Showing posts with label Masomo ya Tarehe 01/02/2015. Show all posts
Showing posts with label Masomo ya Tarehe 01/02/2015. Show all posts

Sunday, February 1, 2015

Masomo ya Tarehe 01/02/2015, Jumapili: Dominika ya 4 ya Mwaka "B".

01

February

 Jumapili: Dominika ya 4 ya Mwaka "B".
SOMO  1. Kumb. 18:15-20

 Bwana, Mungu wako, atakuondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zako kama nilivyo mimi; msikilizeni yeye. Kama vile ulivyotaka kwa Bwana, Mungu wako, huko horebu, siku ya kusanyiko, ukisema, nisisikie tena sauti ya Bwana, Mungu wangu, wala nisiuone tena moto huo mkubwa, nisije nikafa. Bwana akaniambia, wametenda vyema kusema walivyosema . Mimi nitawaondoshea Nabii miongoni mwa ndugu zao mfano wako wewe, nami nitatia maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru. Hata itakuwa, mtu asiyesikiliza maneno yangu atakayosema yule kwa jina langu, nitalitaka kwake. Lakini Nabii atakayenena neno kwa kujikinai kwa jina langu, ambalo sikumwagiza kulinena, au atakayenena katika jina la miungu mingine, nabii yule atakufa.

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR