Monday, October 6, 2014

Maporomoko ya Rusumo - Ngara

haya maporomoko ni ya maji Rusumo Falls
Mto huu unatokea upande wa Tanzania kuingia kwenye haya maporomoko
Maporomoko ya Rusumo-Ngara
Mungu azidi kushukuriwa na kutukuzwa kwa uumbaji




Kipa wa JKT Ruvu, Jackson Chove akiruka juu kuokoa hatari langoni mwake. Ambapo Hii Leo October 05,2014, huko Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam, Yanga SC wameichapa JKT Ruvu Bao 2-1 na kukwea hadi Nafasi ya 3 ya Ligi Kuu Vodacom
Yanga walifunga Bao lao la kwanza Dakika ya 32 kupitia Kelvin Yondani na Bao hilo kudumu hadi Haftaimu.

 Dakika ya 73, Haruna Niyonzima aliipatia Yanga SC Bao la Pili lakini JKT Ruvu walipata Bao lao moja katika Dakika za mwishoni Mfungaji akiwa Jabir Aziz.


KONGAMANO NA UJIRANI MWEMA

Kongamano hili litakuwa la Mkesha washiriki watatakiwa kuwasili Parokiani Boko siku ya Ijumaa tarehe 28/11/2014 saa tisa alasiri,na tunatarajia kuwa na semina na midahalo kwa usiku mzima, jumamosi ya tarehe 29/11/2014, saa kumi alasiri washiriki wote watarejea majumbani kwao baada ya kushibishwa kwa semina, midaho na michezo.

Washiriki kwenye Kongamano hili ni Vijana wote wenye Umri kuanzia miaka kumi na nane(18) wa Parokia ya Boko, Bunju na  Vijana wengine kutoka kwenye Parokia Mbali mbali za Jimbo kuu la Dar es  .
MWAKA WA FAMILIA.
Inafurahisha kuona kwamba, wazee wawili na vijana wawili wanakutanishwa na Yesu. Hii
inaonesha kwamba, Yesu ana uwezo wa kukutanisha na kuunganisha vizazi, kwani Yeye ni
chemchemi ya upendo inayovuka ubinafsi, upweke na masikitiko. Baba Mtakatifu anasema,
familia katika hija ya maisha yao wanashirikishana na kumegeana mambo mengi mema:
chakula na mapumziko; kazi za nyumbani, starehe, sala, safari na hija ya maisha ya kiroho
pamoja na matendo ya huruma.
Pale panapokosekana upendo, hapo hukosekana furaha , Upendo wa kweli
unabubujika kutoka kwa Kristo kwa njia ya Neno lake ambalo ni mwanga katika mapito ya
waamini; anawapatia Mkate wa maisha ya uzima wa milele, unaowasaidia waamini kupambana
na changamoto za maisha ya kila siku.
Baba Mtakatifu Francisko kama sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya Sinodi Maalum ya
Maaskofu kwa ajili ya Familia itakayoadhimishwa Mwezi Oktoba 2014 mjini Vatican, kwa
kuongozwa na kauli mbiu "Changamoto za kichungaji kuhusu familia mintarafu Uinjilishaji"
ameandika barua kwa familia zote duniani ili kukazia dhamana ya Kanisa kuendelea kutangaza
Injili kwa kukabiliana kinaga ubaga na changamoto mpya zinazohusu familia.
Baba Mtakatifu anasema, maandalizi haya yanawahusu Watu wote wa Mungu kwa kuhakikisha
kwamba, wanashiriki kikamilifu kwa kutoa mawazo pamoja na kusindikiza mchakato mzima kwa
njia ya sala, jambo muhimu sana kutoka kwa familia zote. Sinodi hii ni maalum kwa ajili ya: wito
na utume wa Kanisa na Jamii; matatizo yanayowakabili wanandoa; maisha ya kifamilia, elimu
na malezi kwa watoto; dhamana na utume wa familia katika maisha ya Kanisa.
Hivyo nakualika kijana mwenzangu uungane nasi hiyo siku katika kuyachambua haya kwa kina anza sasa kufanya maandalizi

ELIMU YA UJASIRIAMALI.
Elimu ya ujasiriamali katika nchi yetu haina ‘umri’ mkubwa kama zilivyo taaluma nyingine zikiwamo lugha, historia, siasa na sayansi. Hii ni kutokana na historia ya nchi yetu hasa baada ya kupata uhuru, kwamba tuliamua kufuata siasa ya ujamaa na kujitegemea kupitia Azimio la Arusha.
Siasa ya ujamaa na kujitegemea haikushadidia ujasiriamali kwa vile ulifananishwa na ubepari ambao ulichukuliwa kama unyama. Wale wote waliokuwa wanajihusisha na shughuli za kijasiriamali hasa biashara katika kipindi hicho walionekana kama ‘wanyama’ au watu ambao walikuwa wamechepuka kutoka katika njia kuu ambayo ilikuwa inaaminiwa na jamii kubwa wakati huo.
Wafanyakazi serikalini walikuwa hawaruhusiwi kujihusisha na biashara na kwamba shughuli za ujasiriamali zilionekana kufanywa na watu ambao hawakuwa na elimu ya kutosha kupata ajira, na wageni hasa kutoka Bara la Asia kama vile Wahindi.
Hata hivyo, kutokana na hali halisi ya maisha katika nchi yetu na duniani kwa jumla, kwenye miaka ya katikati ya 2000, taifa lilianza utaratibu wa kuingiza elimu ya ujasiriamali katika elimu ingawa haikuwekewa kipaumbele sana. Kwa sasa elimu ya ujasiriamali imekuwa kama wimbo wa taifa, siyo shuleni na vyuoni bali hata katika sekta ambazo si rasmi kama ambavyo tumekuwa tukishuhudia matangazo mbalimbali juu ya kuendesha elimu ya ujasirimali katika makundi mbalimbali ya jamii yetu.
Kutokana na wanajamii na taifa kwa jumla kuanza kuona elimu ya ujasiriamali kama mwarobaini wa matatizo yanayowakabili kama vile ajira na umaskini, lengo la la Kongamano letu  ni kuelezea umuhimu wa elimu ya ujasiriamali katika Chama chetu cha VIWAWA  kama njia mojawapo yenye kuonyesha jinsi elimu ya ujasiriamali inavyoweza kuisaidia jamii na taifa katika kuleta maendeleo.
Ujasiriamali ni mchakato au hali waliyonayo baadhi ya watu ya kutaka mafanikio yanayoshadadiwa na moyo wa ushindani, kujiamini, uwezo binafsi wa kukabiliana na kutatua changamoto zilizopo ikiwa ni pamoja na uthubutu wa kukabiliana na changamoto ambazo wakati mwingine huweza kuathiri maisha yao katika kipindi cha mpito.
Kumekuwa na mjadala wa muda mrefu kama ujasiriamali hufundishwa au mtu huzaliwa nao ingawa si lengo la kongamano letu si kujikita katika mjadala huo, kwa kuwa tunaelewa nguvu iliyonayo elimu katika kuyatengeneza maisha ya mwanadamu.
Tunaamini kuwa vijana wana maono na matamanio yao katika maisha kama walivyo watu wazima ingawa watu hawa wawili wanaweza kutofautiana hapa na pale kutokana na sababu za umri, mazingira, wakati na uzoefu katika maisha.
Elimu ya ujasiriamali katika Vyama au kikundi  hujenga msingi mzuri wa kujiamini miongoni mwa vijana na hivyo kuwafanya wayakabili maisha bila woga, jambo ambalo litawafanya kufanya kazi zao wanazozipenda kwa umahiri, weledi na kujiamini zaidi.
hivyo basi nakusi sana kuungana nasi katika kupata elimu hiyo, tunatarajia pia kuunda vikundi vya ujasiriamali kwa vijana watano watano na kuwapatia wataalamu watakao wasimamia.
kwa maelezo zaidi tuandikie kupitia viwawaboko@yahoo.com au piga 0713 900 905


NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR