Showing posts with label SHIRIKA LA DAMU TAKATIFU YA YESU. Show all posts
Showing posts with label SHIRIKA LA DAMU TAKATIFU YA YESU. Show all posts

Tuesday, May 21, 2013

Miaka 10 tangu Mwenyeheri Maria de Mattias alipotangazwa kuwa Mtakatifu

Miaka 10 tangu Mwenyeheri Maria de Mattias alipotangazwa kuwa Mtakatifu: Wanovisi wanne waweka nadhiri za kwanza Jimboni Dodoma



Shirika la Masista Waabuduo Damu Takatifu ya Yesu linaadhimisha Kumbu kumbu ya Miaka 10 tangu Baba Mtakatifu Yohane Paulo wa pili alipomtangaza Mwenyeheri Maria de Mattias kuwa Mtakatifu hapo tarehe 18 Mei 2003. Itakumbukwa kwamba, ni Papa Pio wa XII aliyemtangaza kuwa Mwenyeheri kunako mwaka 1950.

Kumbu kumbu ya miaka kumi tangu Mtakatifu Maria de Mattias kutangazwa kuwa Mtakatifu imesherehekewa na Masista Waabuduo Damu Takatifu ya Yesu kwa: Makongamano, Ibada ya Misa Takatifu na Mafungo ya kiroho.

Shirika la Masista Waabuduo Damu Takatifu ya Yesu nchini Tanzania limeadhimisha Kumbu kumbu hii kwa Ibada ya Misa Takatifu iliyoongozwa na Askofu Gervas Nyaisonga wa Jimbo Katoliki Dodoma katika Kikanisa cha Makao Makuu ya Shirika hili, nchini Tanzania sanjari na Wanovisi wanne kuweka nadhiri zao za kwanza. Hawa ni Sr. Immaculata Sayumwe, Sr. Leticia Kisena, Sr. Maria Mrema pamoja na Sr. Theresia Mwendwa.

Katika Ibada ya Misa Takatifu, Askofu Nyaisonga amewataka watawa kulinda na kutunza thamani ya maisha na wito sanjari na kuienzi Damu Azizi ya Kristo mto wa rehema na chemchemi ya huruma na upendo wa Mungu kwa watu wake. Amewataka watawa kujiamini kwa kuwa Mwenyezi Mungu anaendelea kutembea pamoja nao katika hija ya maisha na imani. Watawa wanatakiwa kukumbuka kwamba, nadhiri zao ni bendera ya ushindi na mwenge unaowaangazia wengine nuru katika maisha.

Ibada hii ya Misa Takatifu imehudhuriwa na viongozi wa Kanisa, Watawa na Waamini walei kutoka ndani na nje ya Jimbo Katoliki la Dodoma.

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR