Sunday, February 24, 2013

Jimbo Katoliki la Mbulu

Jimbo katoliki la Mbulu (kwa Kilatini Dioecesis Mbuluensis) ni mojawapo kati ya majimbo 33 ya Kanisa Katoliki nchini Tanzania na kama hayo yote linafuata mapokeo ya Kiroma.

Kikanisa linahusiana na jimbo kuu la Arusha.
Askofu wake ni Beatus Kinyaiya.

Historia

  • 1943: Kuanzishwa kwa Apostolic Prefecture ya Mbulu kutokana na Apostolic Vicariate ya Dar-es-Salaam
  • 1952: Kupandishwa cheo kuwa Apostolic Vicariate ya Mbulu
  • 25 Machi 1953: Kufanywa dayosisi

Uongozi

  • Maaskofu wa Mbulu
    • Beatus Kinyaiya (since 2005)
    • Juda Thadaeus Ruwa’ichi OFMCap (1999 – 2005)
    • Nicodemus Atle Basili Hhando (1971 – 1997)
    • Patrick Winters SAC (1953 – 1971)
  • Vicar Apostolic wa Mbulu
    • Patrick Winters SAC (1952 – 1953)
  • Prefect Apostolic wa Mbulu
    • Patrick Winters SAC (1944 – 1952)

Takwimu

Eneo ni la kilometa mraba 16,057, ambapo kati ya wakazi 995,000 (2006) Wakatoliki ni 269,620 (27.1%).

MALENGO YA ZIARA YA MBULU

Lengo kubwa la ziara hii ni kwaona Vijana wenzetu na kushirikiana nao jinsi ya kueneza Injili  pia kujenga mashirikiano katika maswala ya kiuchumi na maendeleo kwa ujumla pia tutapata nafasi ya kujifunza tamaduni mpya kutoka katika makabila mbali mbali yalipo huko

Zaidi tutafika katika kanisa Kuu la Jimbo la Mbulu na kujionea ukubwa wake ambapo ndilo kanisa kubwa kuliko yote hapa Africa Mashariki.

mwisho tutaenda Mbuga ya wanyama ya Ngorongoro kuona uzuri wa nchi Yetu na Maajabu ya Mungu.

 KUWA TAYARI NA ANZA MAANDALIZI SASA KWA KUJAZA FORM NA KUWAKILISHA FEDHA YAKO NAFASI NI KWA VIJANA 60 TU.

Matangazo ya Juma la lijalo......

      JUMAMOSI TAREHE 02/03/2013
  1.  Kutakuwa na mafungo ya jubilee ya Miaka 200 ya Shirika la Damu Takatifu, Mafungo hayo yatafanyikia katika kituo cha Hija cha Shirika kilichopo Parokia ya Mt. Gasper De Bufalo Mbezi Beach na yataanza saa 2:00 asubuhi
  2. Kamati tendaji ya VIWAWA Kigango cha Mt. Rafael Mbweni Malindi watafanya kikao saa kumi na moja jioni Kigangoni...Pia Vijana wote wanakumbushwa kufika saa kumi Jioni kwa ajili ya Mazoezi ya Kwaya.
  

       JUMAPILI TAREHE 03/03/2013
      RATIBA ZA IBADA ZA MISA TAKATIFU
KIGANGO CHA BOKO.
MISA YA KWANZA 12:30-2:00 ASUBUHI
MISA YA PILI     SAA 2:00-4:00 ASUBUHI
MISA YA TATU SAA 4:00-5:30 ASUBUHI

KIGANGO CHA MBWENI 
MISA YA KWANZA SAA 2:00-4:00 ASUBUHI
MISA YA PILI SAA 4:00-5:30 ASUBUHI

KIGANGO CHA MT. RAFAEL-MBWENI MALINDI
SAA 2:00-4:00 ASUBUHI

Halmashauri ya VIWAWA Parokia watakuwa na Kikao mara baada ya Misa ya Pili Saa 4:00 asubuhi kikao kitafanyikia Parokiani Boko wajumbe wote mnatakiwa kufika Bila kukosa.

Wasilisha Mchango wako wa Hija ya Bagamoyo kwa Mhazini wa Jumuiya yako au Kigango chako Kabla ya Tarehe 09/03/2013

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR