Showing posts with label Ni kwanini vijana wanaogopa ndoa (kwanini vijana hawataki kuanzisha kanisa dogo). Show all posts
Showing posts with label Ni kwanini vijana wanaogopa ndoa (kwanini vijana hawataki kuanzisha kanisa dogo). Show all posts

Tuesday, November 18, 2014

Ni kwanini vijana wanaogopa ndoa (kwanini vijana hawataki kuanzisha kanisa dogo)

kuelekea kwenye semina ya Mwaka wa familia tarehe 28-29/11/2014. vijana wanaandaliwa kujenga familia Bora familia ya Kikristo, familia ambayo ni kanisa Dogo, kanisa la nyumbani
 
Matunda ya familia bora ni kuwa na Imani, mapendo na matumaini miongoni kwa wanafamilia, kazi mbayo ni kubwa, familia ilikabiliana na kinzani pamoja na changamoto kubwa za kitamaduni, lakini imani ikaendelea kukua na kuota mizizi katika familia zetu,

tunu za maisingi ya Kikristo kuleta mabadiliko miongoni mwa wa vijana ambao walianza kupata malezi hayo tokea utotoni ,hapo ndipo huibuka miito ya  kipadre na kitawa, neema na baraka kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
 

Kwa sasa vijana  tunaendelea kukabiliana na changamoto mbali mbali katika maisha, hasa kutokana na ongezeko la umaskini, hali ambayo inazifanya familia nyingi kutafuta njia za mkato; mambo ambayo wakati mwingine yanahatarisha imani na matokeo yake ni watu kukata tamaa. Baba Mtakatifu anasema, Familia inapaswa kupewa kipaumbele cha kwanza kwani ni msingi wa Jamii, mahali ambapo watu wanajifunza kuishi kwa pamoja, licha ya tofauti zao msingi na kwamba ni mahali pa kurithisha imani, dhamana inayotekelezwa na wazazi. Familia ni madhabahu ya Injili ya Uhai, inayopaswa kudumishwa na kuendelezwa.

Wanandoa ambao wengi ni wazazi wetu na vijana wenzetu wadumishe uaminifu na mapendo ya ndoa, wasaidie majiundo ya kina kwa watoto wao sanjari na kudumisha tunu msingi za maisha ya ndoa na familia yanayojikita katika Mafundisho tanzu ya Kanisa na kumwilishwa katika uhalisia wa maisha, ili kuwa kivutio kwa vijana wanajianda kuingia kwenye wito huo.

Viongozi wa Kanisa waendelee kuwa karibu zaidi na vijana katika malezi na makuzi yao, ili waweze kuwa na utambulisho makini, tayari kushiriki katika kazi ya uumbaji kwa kujikita katika wito wa ndoa au Daraja takatifu au maisha ya kitawa kwa ajili ya wokovu wa roho za watu. Vijana wafundwe kuchuchumilia usafi wa moyo pamoja na kukuza ushirikiano miongoni mwa utume wa vijana wa Parokia hizi, ili wote waweze kujisikia kuwa wako ndani ya Familia ambayo kimsingi ni Kanisa dogo la nyumbani.
...bonjeza hapa Kuendelea kusoma hapa


NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR