Showing posts with label tamasha 2013. Show all posts
Showing posts with label tamasha 2013. Show all posts

Monday, July 29, 2013

Tamasha la vijana 2013

Kila mwaka vijana wa Parokia ya Boko huwa wanakutana kwa siku tatu katika Tamasha la Vijana Parokia, Kilele cha Tamasha hili huwa ni siku ya kumbukumbu ya Mwenye Heri Isidore Bakanja ambaye ni Somo wa Parokia yetu. 

Kwa mwaka huu sherehe hizi zitaambatana na maadhimisho ya miaka kumi tangu tuwe parokia, kutokana na ukubwa wa sherehe hiyo.. Halmashauri ya Walei Parokia wakaombe sherehe hizi pamoja na tamasha zisogwe mbele mpaka tarehe 18/08/2013, ili maandalizi yaweze kufanyika kwa ufasaha zaidi.

kwa upande wa Vijana mashindano ya Mpira wa miguu yanaendelea na fainal inatarajiwa kufanyika tarehe 17/08/2013 katika uwanja wa Boko... pia tutakuwa na fainal ya mpira wa Pete kwa wasichana, michezo ya ndani kama kuvuta kamba, kukimbia na Yai, maigizo, mashairi, vichekesho, sarakasi , kuimba n.k.

Kwa upande wa semina ni furaha kubwa sana kwetu, kwani tunao mababa wa kiroho ambao wapo Parokiani kwetu na wanasubiri tu hiyo siku tutakuwa naye Baba Paroko Pd: Dismass, Pd:Mlezi wetu Dominick na Sauti ya Radi Paroko Msaidizi PD: Nicolus Ngowi.

Fika uwe sehemu ya Mabadiliko chanja....yenye tija ya kukomaza mapendo Mioyoni mwetu, kuleta maendeleo ya Kiroho na Kijamii ndani ya Familia zetu na Jamii nzima kwa ujumla.

Kwa mchango wa Tshs 7000 kwa ajili ya Chakula Vinjwaji na Malazi Mepesi..........

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR