Showing posts with label mwaka 2015.. Show all posts
Showing posts with label mwaka 2015.. Show all posts

Monday, October 12, 2015

WAJUE WAGOMBEA WA URAIS TANZANIA 2015

Tukiwa tunakaribia kabisa tarehe 25/10/2015, hebu leo tujikumbushe wasifu wa Wagombe wa Urais na vyama vyao.

1. Mh. Edward Ngoyai Lowassa KUPITIA CHAMA CHA CHADEMA NA KUUNGWA MKONO NA UKAWA.

 

WASIFU:   

Edward Ngoyai Lowassa alizaliwa tarehe 26 August 1953, katika kijiji cha Ngarash wilayani Monduli mkoa wa Arusha, akiwa ni mtoto wa 4 kati ya watoto 23 wa mzee Ngoyai Lowassa. 
ELIMU:
1961 – 1967: shule ya msingi Monduli1968-1971: shule ya sekondari Arusha1972 – 1973: St. Marry’s High School (Milambo High School) Tabora.1983 – 1984: Chuo Kikuu cha BATH Uingereza M.Sc (Development Studies).
UZOEFU KAZINI
1995 – 2000 – Waziri nchi ofisi ya makamu wa Rais Mazingira, Muungano nakuondoa umasikini. 2000 -2005 – Waziri wa maji na maendeleo ya mifugo.
Desemba 2005 Februari 2008 Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
1985 – 2005 – Mbunge wa Monduli (ccm).
2010 – 2011 – Mwenyekiti Kamati ya bunge ya ulinzi na usalama na mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa .
 2011 – 2015 – Mwenyekiti kamati ya bunge ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa. 
28/07/2015 – Kujitoa CCM na kujiunga na CHADEMA 

Mhe. Edward Lowassa amemuoa Regina Lowassa na kujaliwa kupata watoto watano, watatu wa kiume na wawili wa kike

 Edward Lowassa ni shabiki wa michezo na alikuwa mchezaji mzuri wa mpira wa kikapu.

2. Dk. John Pombe Magufuli kupitia cha cha  CCM

 -1x-1

WASIFU: 

 John Pombe Magufuli alizaliwa Oktoba 29, 1959 katika Wilaya ya Chato ambayo ni mojawapo ya wilaya tano za mkoa mpya wa Geita uliopo kaskazini magharibi mwa Tanzania.

Wilaya ya Chato ilikuwa sehemu ya Wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera na ni mwaka 2012 tu ndipo ilipohamishiwa Mkoa wa Geita. Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012, Chato ina jumla ya wakazi 365, 127. 
ELIMU
Magufuli alipata elimu ya msingi katika Shule ya Chato na masomo ya sekondari ya awali katika Seminari ya Katoke, Biharamulo. Alimalizia kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Lake, mkoani Mwanza. Kidato cha sita alimalizia katika sekondari ya Mkwawa mkoani Iringa.
Wasifu wa Magufuli unaonyesha kwamba alipata cheti cha Stashahada ya Ualimu katika Chuo cha Elimu Mkwawa mnamo mwaka 1982 – alikojikita zaidi katika masomo ya hisabati na kemia.
Kati ya mwaka 1985 hadi 1988, Magufuli alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa ajili ya masomo yake ya shahada ya kwanza ya ualimu wa kemia na hisabati.
UZOEFU KAZINI
John Pombe Magufuli ni mwanasiasa Mtanzania wa CCM ambaye aliwahi kutumikia Baraza la Mawaziri la Tanzania, kama Waziri wa Ujenzi tangu 2010. Hapo awali alikuwa Naibu Waziri wa Ujenzi tangu 1995 hadi 2000, Waziri wa Ujenzi tangu 2000 hadi 2006, Waziri wa Ardhi na Makazi tangu 2006 hadi 2008, na Waziri wa Mifugo na Uvuvi kutoka 2008 hadi 2010. Aliwahi kuwa Mbunge wa jimbo la Chato tangu mwaka 1995. Yeye ndiye mgombea Urais wa CCM katika uchaguzi mkuu wa 2015.

3. Mh. Anne E. Mghwira kupitia chama cha ACT-Wazalendo

 WASIFU: 
 Bi. Anna Mghwira ni mwenyekiti wa kitaifa wa chama kipya cha siasa, ACT – Wazalendo. Alizaliwa tarehe 23 Januari 1959 katika hospitali ya mkoa wa Singida, Kata ya Mungumaji, Kitongoji cha Irao manispaa ya Singida Mjini. (Mwezi Januari mwaka huu ametimiza miaka 56).
Baba mzazi wa Anna alikuwa diwani na kiongozi wa TANU kabla ya CCM hadi mwaka 1985, mama yake alijishughulisha na kilimo na ufugaji na wazazi hawa kwa ujumla walijipatia watoto tisa, akiwemo Bi. Anna.
ELIMU
Anna aliendelea na masomo ya Chuo Kikuu mwaka 1982 baada ya kujiunga Chuo Kikuu cha Thiolojia (Chuo Kikuu cha Tumaini) na kuhitimu shahada ya Thiolojia mwaka 1986.
Mwaka huohuo 1986 alijiunga Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam akitafuta shahada ya Sheria na akaimaliza na kutunukiwa mwaka 1986.
Kati ya mwaka 1987 – 1998, Bi Anna aliendelea na shughuli za ujenzi wa Taifa, akifanya kazi ndani na nje ya nchi na kupata uzoefu mkubwa sana.
Safari ya Elimu ya Bi. Anna ilikamilikia Chuo Kikuu cha Essex nchini Uingereza ambako alianza shahada ya uzamili ya sheria (LLM) mwaka 1999 na kutunukiwa mwaka 2000.
Licha ya kuwa mwanasheria na mtheologia aliyebobea, pia amefanya kazi za maendeleo kwa muda mrefu na ana uzoefu katika uendeshaji wa serikali za mitaa, uzoefu wa utumishi katika mashirka ya kimataifa, kitaifa na mashirika ya dini ambamo amejihusisha na masuala ya wanawake, watoto, wakimbizi, utawala na haki za binadamu.
Anna  alianza siasa tangu wakati wa TANU akiwa ni mwanachama wa Umoja wa Vijana wa Tanu (Tanu Youth League) na aliwahi kushinda tuzo mbalimbali kutokana na ushiriki wa juu katika TANU lakini baadaye ilipoanzishwa CCM alipunguza ushiriki wake ili ajipe muda katika masomo na baadaye ndoa na malezi ya watoto.
Kwa kipindi kirefu hakuwa anajihusisha na siasa hadi alivyoamua kujiunga na CHADEMA mwaka 2009 ambako alishika nafasi mbili tu za Uenyekiti wa baraza la wanawake ngazi ya wilaya na Katibu wa Baraza la wanawake Mkoa.
Mwezi Machi 2015 alijiunga rasmi na chama cha ACT – Wazalendo na katika Mkutano Mkuu wa kwanza wa chama hicho, yeye ndiye akachaguliwa kuwa mwenyekiti wa kwanza wa ACT.
 August 20 2015 ACT walikaa Kikao Dar na kuyapitisha Majina mawili, Anna Elisha Mgwira kuwa Mgombea wao wa Urais kwenye Uchaguzi Mkuu wa Tanzania  October 2015 na Mussa Yusuph kuwa Mgombea Mwenza wake.

4. Hashim Rungwe Spunda- Chama cha 

Ukombozi wa Umma (CHAUMA)

 


WASIFU wa Hashim Rungwe Spunda.
Hashim Rungwe Spunda, ni Wakili wa Mahakama Kuu ya Tanzania akifanya kazi zake kama wakili binafsi. Alizaliwa tarehe 01 Januari 1949 katika eneo la Ujiji, mkoani Kigoma (Ametimiza miaka 66 mwezi Januari mwaka huu). Hashim Rungwe ameoa na ana watoto watano.
ELIMU.
Mwaka 1975 alisoma ngazi ya Cheti katika Taasisi ya Kukuza Mauzo (Tafsiri yangu) ya Dar Es Salaam, mwaka 1977 alisoma Lugha ya Kifaransa kwa ngazi ya cheti katika taasisi ya “Alliance Francais” ya jijini Dar Es Salaam na kisha akasoma lugha ya kiarabu na elimu ya dini ya kiislamu kwa ngazi ya shahada katika Chuo Kikuu cha Mfalme Abdul kilichoko Saudi Arabia kati ya mwaka 1979 – 1982.
Mwaka 1989 – 1989 alisoma Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam ngazi ya Cheti, akichukua masomo ya Usimamizi wa Umma lakini pia mwaka 1991 alisoma ngazi ya cheti hapo hapo Chuo Kikuu, akijikita katika eneo la Historia ya Afrika na Falsafa ya Historia na Masuala ya Maendeleo (Tafsiri yangu).
Hashim aliendelea zaidi kielimu alipoamua kubobea katika sheria, alijiunga na Chuo Kikuu Huria Tanzania na kusoma shahada ya sheria kuanzia mwaka 1996 na kuhitimu mwaka 2003 na mwaka huohuo 2003 akasajiliwa kuwa wakili wa Mahakama Kuu ya Tanzania.
Kwa upande wa ajira, Hashim amefanya kazi na mashirika mbalimbali ya ndani ya nchi. Kwa mfano, kuanzia mwaka 1969 hadi 1973 amekuwa ni Ofisa aliyeajiriwa serikalini na kufanya kazi katika idara mbalimbali za sekta ya umma.
Kisiasa, Hashim aliwahi kuwa mwanachama imara wa TANU kati ya mwaka 1966- 1977 na kisha CCM kati ya mwaka 1977 – 1995. Ndiyo kusema kuwa wakati mfumo vyama vingi unaanzishwa mwaka 1992 yeye alikuwa mwanachama wa CCM kwa miaka mitatu zaidi kabla ya kuhamia NCCR Mageuzi mwaka 1996.
Alipokuwa NCCR alishiriki hatua mbalimbali za chama hicho katika kupigania mabadiliko, lakini alijiondoa NCCR mwaka 2012 na kuanzisha chama cha siasa kinachojulikana kama CHAMA CHA UKOMBOZI WA UMMA (CHAUMMA) na baada ya kuanzisha chama hicho alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kitaifa wa CHAUMMA mwaka 2014 na anashikilia wadhifa huo hadi hivi sasa.

 

 5.Fahmi Nasoro Dovutwa- Chama cha United Peoples Democratic Party (UPDP)
 
WASIFU: Historia yake Fahmi Nasoro Dovutwa ni Mwenyekiti wa kitaifa wa Chama cha United Peoples Democratic Party (UPDP). Alizaliwa Februari 27, 1957 mjini Kisarawe mkoani Pwani (Amefikisha miaka 58 Februari mwaka huu).
4. Hashim Rungwe Spunda
1 2 3

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR