Showing posts with label DOMINIKA YA 3 YA PASAKA MWAKA A 2014. Show all posts
Showing posts with label DOMINIKA YA 3 YA PASAKA MWAKA A 2014. Show all posts

Tuesday, April 29, 2014

MASOMO YA JUMAPILI DOMINIKA YA 3 YA MWAKA A TAREHE 04/05/2014

JUMAPILI DOMINIKA YA 3 ya Pasaka ya Mwaka A.
      RATIBA ZA IBADA 
KIGANGO CHA MH. ISIDORI BAKANJA- BOKO.
MISA YA KWANZA 12:15-2:00 ASUBUHI
MISA YA PILI     SAA 2:00-4:00 ASUBUHI
MISA YA TATU SAA 4:00-5:30 ASUBUHI
KIGANGO CHA MT. FRANCIS WA ASIZ-MBWENI 
MISA YA KWANZA SAA 1:10-3:00 ASUBUHI
MISA YA PILI SAA 3:00-4:30 ASUBUHI

KIGANGO CHA MT. RAFAEL-MBWENI MALINDI
SAA 1:00-3:00 ASUBUHI.
MISA YA PILI SAA 3:00-5:00

KIGANGO CHA ANTHONY WA PADUA-MBWENI TETA
MISA NI SAA 3:00-5:00.


MASOMO 

SOMO 1:Mdo.2:14,22-28
Petro alisimama pamoja na wale kumi na moja,akapaza sauti yake, akawaambia, enyi watu wa Uyahudi, ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu, Yesu wa Nazareti, mtu aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujuza na ajabu na ishara, ambazo Mungu alizifanya kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe mnavyojua; mtu huyu aliotolewa kwa shauri la Mungu lilikusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulubisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua; ambaye Mungu alimfufua, akaufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao. Maana Daudi ataja habari zake. Nalimwona Bwana mbele yangu siku zote, kwa kuwa yuko upande wa mkono wangu wa kuume, nisitikisike. Kwa hiyo moyo wangu ukapendezewa, ulimi wangu ukafurai; tena mwili wangu nao utakaa katika matumaini. Kwa maana hutaiacha roho yangu katika kuzimu; wala hutamtoa mtakatifu wako aone uharibifu. Umenijulisha njia za uzima; utanijaza furaha kwa uso wako.

SOMO 2: 1Pet. 1:17-21
Ikiwa unamwita Baba, yeye ahukumuye kila mtu asipo upendeleo, kwa kadri ya kazi yake, enendeni kwa hofu katika wakati wenu wa kukaa hapa kama wageni. Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhambi; mpate kutoka katika mwenendo wenu usiofaa mlioupokea kwa Baba zenu; bali kwa damu ya thamani, kama ya mwana-kondo asiye na ila, asiye na waa, yaani, ya Kristo. Naye amejulikana kweli tangu zamani, kabla haijawekwa misingi ya dunia; lakini alifunuliwa mwisho wa zamani kwa ajili yenu; ambao kwa yeye mmekuwa wenye kumwamini Mungu, aliyemfufua katika wafu akampa utukufu; hata Imani yenu na tumaini lenu liwe kwa Mungu.

INJILI. :Lk. 24:13-35
Siku ile watu wawili miongoni mwa wafuasi wa Yesu walikuwa wakienda kijiji kimoja, jina lake Emau, kilichokuwa mbali na Yerusalemu kama mwendo wa saa mbili. Nao walikuwa wakizungumza wao kwa wao habari za mambo hayo yote yaliyotokea. Ikawa katika kuzungumza na kuulizana kwao Yesu mwenyewe alikaribia, akaandamana nao. Macho yao yakafumbwa wasimtambue. Akawaambia, ni maneno gani haya tangu yalipotendeka mambo haya; tena wanawake kadha wa kadha wa kwetu walitushitusha, walivyokwenda kaburini asubuhi na mapema, wasiuone mwili wake; wakaja wakasema ya kwamba wametokewa na malaika waliosema kwamba yu hai. Na wengine walikuwa pamoja nasi walikwenda kaburini wakaona vivyo hivyo kama wale wanawake walivyosema, ila yeye hawakumwona. Akawaambia, enyi msiofahamu, wenye mioyo mizito ya kuamini yote waliyoyasema manabii! Je! Haikupasa Kristo kupata mateso haya na kuingia katika utukufu wake? Akaanza kutoka Musa na manabii wote, akawaeleza katika maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye mwenyewe. Wakakaribia kile kijiji walichokuwa wakienda, naye alifanya kama anataka kwendelea mbele. Wakamshawishi wakisema, kaa pamoja nasi, kwa kuwa kumekuchwa, na mchana unakwisha. Akaingia ndani kukao nao. Ikawa alipokuwa ameketi nao chakulani, alitwaa mkate, akaubariki, akaumega,akawapa.yakafumbuliwa macho yao, wakamtambua; kasha akatoweka mbele yao. Wakaambiana, je! Mioyo yetu haikuwaka ndani yetu hapo alipokuwa akisema nasi njiani, kutufunulia maandiko? Wakaondoka saa ile ile, wakarejea Yerusalemu,wakawakuta wale kumi na moja wamekutanika, wao na wale waliokuwa pamoja nao, wakisema, Bwana amefufuka kweli kweli, naye amemtokea Simoni. Nao waliwapa habari ya mambo yale ya njiani, na jinsi alivyojitambulisha nao katika kuumega mkate.


  1.  form za ziara ya uinjilishaji parokia ya Dareda na ziara ya mbuga ya wanyama ya ngorongoro zipo tayari na nafasi zimebaki chache wahi sasa nafasi ikiwa kama kijana mkatoliki askari kamili wa Yesu,...twende tuungane pamoja katika kumtangaza yeye aliye njia ya uzima na ukweli mchango na tshs 180,000 tu na mwisho wa kupokea michango ni tarehe 18/06/2014.
  2. tunawakumbusha vijana wote kuendelea kulipa ada kwa maendeleo ya chama chetu..... mapendo sana malipo kwa njia ya benk kwa jina na number hii :viwawa parokia ya boko account no 01524526820100 crdb bank tegeta branch
JIANDAE NA ZIARA YA UINJILISHAJI MWAKA 2014.....................

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR