Showing posts with label 12 0ctober 2014: Masomo ya JUMAPILI YA 28 YA MWAKA "A" 2014.. Show all posts
Showing posts with label 12 0ctober 2014: Masomo ya JUMAPILI YA 28 YA MWAKA "A" 2014.. Show all posts

Monday, October 13, 2014

Masomo ya Dominika ya 28 ya Mwaka A wa kanisa, Tarehe 12/10/2014

12
 October
 JUMAPILI YA 2 YA MWAKA "A" 2014.
SOMO  1. Isa. 25:6-10

Somo katika  kitabu cha Nabii Isaya.
Katika mlima huu Bwana wa majeshi  atawafanyia mataifa yote karamu ya vitu vinono, karama ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, karamu ya vinono vilivyojaa mafuta, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo  wake, iliyochujwa sana. Naye katika mlima huu atauharibu uso wa sitara iliyowekwa juu ya watu wote, na utaji ule uliyotandwa juu ya mataifa yote. Amemeza mauti hata milele; na Bwana Mungu atafuta machozi katika nyuso zote; na aibu ya watu wake ataiondoa katika ulimwengu wote; maana Bwana amenena hayo. 

Katika siku hiyo watasema, 
Tazama huyu ndiye Mungu wetu, 
Ndiye tuliyemngoja atusaidie; 
Huyu ndiye Bwana tuliyemngoja,
 Na tushangilie na kuufurahia wokovu wake.
 Kwa maana mkono wa Bwana utatulia katika mlima huu.


SOMO  2. Flp. 4:12-14,19-20
Somo katika waraka wa mtume Paulo kwa Wafilipi. 
Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; katika hali yo yote, na katika mambo yo yote, nimefundishwa kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na kupungukiwa.Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu. Lakini mlifanya vema, mliposhiriki nami katika dhiki yangu. Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu. Sasa atukuzwe Mungu, Baba yetu, milele na milele. Amena.


  INJILI.Mt. 21:33-43

Somo katika Injili ilivyoandikwa na Mathayo.


Yesu alijibu, akawaambia tena kwa mithali, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyemfanyia mwanae arusi. Akawatuma watumwa wake wa waite walioalikwa kuja arusini; nao wakakataa kuja. Akatuma tena watumwa wengine, akisema, Waambieni wale walioalikwa, Tazameni nimeandaa karamu yangu; ng'ombe zangu na vinono vimekwisha kuchinjwa, na vyote vimekuwa tayari, njoni arusini. Lakini hawakujali, wakaenda zao mmoja shambani kwake, mmoja kwenye biashara yake; nao waliosalia wakawakamata watumwa wake, wakawatenda jeuri, na kuwaua. Basi yule mfalme akaghadhibika;akapeleka majeshi yake,akawaangamiza wauaji wake, akauteketeza mji wao. Kisha akawaambia watumwa wake, arusi i tayari, lakini wale walioalikwa hawakustahili. Basi enendeni hata njia panda za barabara, na wote mwaonao waiteni arusini. Watumwa wale wakatoka wakaenda njia kuu, wakakusanya wote waliowaona, waovu kwa wema; arusi ikajaa wageni. Lakini alipoingia yule mfalme ili kuwatazama wageni wake, akaona mle mtu mmoja asiye vaa vazi la arusi. Akamwambia, Rafiki, uliingiaje humu nawe huna vazi la arusi? Naye akatekewa. Mfalme akawaambia watumishi, Mfungeni mikono na miguu, mchukueni mkamtupe katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno. Kwa maana waitwao ni wengi, bali wateule ni wachache.

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR