Showing posts with label MAUAJI YA SISTER KAPULI WA MAKOKA. Show all posts
Showing posts with label MAUAJI YA SISTER KAPULI WA MAKOKA. Show all posts

Thursday, June 26, 2014

MAJAMBAZI WALIOMUA MTAWA ( SISTER KAPULI) WA MAKOKA

POLISI Kanda Maalumu ya Dar es Salaam imeanzisha msako mkali, kuwatafuta watu waliohusika na mauaji ya Mhasibu wa Kanisa Katoliki Parokia ya Makoka jijini Dar es Salaam, Sista Cresencia Kapuri (50), ambao utahusisha vikosi vyote vya Polisi. Vikosi hivyo ni Usalama Barabarani, askari wa doria wanaotumia pikipiki na magari, wapelelezi na askari Polisi wa kawaida.
 
Mauaji ya mtawa huyo, yalitokea juzi mchana katika eneo la Ubungo Riverside, jijini humo, ambapo alipigwa risasi na watu wanaodaiwa kuwa ni majambazi na kumpora Sh milioni 20 pamoja na nyaraka mbalimbali za ofisi.
 
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Mkoa wa Dar es Salaam, Suleiman Kova, aliwaambia waandishi wa habari ofisi kwake jana kuwa Sista Cresencia wakati anapigwa risasi, alikuwa ameongozana na wenzake, ambao ni Sista Brigita Mbaga (32) na dereva wao Mark Mwarabu, aliyekuwa akiendesha gari aina ya Toyota Hilux Pick-Up, yenye namba T213 CJZ.
 
Kova alisema wakati watawa hao, wakitoka katika Benki ya CRDB Tawi la Mlimani City, walipofika Ubungo Riverside kulipa deni la chakula katika duka la Thomas Francis, ndipo walitokea watu hao wawili wanaodaiwa kuwa ni majambazi wakiwa na pikipiki, ambayo haikusomeka namba, huku mmoja akiwa na bunduki aina ya SMG.
kova  
“Yule dereva wa gari la masista walimpiga risasi katika kidole gumba cha mkono wa kulia na kisha kumpiga mtawa huyo risasi ya kifuani na kupora kiasi hicho cha fedha na nyaraka hizo,” alisema Kova. 
 
Alisema kuwa jambo kubwa walilogundua ni kuwa matukio mengi ya ujambazi, hasa unaohusisha wananchi kuporwa kiasi kikubwa cha fedha, yanaanzia katika mabenki, hivyo kuna uwezekano wa watu ambao si waaminifu, wanafanya uhalifu huo.
 
Alisema kuwa katika matukio ya aina hiyo, majambazi huwafuatilia wateja wanapoingia au kutoka katika benki mbalimbali.
 
Alisema imeonekana kwamba mara nyingi benki, zinapohitaji kusafirisha pesa nyingi, hutumia askari au taasisi nyingine za usalama kusafirisha fedha zao.

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR