Showing posts with label uchaguzi wa viongozi wa dekania ya Mt. Gasper del buffalo-mbezi beach. Show all posts
Showing posts with label uchaguzi wa viongozi wa dekania ya Mt. Gasper del buffalo-mbezi beach. Show all posts

Tuesday, January 6, 2015

UMOJA WA VIJANA DEKANIA YA MT. GASPER DEL BUFFALO - kufanya uchanguzi wa Viongozi tarehe 10/01/2015

Dekania ya Mt. Gasper ni Dekania ilipo katika Jimbo kuu la Dar es salaam, inaundwa na Parokia kumi na moja ambazo ni  Parokia ya Bunju, Boko Tegeta, Madale, Bahari Beach, Mtongani, St. Gasper, Maria Del Mathias, Sala sala, Mt. Dominiko, Bikira Maria Mama wa huruma, Mbezi Beach  Pamoja na Parokia teule za Thomas More Mbezi Beach, Yohane Mtume, Nyaishozi Tegeta na Parokia ya Ununio tegeta.

Baada ya Baba mlezi wa vijana wa Dekania kuona mwenendo mbaya wa viongozi na kuamua kuwashirikisha Mapadre wote wa parokia za Dekani hii, kwa pamoja wameridhia kuvunja uongozi wa VIWAWA dekania, na kuitisha uchaguzi mpya ili wapatikane viongozi wapya watakao leta maendeleo kwenye dekania yetu.

Uchaguzi huo utafanyika tarehe 10/01/2015 Parokiani Bunju kuanzia saa 3:00 asubuhi, wajumbe wa uchaguzi huo ni Kamati tendaji ya VIWAWA, Parokia zote za dekania yetu.

Pia tarehe 17/01/2015 kutakuwa na Semina ya vijana wote wa Dekania itakayofanyikia Pale Parokiani St. Gasper na atakuwepo Msanii wa Nyimbo za Bongo Fleva Roma Mkatoliki.

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR