Showing posts with label Heri ya Pasaka Mwaka 2015 (masomo ya dominika ya Paska). Show all posts
Showing posts with label Heri ya Pasaka Mwaka 2015 (masomo ya dominika ya Paska). Show all posts

Saturday, April 4, 2015

Masomo ya Jumapili ya Paska "mwaka B wa Kanisa (Tarehe 05/04/2015)

05

 APRILI
 Heri ya Paska Masomo ya Mwaka "B".

SOMO  1: Mdo. 10:34, 37- 43
Somo katika kitabu cha Matendo ya Mitume.
  Petro akafumbua kinywa chake, akasema, Jambo lile ninyi mmelijua, lilionea katika Uyahudi wote likianzia Galilaya, baada ya ubatizo aliohubiri Yohane; habari za Yesu wa Nazareti, jinsi Mungu alivyomtia mafuta kwa Roho Mtakatifu na nguvu; naye akazunguka huko na huko, akitenda kazi njema na kuponya wote walioonewa na Ibilisi; kwa maana Mungu aikuwa pamoja naye. Nasi tu mashahidi wa mambo yote yaliyotendeka katika nchi ya Wayahudi na katika Yerusalemu; ambaye walimwua wakamtundika mtini. Huyo Mungu alimfufua siku ya tatu, akamjalia kudhihirika, si kwa watu wote, bali kwa mashahidi waliokuwa wamekwisha kuchaguliwa na Mungu, ndiyo sisi, tuliokula na kunywa naye baada ya ufufuka kwake kutoka kwa wafu. akatuagiza tuwahubiri watu na kushuhudia ya kuwa huyu ndiye aliyeamriwa na Mungu awe mhukumu wa wahai na wafu. Huyo manabii wote humshuhudia, ya kwamba kwa jina lake kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi.

WIMBO WA KATIKATI. 
Zab. 118:1-2, 16-17, 22-23. 
1.Aleluya.
            Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema
  kwa maana fadhili zake ni za milele.
           Israeli na aseme sasa,
    Ya kwamba fadhili zake ni za milele.

K. siku hii ndiyo aliyoifanya Bwana, Tutashangilia na kuifurahia.

2. Mkono wa kuume wa Bwana umetukuzwa;
                   Mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu.
     Sitakufa bali nitaishi,
                   Nami nitayasimulia matendo ya Bwana.
(K)
3. Jiwe walilolikataa waashi
                Limekuwa jiwe kuu la Pembeni.
     Neno hili limetoka kwa Bwana,
                Nalo ni ajabu machoni petu (K)

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR