za Stempu, kutoka kushoto kwenda kulia,
Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph, Kanisa Kuu la Kristo,
Msikiti wa Malindi, Msikiti wa Hujjatul Islam,
Hekalu la Kihindi.
Wednesday, February 27, 2013
HISTORIA FUPI YA MAKANISA YA MWANZO YA ZANZIBAR
WARENO 1500 – 1800
Ukiristo uliletwa kwa mara ya mwanzo Zanzibar na Wareno.
Wareno wakielekea juu kutoka kusini baada ya kufanikiwa kuizunguka Rasi ya
matumaini mema – Cape of Good Hope katika mwaka 1488 walifanya jaribio la nguvu
la kudai bandari, njia za biashara na raslimali kiasi cha maili 2000 za mwambao
wa Afrika.
Mara tu ya kuwasili Zanzibar Wareno katika mwaka 1499
walianzisha Ujumbe wa Kanisa la Kikatoliki na kituo cha biashara ndani ya mji wa
Zanzibar. Wareno kwa miaka 200 iliyofuata walihodhi njia za baharini za meli za
Afrika Mashariki na walijitahidi kuanzisha msururu wa makaazi katika eneo la
mwambao. Mabaki ya makaazi ya Wareno bado yanaweza kuonekana karibu na
Fukuchani Kaskazini Unguja na Kisiwani Pemba. Ngome Kongwe ambayo ipo karibu na
bandari ya mji wa Zanzibar ilijengwa juu ya eneo lilipokuwepo kanisa dogo la
kikatoliki la mwanzo baada ya kutekwa na Jeshi la Oman. Jeshi hili la Oman
inasemekana liliitwa na wenyeji wa Zanzibar na Pemba ili kuwasaidia kuwangóa
Wareno waliokuwa makatili na madhalimu.
Baada ya miongo ya vita na maangamizo ambayo yaliyoshuhudi
kuwaka moto mji wa Mombasa, Wareno walirudi nyuma, na kurejea kuendea kusini,
mbali na mafikio ya mashambulizi ya moja kwa moja ambayo yaliyotokana na pepo za
miongo za jahazi (waarabu).
OASISI YA UVUMILIVU (OASIS OF TOLERANCE)
Katika mwaka 1841 mpiganaji wa Kioman/Oman Sultan, Seyyid
Said alivutiwa sana na visiwa hivyi vya Zanzibar kwa hiyo alihakikisha
anahamishia makao makuu yake Zanzibar kama ni mji mkuu. Malezi yake katika
maisha ya Jangwani yalimshajiisha yeye kwa nguvu zake zote kuviendeleza visiwa
hivyi vyenye ustawi. Sultan Seyyid Said aliona Zanzibar kama kama ni Oasisi
katika bahari. Alisimamia mipango mikubwa ya upandaji miti, alichimba visima
vya maji vyingi tu na kujenga nyumba nyingi ambazo zilitosha mamia ya wageni.
Sultan alitambua wageni watakaa na kujiliwaza katika Oasisi. Na alijua kwamba
biashara itakuwa na kufanyika katika eneo hili ikiwa litaimarishwa kwa vitu na
mambo mengine pamoja na usalama. Vile vile alitarajia na kutambua kwamba
angelipata asilimia fulani inayotokana na shughuli za kibiashara zitakazo
endeshwa Visiwani kama ni malipo ya kuviimarisha visiwa hivyi. Aliwakaribisha
na kuwaomba wafanyabiashara kutoka India kufungua matawi ya ofisi zao ndani ya
Zanzibar ili kuimarisha biashara. Wafanyabishara hawa wengi kutoka India
walikuwa ni raia wa kiingereza hii ilikuwa ni kwa sababu ya kutekwa India na
Uingereza. Kwa maana hiyo, alianza kuwakaribisha maofisa wa kiingereza visiwani
ili kuwakilisha maslahi ya raia hawa wahindi wa kiingereza. Mara tu tena baadae
alianza kuingia katika mikataba rasmi ya kibiashara na Serikali ya kiingereza na
Serikali nyengine za Magharibi.
Majengo ya biashara yalijengwa ndani ya Mji Mkongwe na
Kampuni za Kimarekani, Kijerumani, Ufaransa na na Kiingereza. Bandari ya
Zanzibar ilitoa huduma za fueli na kufanyia
matengenezo
Meli za kivita na vyombo vya usafiri vya wafanyabiashara. Meli hizi zilileta
mapote ya ziada ya watu wa magharibi ndani ya Zanzibar. Kama ni makaribisho
mema ya wageni wengi katika Oasisi yake. Sultani aliruhusu watu wa imani zote
kuendesha shughuli zao za kidini walivyopenda.


1800 – 1900
WAKATOLIKI, MAKUNDI YA WAKIRISTO WASIOPENDA MIKUTANO ASMI, VITA AU GHASIA (QUAKERS) NA UJUMBE WA VYUO VIKUU KWA AFRIKA YA KATI ( UMCA)
Baada ya Wareno kurudi nyuma Wakiristo kidogo tu Wakigoa
ndio waliobakia Zanzibar.
Wakiristo
hawa hawakuwa na kanisa la kufanyia Ibada lakini waliweza kuifanya hai jumuia
yao kwa kwa kuifanya ibada zao kibinafsi. Baadae katika miaka 1800 makundi ya
watu wa wamagharibi yalianza kujumuisha wamisionari na wachungaji wamisionari
waliokuwa wakipita pita mara chache na wachungaji katika meli bandarini. Katika
mwaka 1844 wamisionari wa kikiristo zaidi wa kudumu waliwasili Afrika mashariki
kwa kupitia mchungaji wa kilutheri Joseph Krapf na wafuasi wawili ambao
walifanya kazi kwa ajili wa Jumuia ya kimisheni ya kanisa la kiingereza (English
Church Missionary Society). Wakifanyakazi, Mombasa, walitembelea Zanzibar na
miaka michache mbeleni walitoa kamusi bora kabisa la Kiswahili lakini hawakuwahi
kuanzisha kanisa ndani ya visiwa hivyi.


Hotuba zake zilipelekea kuundwa kwa ujumbe wa Vyuo Vikuu
kwa Afrika ya Kati (UMCA). Ujumbe wa Vyuo Vikuu kwa Afrika ya Kati ulikuwa ni
mashirikiano baina ya kitivo na wanafunzi waliopitia vyuo vikuu vya Oxford and
Cambridge, ambao baadae tu waliungana na mashabiki kutoka vyuo vikuu vya Durham
na Dublin. Katika mwaka 1860 walimchagua Charles Mackenzie kama ni “Askofu wa
Afrika ya kati” na ilipofikia mwezi wa Oktoba wa 1860 alikuwa njiani kuelekea
huko Afrika ya Kati.
Lengo la ujumbe wa vyuo vikuu kwa Afrika ya kati (UMCA)
lilikuwa ni kufikisha dini ya kikiristo kwa watu wengi sana waliokuwa Afrika ya
Kati, kuzunguka ziwa Nyasa, ambalo Livingstone alilizungumzia kwa ufanisi. Kwa
ajili hiyo, baada ya kufika Afrika Kusini Askofu Mackenzie na wafuasi aliokuwa
nao walisafiri kwa boti mpaka mto Zambezi na baadae hadi mto shire kuasisi
ujumbe wa mwanzo wa ujumbe wa vyuo vikuu kwa Afrika ya Kati katika Afrika katika
sehemu iliyojulikana kama Magomero.
Wakati ujumbe huu na eneo lake ulichukuana na jina na ari
ya jumuia mama, Ujumbe huu ulishuhudia kushindwa kwa aina yake kutekeleza
malengo yake. Maradhi na njaa na ukame uliwakumba wamisionari wa mwanzo na
kupelekea kufa kwa askofu. Kundi hili lililazimika kuondoka katika eneo hilo
ndani ya kipindi
cha miaka mitatu kwa sababu eneo hilo lilikuwepo mbali sana
na upatikanaji wa bidhaa kutoka nje na vituo vya mawasiliano, eneo hilo halikuwa
na mazingira mazuri ya kiafya kwa wale ambao hawana uzoefu na mazoea na hali ya
hewa ya hapo na pia eneo halikuwa na utulivu wa kisiasa. Askofu mpya, George
Tozer, kwanza alijaribu kuupeleka ujumbe maili 200 mafikio ya mtiririko wa mto
kuelekea eneo la muanuko lakini hata hivyo eneo hilo mara tu liligundulika kuwa
halikuwa na mazingira mazuri ya kiafya na kwa hiyo lilihamwa kwa miezi hivi tu.
Wakichukua bidii za makusudi, ili kutorejea makosa
yaliyopita viongozi wa ujumbe wa Vyuo Vikuu kwa Afrika ya Kati (UMCA)
waliangalia uwezekano wa kituo au eneo jengine ambalo litatumika kuweza kufika
kati kati ya Afrika. Maeneo mbali mbali yalifikiriwa kutumika kama Kisiwa cha
Johanna, maeneo katika mwambao wa Afrika Kusini lakini kwa bahati Zanzibar
ilikubalika kutumika kutokana na muundo mzuri wa njia za mawasiliano,
upatikanaji mzuri wa bidhaa za chakula na wingi wa upatikanaji nguvu kazi bora.
Ujumbe wa Vyuo Vikuu kwa Afrika ya Kati (UMCA) uliobakia uliwasili Zanzibar
tarehe 31/08/1864.

Click here: Kuendelea ..........
Tuesday, February 26, 2013
Kwaresima ni kipindi cha toba, matendo ya huruma na utii kwa maagizo ya Mwenyezi Mungu
Wakati huu wa Kipindi cha Kwaresima sanjari na Maadhimisho ya Mwaka wa Imani, kutubu na kumwongokea Mwenyezi Mungu, tayari kuanza hija ya maisha mapya, kwa kumtii Mwenyezi Mungu. Inafahamika kuwa, Imani bila matendo hiyo imekufa ndani mwake! Kumbe, kuna haja kwa waamini kumwilisha imani yao kwa Kristo na Kanisa lake kwa njia ya matendo ya huruma kwa maskini na wote wanaosukumizwa pembezoni mwa Jamii, kila mtu akijitahidi kuwa kweli ni Msamaria mwema kwa jirani yake. Ni mwaliko wa kuwa na mwono mpana zaidi kwa kuwaangalia wote wanateseka kutokana na majanga asilia, vita na madhulumu.
Kwaresima kiwe ni kipindi cha maandalizi ya kina katika Maadhimisho ya Fumbo la Pasaka, yaani, mateso, kifo na ufufuko wa Kristo. Kwaresima iwawezeshe waamini kujenga fadhila ya imani, matumaini na mapendo katika Fumbo la Ufufuko wa Kristo, ili hatimaye, kuweza kulitolea ushuhuda. Imani ya Wakristo wa mwanzo ilijikita katika Ufufuko, wakaliona Kaburi wazi, hapo ukawa ni mwanzo wa Habari Njema ya Wokovu inayojikita katika: maisha, maneno na matendo ya Yesu Kristo kwa ajili ya wokovu wa mwanadamu kutoka katika lindi la dhambi na mauti.
DEKANIA YA MT.GASPER DE BUFALO-KUNDUCHI
Dekania ya Mt Gasper inazijumuisha parokia zilizipo
Mbezi Beach, Kunduchi, Tegeta, Boko na Bunju.
Dekania Hii inajumla ya Parokia kumi mpaka sasa:
Parokia ya Bikira Maria Mama wa Huruma -Mbezi Beach
parokia ya Mt. Dominick - Mbezi Juu
Parokia ya Mt. Gasper De Bufalo- Mbezi Chini(Machakani)
Parokia ya MT. Agustino -Salasala
Parokia Mt. Nicolous- Kunduchi
Parokia ya Damu Takatifu-Tegeta
Parokia ya Mt.Adrea Bahari Beach
Parokia ya Madale
Parokia ya Mwenye Heri Isidori Bakanja -Boko
Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Karmel - Bunju
Ndani ya Dekania hii kuna Vituo vya Hija viwili(2)
Kituo cha Hija ya Vijana Jimbo la Dar es salaam- Parokia ya Boko
Kituo cha Hija ya Shirika la Damu Takatifu ya Yesu - Parokia ya Mt. Gasper- Mbezi Beach
HISTORIA YA UJENZI WA KANISA LA MBULU
Shujaa wetu: Franz Wesinger-Mhandisi aliyejenga kanisa Katoliki Mbulu
Mwaka 2003, akiwa na miaka 75 mhandisi Franz Wesinger ambaye pia ni msanifu wa majengo alirudi Tanzania kwa ajili ya kupanga ujenzi wa kanisa jipya la Katoliki Arusha na ni katika kipindi hicho ambacho mapadre wawili wa kanisa Katoliki jimbo la Mbulu walikumbwa na kashfa ya ufisadi kama baada ya kufuja jumla ya Shilingi za Kitanzania Milioni 340 kwa bei ya 1000 kubadili dola moja wakati huo (dola 340,000). Mapadre hao, msaidizi wa askofu (Vicar General) John Nada na father Melkiadus Qameyu wa parokia ya Dareda walituhumiwa kupoteza kiasi hicho cha fedha baada ya kutapeliwa na mganga wa kienyeji aliyefahamika kwa jina la Mohamed mrisho kuwa angeziongeza mara mbili....mafaza wakaingia mkenge...
Turudi kwa Franz Wesinger, huyu bwana alifanya mahojiano na gazeti la Arusha Times mwaka 2003 na haya ni sehemu ya maelezo yake kuhusu ujenzi wa Kanisa hilo
"Katika miaka 15 iliyopita, Jimbo la Mbulu limepiga hatua kubwa sana. Jitihada za awali za marehemu Askofu Hhando zimezaa matunda kwani walianza kidogo au kusema ukweli halisia walianza bila fedha lakini waliweka imani yao kwa Mungu huku wakitumia msaada kidogo kutoka kwa wamihionari kutoka Ulaya na ujenzi ulianza. Amini usiamini, walianza ujenzi wakitumia sepetu lililovunjika na toroli la mbao. Kanuni kuu ilikuwa kubana matumizi na kuhudumu (huduma) pamoja kukawa kichocheo kikubwa katika jimbo zima kumtumikia Mungu" alisema Franz
"Hata baada ya ujenzi na kanisa kuwekwa wakfu zilibaki kontena 12 zikiwa zimejaa vifaa vya ujenzi, mashine, magenerata, jukwaa kubwa, magari mawili na lifti (cranes) bila kutumika"
"Kuna tofauti kati kuhudumu kwa imani na kutumaini kupata faida pasipo kufanya kazi" aliongeza Franz akizungumzia ufisadi uliotokea Mwaka moja baada ya ujenzi wa kanisa hilo kukamilika.
"Hata wana wa Israeli walimsahau Mungu na kuabudu ndama wa dhahabu baada ya Mungu kuwatoa utumwani mwa Wamisri na kuwapitisha katika bahari ya Shamu"
"Waisraeli walikombolewa lakini walitaka kupata faida pasipo kufanya kazi, hauwezi kumtumikia Mungu kwa ulanguzi"
Franz Wesinger alieleza kuwa anajisikia fahari kubwa sana moja ya sehemu maskini zaidi Tanzania ina Kanisa kubwa zaidi na zuri zaidi nchini na kuona fahari kuwa imejenga hilo kanisa lenyewe kwa msaada pekee wa Mungu"
Chini ya usimamizi wa Franz Wesinger ujenzi wa kanisa hili ambalo leo ni fahari kubwa kwetu ulikamilika kwa ufanisi wa hali ya juu na kutimiza ndoto ya aliyekuwa Askofu wa Jimbo Kuu la Mbulu Marehemu Hhando. Franz Wesinger anatoa funzo la uaminifu na kuacha "legacy" kwa vizazi vijavyo. Sina uhakika kama bado yupo hai lakini Franz Wesinger alifanya kazi kubwa sana tofauti na "wahandisi" wetu ambao ninauhakika kisingebaki kitu baada ya ujenzi na katu kazi ya ujenzi wa kanisa hilo usingekamilika.
MATANGAZO YA JUMA TAREHE 02-03/03/13
JUMAMOSI TAREHE 02/03/2013
- Kutakuwa na mafungo ya jubilee ya Miaka 200 ya Shirika la Damu Takatifu, Mafungo hayo yatafanyikia katika kituo cha Hija cha Shirika kilichopo Parokia ya Mt. Gasper De Bufalo Mbezi Beach na yataanza saa 2:00 asubuhi.
- Kamati tendaji ya VIWAWA Kigango cha Mt. Rafael Mbweni Malindi watafanya kikao saa kumi na moja jioni Kigangoni...Pia Vijana wote wanakumbushwa kufika saa kumi Jioni kwa ajili ya Mazoezi ya Kwaya.
JUMAPILI TAREHE 03/03/2013
RATIBA ZA IBADA ZA MISA TAKATIFU
KIGANGO CHA BOKO.
MISA YA KWANZA 12:30-2:00 ASUBUHI
MISA YA PILI SAA 2:00-4:00 ASUBUHI
MISA YA TATU SAA 4:00-5:30 ASUBUHI
KIGANGO CHA MBWENI
MISA YA KWANZA SAA 2:00-4:00 ASUBUHI
MISA YA PILI SAA 4:00-5:30 ASUBUHI
KIGANGO CHA MT. RAFAEL-MBWENI MALINDI
SAA 2:00-4:00 ASUBUHI.
KIKAO CHA HALMASHAURI YA VIWAWA PAROKIA
KIKAO CHA HALMASHAURI YA VIWAWA PAROKIA
Halmashauri ya VIWAWA Parokia watakuwa na Kikao mara baada ya Misa ya Pili Saa 4:00 asubuhi kikao kitafanyikia Parokiani Boko wajumbe wote mnatakiwa kufika Bila kukosa.
Subscribe to:
Posts (Atom)
-
Mkoa wa Njombe ni moja kati ya mikoa Tanzania, ukiwa umeanzishwa rasmi mwaka 2012. Umepakana na mikoa ya jirani ya Morogoro, Ruvuma, Mbeya...
-
Shujaa wetu: Franz Wesinger-Mhandisi aliyejenga kanisa Katoliki Mbulu Kanisa la Mbulu ndilo kanisa kubwa kuliko yote Tanzania na la ...
-
MAJIMBO YA ILALA, SEGEREA NA UKONGA – CCM ITAKUWA NA WAKATI MGUMU Halmashauri ya Manispaa ya Ilala ipo kati ya Latitudo 6 na 7 kusini mwa I...