Friday, October 31, 2014

MAFUNZO YA WALIMU WA WALIMU wa UJASILIAMALI


 Mafunzo ya walimu wa walimu "Training of Trainers" kuhusu ujasiliamali yatatolewa kwa Halmashauri za VIWAWA za Parokia za BOKO na BUNJU siku ya Tarehe 08/11/2014 kwenye ukumbi wa Masista wa Karmeli Boko. Mafunzo yamepangwa kuanza saa 2:00 asubuhi. Pamoja na viogozi hao kijana yoyote mwenye nia na anayependa kuhudhuria anakaribishwa.

Tofauti na mafunzo mengine ya Ujasilimali ambayo hufundisha mfano: - jinsi ya kuzalisha bidhaa mbalimbali, mafunzo haya yatalenga katika kumwezesha kijana kutambua na kuzitumia mbinu zifuatazo: -

  • Je unataka kuzifahamu "Sifa 12 za mjasilimali mwenye mafanikio?"
  • Je unafahamu "Kanuni saba ambazo humuungoza mjasiliamali?"
  • Je unafahamu kuwa "biashara/ huduma/ bidhaa inao mzunguko wa maisha  na Ipo misingi ya kubadili biashara/ bidhaa husika iwapo haileti faida yoyote?".
  • Je ungependa "kubuni biashara mpya kabisa?"
  • Je ungependa kufahamu jinsi ya "Kuchagua bidhaa au huduma gani iwe biashara yako?"
  • Jifunze "Mbinu za kuingiza biashara/ bidha/ huduma sokoni"
  • Jifunze kuhusu "Vyanzo vya mitaji"
  • Jifunze kujiandalia mchanganuo wa biashara yako kwa kutumia "Njia rahisi ya kutayarisha mchanganuo wa biashara"

Hizi ni baadhi ya elimu utakazopata katika mafunzo haya na pia mengine mengi katika mfululizo wa mafunzo siku zijazo. Kumbuka Biashara inaishi, hukua na hubadilika, hivyo katika kila hatua mbinu muafaka zinahitajika ili isife.

 Mafunzo haya yamegawanyika kama ifuatavyo: - 40% nadharia na 60% jinsi ya kutenda. Kijana ukitoka katika mafunzo haya ya awali utajengwa kuwa mwalimu ambaye utashiriki kuongeza timu ya walimu wa ujasiliamali. Pia utaweza kubuni biashara yako mwenyewe na jinsi ya kuiingiza kwenye soko lenye ushindani mkali.

Mwana halmashauri, na kijana USIKOSE fursa hii adimu kwa gharama nafuu sana Jiandikishe sasa. Kwa mawasiliano piga simu namba 0713 900 905,0784 799 455, 0765 755 519 na0714 118 788


Mapendo…..



NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR