Saturday, March 9, 2013

HISTORIA YA JIMBO LA MOROGORO

Jimbo Katoliki la Morogoro Historia
Historia Fupi ya Jimbo
-         Jimbo la Morogoro lilizaliwa Machi 25, 1953 na Mhasham Bernard Hilhorst alikuwa askofu wake wa kwanza.
-         Hata hivyo, historia ya Jimbo la Morogoro inaanza karne ya 19 katika miaka ya 1860. Mapema mwaka 1858 Askofu Amandus R. Maupoint wa Jimbo Katoliki la Mtakatifu Denis, Reunion alifanya makao yake Kisiwani Unguja. Miaka miwili baadaye Wamisionari wengine walikuja Unguja kufanya uinjilishaji.   Baada ya miaka michache ilionekana ilifaa kazi ya uinjilishaji Unguja ikabidhiwe kwa Shirika la Kidini lenye uzoefu. Shirika la Mapadri wa Roho Mtakatifu walikabidhiwa jukumu hilo.
-   Novemba 12, 1862  Unguja  ilipandishwa hadhi toka “Mission Territory”  na kuwa “Apostolic Prefecture of Zanguebar.”  Unguja  ikapata Msimamizi wa Kitume chini ya  Mamlaka ya Askofu Maupoint.
-         Juni 16, 1863  Mapadri  Anthony Horner na Edward Baur na Mabradha  Celestine na Felician wa Shirika la Roho Mtakatifu waliingia Unguja na  Baadaye mwaka 1868 Wamissionari  hao waliongozwa na Padre Horner   walifika Bagamoyo mara ya kwanza Machi 4, 1868.
-         “Apostolic Prefecture of Zangueber, kama eneo la Kitume lilivyojulikana siku hizo, lilikuwa ni pamoja na Kisiwa cha Unguja na ukanda wa mashariki kuanzia Guardafui hadi Cap Delgado, yaani eneo lote la Afrika ya Mashariki.
-         “Prefecture”  hiyo iligawanywa katika sehemu mbili kuu Wamisionari wa Afrika yaani “White Fathers”walipoingia Unguja April 29, 1878. Hivyo, sehemu iliyojulikana kama ya Maziwa Makuu ambayo ilikuwa ni pamoja na Nyanza ambayo kwa sasa ni Jimbo Kuu la Mwanza, Musoma, Shinyanga na Geita; Tanganyika, ambayo ni Majimbo ya Kigoma, Sumbawanga na Mbeya na Congo ilikabidhiwa kwa Mapadri hao wapya, Wamisionari wa Afrika. Na sehemu iliyobaki ilikuwa bado chini ya Shirika la Roho Mtakatifu.
-         Mwaka 1887 sehemu ya “Prefecture” ambayo sasa ilipata hadhi ya kuitwa “Vacariate” of  “Zanguebar” nayo ikagawanywa katika sehemu kuu tatu:
(a)   Zanguebar Kaskazini na Nairobi. Hii ilijumlisha Mombasa.
(b)  Zanguebar Kusimi, yaani Kilwa na Mzizima au Dar es Salaam.
(c)  Zanguebar Kati, ambayo mwaka 1906 iliitwa Vicariat ya Bagamoyo.
-         Zanguebar Kusini ilikabidhiwa kwa Wamisionari Wabenediktini. Ilikuwa na hadhi ya “Prefecture.”
-         Mwaka 1910 Vikariat ya Bagamoyo iligawanywa tena katika sehemu mbili, yaani Vikariat ya Kilimajaro na Vikariat ya Bagamoyo. Zote zilikuwa chini ya Shirika la Roho Mtakatifu.
-         Mwaka 1934 Vikariat ya Dodoma  ilizaliwa, sehemu ilimegwa toka Vikariat ya Dar es Salaam na Vikariat ya Iringa, na sehemu nyingine ilimegwa toka Vikariat ya Bagamoyo.
-         Mwaka 1950 Vikariat ya Bagamoyo ikamegwa na kuunda Vikariat ya Tanga na miaka mitatu baadaye, yaani Machi 25, 1953 wakati Majimbo yalipoundwa Tanganyika, Vikariati ya Bagamoyo iliyobakia ikapata hadhi ya Jimbo na kuwa Jimbo la Morogoro wakati Dar es salaam ikainuliwa na kupata hadhi ya kuwa Jimbo Kuu la Dar es salaam.  
Maaskofu wa Morogoro  
-         Tangu kuanzishwa kwake kama Vikariat ya
Bagamoyo mwaka 1906, wafuatao ndio Maaskofu Wake:  
Askofu Raoul De Courmont (1883 - 1896)
Askofu Emille Allgeyer (1897 - 1906)
Askofu F.X.Vought (1906 – 1923)  
Askofu B.Wilson (1924 – 1933)  
Askofu Bernard Hilhorst (1934 – 1954)
Askofu Herman V.Elswijk (1954 – 1967)  
Askofu Adrian Mkoba (1967 – 1992)  
Askofu Telesphor Mkude (1992 sasa)
-         Mhasham Adrian Mkoba ndiye Askofu wa kwanza  Mzalendo wa Morogoro.
    

  Hali ya Kijiografia  
-         Jimbo Katoliki la Morogoro limeundwa na eneo lipatalo kilomita za mraba 43,380 kusini mashariki mwa Jamhuri ya Tanzania. Jimbo la Morogoro limeundwa kutokana na Wilaya za Serikali tano, yaani Morogoro Mjini, Morogoro Vijijini, Kilosa, Mvomero, na Bagamoyo. Wilaya ya Bagamoyo ni sehemu ya Mkoa wa Pwani Kiserikali, wakati Wilaya nne zilizobaki zipo katika Mkoa wa Morogoro.
-         Makao Makuu ya Mkoa wa Morogoro yapo katika Manispaaa ya Morogoro. Vile vile katika Manispaa hii yanapatikana Makao Makuu ya Jimbo la Morogoro, Kanisa Kuu la Jimbo, na Makao ya Askofu wa Jimbo.  
Wakazi wa Jimbo  
-        Jimbo la Morogoro lina wakazi wapatao 1,559,271.  Kati ya hao wakatoliki ni 638,591.
-         Ni asilimia ishirini (20%) tu ya wakazi wa Jimbo la Morogoro wanaishi mijini, wakati asilimia kubwa, yaani 80%, wanaishi vijijini.
-  Makabila asilia yanayopatikana Jimboni Morogoro ni Waluguru, Wanguu, Wakutu, Wazigua,  Wakami, Wakaguru, Wavidunda, Wasagara, Wakwavi, Wakwere, Wazaramo na Wadoe,
-         Mbali ya makabila haya asilia, Jimbo la Morogoro lina wahamiaji vile vile. Makundi haya ya wahamiaji wengi wao ni Wachaga, Wamasai, Wangoni na Wagogo.
-         Kila kabila lina lugha yake ya asili. Hata hivyo, Kiswahili kinatumika katika sehemu zote katika Jimbo la Morogoro

MASHIRIKA YALIYOPO JIMBO LA MOROGORO
Vito mbalimbali katika taji la dhahabu ambalo Kristo amempamba Bibiarusi wake. Au fungu zuri la maua ya kila rangi. Ni mifano miwili iliyotumika kuelezea wingi wa mashirika ya kitawa ndani ya Kanisa Katoliki. Jimbo la Morogoro ni mojawapo kati ya yale yanayofurahia zaidi neema kubwa namna hiyo.
Tukirudi nyuma hadi karne ya XIX , tunakuta kwamba watawa wa Roho Mtakatifu (Holy Ghost Fathers) ndio waanzilishi wenyewe wa Kanisa nchini, wakitokea Zanzibar na Bagamoyo, na kufuatwa muda si mrefu baadaye na masista kutoka kisiwa cha RĂ©union (Filles de Marie) Hivyo tangu awali watawa wamekuwa mstari wa mbele sio tu katika maisha ya Kiroho, bali pia katika umisionari.
Mwanzo mgumu: kwa miaka mingi mashirika hayo yaliinjilisha wakistahimili tabu na hari za mchana, mpaka watawa wengine hasa wananchi, tunda la kazi yao, wakaja kuwaunga mkono kwa saa tofautitofauti.
Masista wengi wa nchi nzima wanafahamu sana jimbo hili kwa sababu waliwahi kusoma Bigwa, katika sekondari iliyoanzishwa kwa ajili yao na Umoja wa Mama Wakuu Tanzania (ambao kwa sasa unakamilisha ujenzi wa kituo kingine cha malezi ya pamoja si mbali na shule hiyo).
Hatua mpya ya uwepo wa mashirika jimboni ilipigwa pale ambapo Wasalvatoriani kisha kupatana na mashirika mengine walichagua Morogoro kama mahali pa kujenga seminari kuu ya kitawa ambayo kwa sasa ni Taasisi ya Falsafa na Tauhidi (wengine wanafikiria kuigeuza tena iwe Chuo Kikuu chenye vitivo mbalimbali). Hayati Askofu Adriani Mkoba alifungua milango ya jimbo kulipokea kila shirika litakalohitaji watawa wake wasomee huko. Tangu hapo ujenzi na malezi havijakoma katika eneo la mlima Kola, kwenye barabara ya Dar es Salaam. Yeyote anayepita anajionea maendeleo hayo na kuzungumzia aina hiyo ya Vatikano chini ya milima ya Uluguru.
Mvuto wa taasisi hiyo ndio sababu kuu ya mashirika kumiminika Morogoro miaka ya mwisho; lakini ukianza kuelekea Dodoma, kwenye eneo la Kihonda unakuta vilevile mashirika mengi, ingawa majengo yao yamefichikafichika kati ya nyumba za wananchi.
Kwa jumla sasa hivi jimbo lina mashirika zaidi ya 30 ya kila aina: ya wanaume na ya wanawake, ya kikleri na ya kilei, ya maisha ya wakfu na ya maisha ya kitume, ya kipapa na ya kijimbo. Inakosekana bado monasteri ya maisha ya sala tu, ingawa Askofu Telesphor Mkude ana hamu nayo.
Mhashamu akiona kwa furaha kubwa ongezeko hilo ambalo linaendelea haraka, mwanzoni mwa Jubilei kuu ya mwaka 2000, pamoja na kumteua kwa mara ya kwanza makamu wake maalumu kwa maisha ya wakfu aliamua kuunganisha mashirika hayo yote katika ASSICAL (Association of Institutes of Consecrated and Apostolic Life – Morogoro Diocese) ili yaweze kufahamiana na kubadilishana mawazo, mang’amuzi, matarajio na mipango hasa upande wa malezi na wa utume.
Tangu hapo utume huo unazidi kuimarika kwa njia ya mikutano na adhimisho la pamoja la sikukuu ya watawa iliyoanzishwa na Papa Yohane Paulo II kwenye tarehe 2 Februari ya kila mwaka. Kwa kweli ni tukio la kufurahisha kuona mamia ya watawa wa mabara karibu yote kushangilia miito yao mbalimbali kwa ajili ya ufalme wa mbinguni. Lakini siku moja haiundi mwaka. Kuna siku nyingine 364 ambazo ni nafasi ya kila mtu kumshukuru Mungu kimatendo kwa karama aliyomjalia. Uaminifu wa kila sasa ndio unaothibitisha kwamba neema inapokewa kwa mikono miwili badala ya kuchezewa. La sivyo adhimisho halina maana. Changamoto hiyo ipo daima mbele ya kila mmoja na ya kila jumuia, kwa sababu maisha ya kitawa ni ya kulenga utakatifu pamoja na wengine, sio kibinafsi.
Mbali ya utakatifu, mashirika yanalenga kutoa mchango katika Kanisa na katika jamii, kila moja kadiri ya karama yake. Ingawa nguvu nyingi za mashirika mbalimbali yaliyohamia jimboni kwa ajili ya malezi zinaishia katika kazi hiyo ya msingi, tunaweza kusema nia ya kufanya kitu hata nje ya nyumba ipo. Kadiri ushirikiano unavyostawi, njia zinaonekana, kwa sababu penye nia pana njia.
Mahitaji ya jimbo hasa ni mengi, kama kawaida. Hivyo mapadri na walei wanatazamia sana kufaidika na uwepo wa umati huo wa waamini wenzao waliojitoa kabisa kwa maisha ya wakfu na ya kitume. Baadhi ya mashirika yana nyumba zisizo za malezi, nazo ndizo zinazoitikia zaidi mahitaji hayo. Kwa namna ya pekee Masista wa Moyo Safi wa Maria wa Morogoro, ambao ndio wengi, wanahudumia parokia, shule na zahanati nyingi jimboni kote.
Mungu atujalie sisi sote kushika kwa unyenyenyeku nafasi aliyotupangia katika kufikisha watu kwenye uzima wa milele.  

1. MASHIRIKA YA MAISHA YA WAKFU

 

1.1. Mashirika ya Kitawa

 

1.1.1. Ya Kiume

 
1.      Ndugu Wafransisko Wakonventuali – SLP 932 – Morogoro
Simu: +023/0784594072 – Barua pepe: krzcie@yahoo.com – Tovuti: www.ofmconv.org

2.      Ndugu Wafransisko Wakapuchini – SLP 900 – Morogoro
Simu: +023/2603204 – Barua pepe: kolafriars@yahoo.comTovuti: www.ofmcap.org

3.      Ndugu Waagustino – SLP 1947 – Morogoro
Simu: +023/2604773 – Barua pepe: osamorogoro@yahoo.comTovuti:

4.      Wakarmeli OCD – SLP 363 – Morogoro
Simu: +023/2603800 – Barua pepe: ocdtzmission@yahoo.com – Tovuti:

5.      Shirika la Roho Mtakatifu – SLP 16 – Bagamoyo
Simu: +023/2440063 – Barua pepe: eap@habari.co.tzTovuti

6.      Wamisionari wa Mt. Francis wa Sales – SLP 12 – Morogoro
Simu: +023/2600036 – Barua pepe: msfsmoro@africaonline.co.tz – Tovuti: www.fransalians.com
7.      Shirika la Madonda Matakatifu (Wastigmatini) – SLP 2213 – Morogoro
Simu: +023/2603523 – Barua pepe: stigmatines@morogoro.netTovuti: www.stigmatines.com

8.      Wamisionari Wana wa Moyo Safi wa Maria (Waklareti) – SLP 427 – Morogoro
Simu: +023/2600429 – Barua pepe: cmfmorobarbastro@yahoo.com – Tovuti: www.claret.org
 
9.   Wasalesiani wa Don Bosco – S.L.P. 4045 – Morogoro – Simu: +0764–854602 – Barua pepe:   – Tovuti:
 
10. Wasalvatoriani – SLP 1878 – Morogoro
Simu: +023/2600897 – Barua pepe: sdsschol@go2.pl – Tovuti: http://www.sds–ch.ch/africa
 
11. Wamisionari wa Consolata – SLP 769 – Morogoro
Simu: +023/2603563 – Barua pepe: allasemi@morogoro.netTovuti: http://www.consolata.org
 
12. Shirika la Misheni (Wavinsenti) – SLP 6051 – Morogoro
Simu: +023/2600029 – Barua pepe: depaulmoro04@yahoo.com – Tovuti:

13. Mabradha wa Elimu ya Kikristo wa Mt. Gabrieli (Wamontfort) – SLP 1124 – Morogoro
Simu: +023/2602204 – Barua pepe: montmoro@africaonline.co.tz – Tovuti:
 
 
1.1.2. Ya Kike
 
1.      Mabinti wa Maria (wa St. Denis)– SLP 230 – Bagamoyo
Simu: 023/2440417 – Barua pepe: dmdestdenistan@yahoo.fr – Tovuti:
2.      Masista Wamisionari wa Damu Takatifu – SLP 865 – Morogoro
Simu: +023/2604655 – Barua pepe: – Tovuti:

3.      Shirika la Moyo Safi wa Maria (wa Morogoro) – SLP 1049 – Morogoro

Simu: +023/2603591/2604314 – Barua pepe: mgololesisters@intafrica.com – Tovuti:
4.      Masista wa Msalaba Mtakatifu (wa Chavonod)– SLP 1677 – Morogoro
Simu: +023/2603328 – Barua pepe: holycross@africaonline.co.tz – Tovuti:

5.      Masista Watersiari Wakapuchini wa Familia Takatifu – SLP 1989 – Morogoro
Simu: +023/2604845 – Barua pepe: htctanz@hotmail.comTovuti
:
6.      Masista wa Mt. Anna (wa Luzern) – SLP 1807 – Morogoro
Simu: +023/2601550 – Barua pepe: stannsmoro@africaonline.co.tzTovuti:

7.      Masista Wakolejina wa Familia Takatifu – SLP 945 – Morogoro
Simu: +023/2600424 – Barua pepe: collemoro@hotmail.com – Tovuti:

8.      Masista wa Maria Imakulata (wa Krishnagar) – SLP 2028 – Morogoro
Simu: +023/2604066 – Barua pepe: smimoro@africaonline.co.tzTovuti:

9.      Masista wa Mama wa Karmeli – SLP 1302 – Morogoro
Simu: +023/2600359 – Barua pepe: – Tovuti:

10. Masista wa Mt. Gemma – SLP 304 – Morogoro
Simu: +0784/457358 – Barua pepe: – Tovuti:
 
11. Masista Waursula wa Yesu Mteswa – SLP 1048 – Morogoro
Simu: +0756/937297 – Barua pepe: – Tovuti:

12. Masista wa Sakramenti Kuu – SLP 2135 – Morogoro
Simu: +023/2602902 – Barua pepe: – Tovuti:

13. Mabinti wa Mt. Fransisko wa Sales – SLP 640 – Morogoro
Simu: +023/2600900 – Barua pepe: dsfstanzania@rediffmail.comTovuti:

14. Masista wa Maria Imakulata (wa Wroclaw) – SLP 1878 – Morogoro
Simu: +0787/759496 – Barua pepe: – Tovuti:

15. Masista wa Mt. Yosefu (wa Annecy) – SLP 58 – Dumila
Simu: +0745/214343 – Barua pepe: agnesadampukulam@yahoo.com – Tovuti:
 
16. Masista wa Mt. Yosefu (wa Chambery) – SLP 135 – Mikumi
Simu: +0787/710338 – Barua pepe: – Tovuti: www.csjchambery.org
 
17. Masista wa Bikira Maria Malkia wa Mitume – SLP 1925 – Morogoro
Simu: +023/2604165 – Barua pepe: – Tovuti:
 
18. Masista wa Mt. Anna (wa Bangalore) – SLP 363 – Morogoro
Simu: +023/603800 – Barua pepe: – Tovuti:

19. Masista Waabuduo Damu ya Kristo – SLP 6508 – Morogoro
Simu: – Barua pepe: – Tovuti:
 
20. Dada Wadogo wa Mt. Fransisko – SLP 1878 – Morogoro
Simu: +0787/759496 – Barua pepe: – Tovuti:
 
21. Masista Wabenedikto Waafrika wa Mt. Agnes – SLP 6015 – Morogoro
Simu: +0784/464024 – Barua pepe: mlowevicky@yahoo.com – Tovuti:
 
22. Masista wa Mt. Karolo Borromeo – SLP 1232 – Morogoro
Simu: +0732/931181 – Barua pepe: – Tovuti:
 
23. Masista Warosmini wa Maongozi – SLP 133 – Morogoro
Simu: +0787/024621 – Barua pepe: – Tovuti:

24. Masista wa Maryknoll – SLP  – Morogoro
Simu: – Barua pepe: – Tovuti:
 
25. Masista Wafransisko wa Upendo – S.L.P. 6083 – Morogoro
Simu: – Barua pepe: – Tovuti:
 
 
 

1.2. Mashirika ya Kilimwengu

 
1.2.1. La Kiume
 
1.      Mapadri wa Shirika la Kilimwengu katika Kazi ya Roho Mtakatifu – SLP 640 – Morogoro
Simu: +023/2603340 – Barua pepe: – Tovuti:
 
 
1.2.2. Ya Kike
 
1.      Unitas kwa Afrika – SLP 1003 – Morogoro
Simu: +023/2600138 – Barua pepe: – Tovuti:
2.      Masista wa Grail – SLP 6090 – Morogoro
Simu: +023/2613690 – Barua pepe: – Tovuti:
 
 
 

2. MASHIRIKA YA MAISHA YA KITUME

 

2.1. Ya Kiume

 
1.      Wamisionari wa Damu Azizi – SLP 1925 – Morogoro
Simu: +023/2604165 – Barua pepe: stgascoll @yahoo.com – Tovuti: www.cpps–preciousblood.org

2.      Jumuia ya Mapadri katika Kazi ya Roho Mtakatifu – SLP 1935 – Morogoro
Simu: +023/2601353 – Barua pepe: – Tovuti:
 
 
2.2. La Kike
 
1.      Jumuia ya Masista katika Kazi ya Roho Mtakatifu – SLP 6038 – Morogoro
Simu: +023/2601764 – Barua pepe: – Tovuti:
 
 
 
3. TAASISI ZA MALEZI YA PAMOJA KATI YA MASHIRIKA YA KIKE
 
1.      Sekondari ya Masista ya Bigwa – SLP 369 – Morogoro
Simu: +023/2603066 – Barua pepe: bigwasrs@yahoo.com – Tovuti:

2.      Kituo cha Malezi ya Masista cha Kola – SLP 913 – Morogoro
Simu: +023/2600658 – Barua pepe: tcastanzania@hotmail.com – Tovuti:
 
 
 
4. CHAMA (CHA WANAUME NA WANAWAKE)
 
1.      Ndugu Wadogo wa Afrika – SLP 6083 – Morogoro
Simu: – Barua pepe: unwa@unwa.tk Tovuti: www.unwa.tk
 


UCHAGUZI WA PAPA 2013


Masuala ya Jamii

Makadinali wakutana vatikani

Makardinali wa kanisa Katoliki kutoka sehemu tofauti za dunia,wameanza utaratibu wa kumchagua mrithi wa Papa Benefickt wa XVI aliyejiuzulu mwezi uliopita.
Zoezi hilo limeanza leo Vatican saa 3.00 asubuhi kwa saa za Vatican sawa na saa 6 mchana kwa saa za Afrika Mashariki kwenye ukumbi wa New Synod Hall.
Mkutano huo ndio utafungua mchakato wa uchaguzi wa Papa mpya na unatarajiwa kuandaa ratiba ya uteuzi wa papa mpya.Makardinali hao ndio watapanga siku ya kufanyika mkusanyiko wao unaoitwa `Papal Conclave' kwa ajili kufanya uchaguzi huo.
Kutokana na utaratibu wa kanisa Katoloki, uchaguzi wa Papa hutakiwa kufanyika siku 15 hadi 20 kufuatia siku kiti cha papa kilipoanza kuwa kitupu na Uchaguzi kwa kawaida hufanyika katika Kanisa la Sistine Chapel.
Takribani makardinali 115 kutoka nchi mbalimbali duniani,wanahusika na uchaguzi huo wa Papa ambapo Kati ya hao, makardinali 67 waliteuliwa na Papa Benedict,Joseph Aloisius Ratzinger.
Kwa upande wake aliyekuwa papa ambaye ni mzaliwa wa Ujerumani amekuwa akitumia muda kufanya ibada, kusoma vitabu na meseji za kumtakia kila la kheri papa aliejuzulu kutoka sehemu mbalimbali duniani na kutafakari.
Hadi sasa hakuna tarehe yoyote iliotajwa kuhusu uchaguzi huo wa papa ingawa vyanzo vya habari vya Italan vimedokeza kuwa huenda Machi 11 2013 ikawa siku hiyo ya uchaguzi wa papa.
Kiongoazi wa chuo cha makardinali Angelo Sodano ameongea kuwa siku maalumu ya kuanza kwa uchaguzi huo,haitatajwa hadi hapo makardinali wateule wote watakapo wasili mjini Rome
Papa mpya atatokea bara gani?

Kadinali Ricardo Jamin Vidal wa Philippines(kulia) na Luis Antonio Tagle wamewasili kuhudhuria mkutano wa makadinali kabla ya kongamano litakalomchagua Papa mpya

Nafasi ya Papa ajae imeendelea kuwa wazi kwa kila mtu kutoka katika maeneo mbalimbali ya dunia, na kutoka katika makanisa mbalimbali.
"Wakati alipofariki John Paul II mwaka 2005, kila mtu alikuwa anafikiria atakaeshinda nafasi hiyo kwa mwezi huo naku ra ilikuwa muda mfupi tuu'' amesema kadinali alijiuzulu akiongea na shirika la habari la AFP.
Kwa upande wa Afrika Makardinali waliotajwa ni pamoja na Peter Turkson kutoka Ghana, Robert Sarah Guinea na Wilfrid Napier kutoka Afrika Kusini

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR