Showing posts with label Kipindi cha Kwaresima: Masomo ya alhamisi ya Majivu mwaka B wa kanisa 2015. Show all posts
Showing posts with label Kipindi cha Kwaresima: Masomo ya alhamisi ya Majivu mwaka B wa kanisa 2015. Show all posts

Thursday, February 19, 2015

Masomo ya Alhamisi ya Majivu Mwaka B wa kanisa Tarehe 19/02/2015

19

 FEBRUARY
 Kipindi cha Kwaresima: Alhamisi ya Majivu. Mwaka "B".
SOMO  1: Kumb. 30:15 - 20

Musa aliwaambia watu akisema: Angalia, nimekuweka leo mbele yako uzima na mema, na mauti na mabaya; kwa hivi nikuagiziayo leo kumpenda Bwana, Mungu wako, kuenenda katika njia zake, na kushika maagizo yake, na amri zake, na hukumu zae upate kuwa hai na kuongezaka; Bwana Mungu wako apate kukubarikia katka nchi uingiayo kuimiliki. Lakini moyo wako ukigeuka, usipotaka kusikiza, laini ukavutwa kando kwenda kuabudu miungu mingine, na kuitumikia; nawahubiri hivi leo hakika mtaangamia, hamtazifanya siku zenu kuwa nyingi juu ya nchi, uivukayo Yordani, uingie kuimiliki. Zasishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti baraka na laana; basi chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako; kumpenda Bwana, Mungu wako kuitii sauti yake, na kushikamana naye, kwani hivyo ndivyo uzima wako, na wingi wa siku zako; upate kukaa katika nchi ya Bwana aliyowaapia baba zako. Ibrahimu na Isaka, na Yakobo, kuwa atawapa.

WIMBO WA KATIKATI. Zab. 1:1-4, 6. 
K. Heri mtu aiyemfanya Bwana kuwa tumaini lake.

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR