Monday, September 29, 2014

TAFAKARI YA NENO LA MUNGU DOMINIKA YA 24 YA MWAKA A, 28SEPTEMBA

TAFAKARI YA NENO LA MUNGU DOMINIKA YA 24 YA MWAKA A, 28SEPTEMBA



Tunakualika katika tafakari yetu, Dominika ya 24 ya mwaka A wa Kanisa tukilenga kukua katika toba na msamaha wa Mungu ulio wa kudumu. Katika historia, kadiri ya mangamuzi ya watu njia rahisi ya kujibu dhuluma ilikuwa ni kwa njia ya hasira na zaidi jino kwa jino (Kut 21:24) wakijaribu kutafuta mlinganyo sahihi (proportionality to the offence) lakini leo hii kadiri ya somo la kwanza toka kitabu cha Hekima ya Yoshua bin Sira tunaalikwa kutawala hasira zetu, kuacha chuki na kuacha kulipiza kisasi maana haya ni machukizo mbele ya Mungu. Ni hali ambayo huongeza taabu katika jumuiya badala ya kupunguza taabu. Basi kama mmoja wetu atashupaa katika haya, naye vivyohivyo atatendewa vivyohivyo yaani atajiondoa katika ufalme wa Mungu. Kumbe ndugu yangu mpendwa, leo tunaalikwa kupiga hatua katika safari ya kiroho tukiunganika na mausia ya Bwana kadiri ya Injili.

Mtume Paulo akiendeleza fundisho tunalolipata katika somo la kwanza anasema sisi hatuishi kwa ajili yetu wenyewe kama watu wenye chuki na visasi waishivyo bali twaishi kwa ajili ya Bwana. Anafundisha hili kwa sababu katika jumuiya ya kirumi mjini Roma kuna utengano kati ya wanaoshika sheria ya kufunga kadiri ya utamaduni wa mwanzo walipopokea imani na wale wanaojiona wa kisasa wanoshika sheria ya mapendo kwa ndugu. Kumbe ili kusahihisha dosari hii Mt. Paulo anasema sisi sote ni mali ya Bwana katika yote na hata tukifa tunakufa katika yeye. Ndiyo kusema matendo, maneno yetu, nyajibu zetu, sheria tunazoshika, familia zetu, parokia zetu, majimbo yetu tunayoyasimamia ni mali ya Kristu. Kwa hivi tuwajibike tukitambua hilo na mwishoni mapenzi ya Mungu yafanyike. Mafundisho ya Mt Paulo ni msaada kwa jumuiya zetu zinapojikuta ziko katika mgongano kwa sababu ya mwono tofauti. Zinaalikwa pande mbili pinzani kuketi na kutatua shida kwa pamoja kwa kuheshimiana.

Tunaendelea bado kutafakari Injili ya Mathayo, na leo Mwinjili atuambia kuwa msamaha ni wa kudumu. Msamaha hauna mipaka bali kama ulivyo upendo unaovumilia basi na msamaha wapaswa kuwa namna hii. Mt Petro akiwa bado katika mawazo ya kiyahudi ya kusamehe kimahesabu, yaani mara saba, anamwuliza Kristu nisamehe mara ngapi ndugu akinikosea? Kristu anakuja na fundisho jipya ya kwamba hakuna tena suala la mahesabu katika kusamehe bali mapenzi ya Mungu yatimizwe daima. Kristu anataka tuondoke katika mazoea ya kila siku na hivi tuingie katika mpango wa milele ambao ni msamaha wa kudumu. Mfano wa mtumwa katika Injili, mtumwa aliyesamehewa deni, deni ambalo asingeweza kulilipa mpaka anakufa kwa hakika ni kielelezo cha huruma ya Mungu iliyo milele!

Pamoja na huruma ya Mungu iliyo milele bado mwanadamu ni dhaifu, haoni vema. Huyu mtumwa aliyesamehewa deni lote yeye mwenyewe hakuweza kuwasamehe wajoli wake. Hiki ni kielelezo cha udhaifu wa mwanadamu ambaye daima hushindwa kusamehe na hasa kosa au dhambi inapojirudia. Ni picha ya kuwa tunahitaji daima huruma ya Mungu. Basi ndugu yangu mpendwa, tukumbuke kuwa kusamehe ni zawadi, ni fadhila tunayopaswa kuiomba daima ili tuweze kuunganika na Kristu mfufuka anayetutaka kusamehe daima na anayesamehe daima. Kinyume cha fadhila hii basi tutakuwa tumejiweka pembeni katika ufalme wa Mbinguni.

Tumalizie tukisema, Suala la kusamehe ni wajibu wa kila mtu awaye yote si wenye mamlaka ya juu tu katika jumuiya bali na wale wanaoongozwa na tukumbuke kuanguka katika dhambi ya kutosamehe na kukuza chuki zisizoisha ni hatari kubwa iliyo mbele yetu. Yaweza kuzuia na hivi tukakosa kuingia mbinguni. Fikiri kidogo mtu asemaye “Mimi nitakapokufa mtu fulani asikaribie na hata kuweka udongo kwenye kaburi langu!! Chuki ya ujazo huu haina maelezo lakini yatishishia usalama wa roho ya mtu huyo aliyefariki!! Tafakari kidogo!Tumwombe Mungu daima atutangulie na kutulinda katika kutekeleza wajibu wa kusamehe. Tumsifu Yesu Kristu.
Tafakari hii imeletwa kwako na Pd Richard Tiganya Cpps
TAFAKARI YA NENO LA MUNGU DOMINIKA YA 24 YA MWAKA A, 28SEPTEMBA

MASOMO YA JUMAPILI TAREHE 28/09/2014 MWAKA" A" WA KANISA

28
 SEPTEMBER
 JUMAPILI YA 26 YA MWAKA "A" 2014.


RATIBA ZA IBADA

KIGANGO CHA BOKO.
IBADA YA MISA YA KWANZA 12:15 – 1:45 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 2:00 – 3:50 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA TATU SAA 4:00-5:20 ASUBUHI
KIGANGO CHA MBWENI.
IBADA YA MISA YA KWANZA 1:15 – 2:55 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 3:00 – 4:50 ASUBUHI
KIGANGO CHA MT. RAFAEL.
IBADA YA MISA YA KWANZA 1:00 – 2:55 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 3:00 – 4:50 ASUBUHI
KIGANGO CHA ANTHONY WA PADUA – MBWENI MPIJI.
IBADA YA MISA NI 3:00 – 5:00ASUBUHI

SOMO  1. Eze. 18:25-28
Bwana ameniambia hivi: Ninyi mwasema; Njia ya Bwana ni sawa. Sikilizeni sasa, Enyi nyumba ya Israeli; je! njia yangu siyo iliyo sawa? Njia zenu sizo zisizo sawa? Mwenye haki atakapoghairi, na kuiacha haki yake, na kutenda uovu, atakufa katika uovu huo; katika uovu wake alioutenda atakufa. Tenamtu mwovu atakapoghairi, na kuuacha uovu wake alioutenda, na kutenda yaliyo halali na haki, ataponya roho yake, nayo itakuwa hai. kwa sababu atafakari, na kughairi, na kuyaacha makosa yake yote aliyoyatenda, hakika ataishi, hatakufa. 

SOMO  2. Flp. 2:1-11


Ikiwako faraja yo yote katika Kristo, yakiwako matulizo yo yote ya mapenzi, ukiwako ushirika wo wote wa Roho, ikiwako huruma yo yote na rehema, ijalizeni furaha yangu, ili mwe na nia moja, mwenye mapenzi mamoja, mwenye Roho moja, mkinia mamoja. Usitende neon lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa na bora kuliko nafsi yake. kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo yake mwenyewe. Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa binadamu; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba. kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa Yesu Kristo ni Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.

  INJILI.Mt. 21:28-32


 Yesu aliwaambia wakuu wa makuhanina wazee, Mwaonaje? mtu mmoja alikuwa na wana wawili; akamwendea yule wa kwanza, akasema, mwanangu, leo nenda kafanya kazi katika shamba la mizabibu. Akajibu akasema, Naenda, Bwana;  asiende. Akamwendea yule wa pili, akasema vile vile. Naye akijibu akasema, sitaki; baadaye akatubu, akaenda. je! katika hao wawili ni yupi aliyefanya mapenzi ya babaye? Wakamwambia, Ni yule wa pili. Basi Yesu akawaambia, Amin, nawaambia, watoza ushuru na makahaba wanatangulia mbele yenu kuingia katika ufalme wa Mungu. kwa sababu Yohana alikuja kwenu kwa njia ya haki, ninyi msimwamini; nanyi hata mlipoona, hamkutubu baadaye, ili kumwamini.


Matangazo
jiandaye na Kongamano la ujirani kati ya Parokia ya Boko na bunju' mwema, nunue Ticketi yako sasa kwa Tshs 18,000. Kongamano litafanyika kuanzia tarehe 28-29/11/2014, Parokiani Boko w

 

 

 


NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR