Showing posts with label wa Kanisa Dominika ya sikuku ya Ubatizo wa Bwana2015. Show all posts
Showing posts with label wa Kanisa Dominika ya sikuku ya Ubatizo wa Bwana2015. Show all posts

Sunday, January 11, 2015

Masomo ya Tarehe 11/01/2015 mwaka B, wa Kanisa Dominika ya sikuku ya Ubatizo wa Bwana2015

11

 Januari
 Jumapili: ya Ubatizo wa Bwana.
SOMO  1. Isa. 42:1-4, 6-7

 Bwana asema: Tazama mtumishi wangu nimtegemezaye; mteule wangu, ambaye nafsi yangu imependezwa naye; nimetia roho yangu juu yake; naye atawatolea mataifa hukumu. Hatalia, wala hatapaza sauti yake, wala kuifanya isikiwe katika njia kuu. Mwanzi uliopondeka hautavunjika, wala utambi utokao moshi hautazima; atatokeza hukumu kwa kweli. Hatazimia , wala hatakata tamaa, hata atakapoweka hukumu duniani; na visiwa vitaingojea sheria yake. Mimi, Bwana, nimekuita katika haki, nami nitakushika mkono, na kukulinda, na kukutoa uwe agano la watu, na nuru ya mataifa; kuyafunua macho ya vipofu, kuwatoa gerezani waliofungwa, kuwatoa wale walioketi gizani katika nyumba ya kufugwa.

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR