Saturday, February 21, 2015

Masomo ya Dominika ya Kwanza ya Kwaresima Mwaka 'B' wa Kanisa 2015

21

 FEBRUARY
 Jumapili ya 1 ya Kwaresima Masomo ya Mwaka "B".
SOMO  1: Mwa. 9:8 - 15

Somo katika kitabu cha Mwanzo.
Mungu akamwambia Nuhu, na wanae pamoja naye, akisema, mimi, tazama, nalithibitisha agano langu nanyi, tena na uzao wenu baada yenu; tena na kila kiumbe hai kilichoko pamoja nanyi; ndege na mnyama wa kufungwa, na kila mnyama wa mwitu katika nchi. Na agano langu nitalithibitisha nanyi; wala kila chenye mwili hakitafutwa tena kwa maji ya gharika, wala hakutakuwa tena gharika,baada ya hayo, kuiharibu nchi. Mungu akasema, hii ndiyo ishara ya agano nifanyalo kati yangu na ninyi, na kila kiumbe hai kilichoko pamoja nanyi, kwa vizazi vyote hata milele; Mimi nauweka upinde winguni, nao utakuwa ni ishara ya agano kati yangu na nchi. Hata itakuwa nikitanda mawingu juu ya nchi, upinde utaonekana winguni, nami nitalikumbuka agano langu, lililoko kati yangu na ninyi, na kila kiumbe hai katika wote wenye mwili, wala maji hayatakuwa gharika tena kuwaharibu wote wenye mwili.

WIMBO WA KATIKATI. Zab. 25:4-9, (k) 10. 
K. Njia zote za Bwana ni fadhili na kweli, kwao walishikao agano lake na shuhuda zake..

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR