Saturday, November 1, 2014

Ben Kiko enzi za uhai wake


 



Ben Kiko Hatunaye tena!

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia Salamu za Rambirambi Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Mheshimiwa Dkt. Fenela Mukangara kuomboleza kifo cha aliyekuwa Mtangazaji na Mwandishi Mkongwe na Mahiri hapa nchini wa iliyokuwa Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD) ambayo kwa sasa ni TBC Taifa, Ben Hamis Kikoromo maarufu kama Ben Kiko.

Ben Kiko amefariki dunia usiku wa kuamkia tarehe 31 Oktoba, 2014 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) Jijini Dar es Salaam alikokuwa amelazwa akiendelea na matibabu ya figo baada ya kuhamishiwa hapo akitokea Hospitali ya Jeshi ya Milambo Mkoani Tabora. “Nimeshtushwa, nimesikitishwa na kuhuzunishwa sana kutokana na taarifa za kifo cha Mwanahabari na Mtangazaji huyu Mahiri ambaye ametoa mchango mkubwa wa kihabari kwa Taifa letu”, amesema Rais Kikwete akiomboleza msiba wa Ben Hamis Kikoromo.

“Namkumbuka Marehemu Ben Kiko, enzi za uhai wake, kama Mtangazaji aliyekuwa na mvuto mkubwa kwa wasikilizaji wake kutokana na namna yake ya kipekee ya kuripoti matukio hususan katika kipindi kilichojizolea umaarufu mkubwa wakati huo cha MAJIRA kilichokuwa kikirushwa hewani na Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD)”.

Wakati wa vita dhidi ya Nduli Idi Amin wa Uganda mwaka 1978, Ben Hamis Kikoromo alifanya kazi kubwa kwa Taifa kwani aliweza kuripoti matukio mbalimbali kutoka katika uwanja wenyewe wa vita, na hivyo kuliwezesha Taifa na wananchi kwa ujumla kuhabarika vilivyo na matukio yaliyokuwa yakiendelea.

“Kutokana na msiba huu mkubwa, pokea salamu zangu za Rambirambi kutoka dhati ya moyo wangu kwa kumpoteza mmoja wa Waandishi na Watangazaji Mahiri katika Tasnia ya Habari hapa nchini.

Vilevile kupitia kwako, naomba Salamu zangu za Rambirambi na pole nyingi ziifikie Familia ya Marehemu Ben Hamis Kikoromo kwa kupoteza Kiongozi na Mhimili Madhubuti wa Familia. Nawaomba Wanafamilia wote, ndugu na Jamaa wa Marehemu wawe wavumilivu na wenye subira wanapoomboleza kifo cha mpendwa wao huku wakitambua kuwa yote ni mapenzi yake Mola”, amesema Rais Kikwete.

Amewahakikishia Wanafamilia kuwa yuko pamoja nao katika muda wote wa maombolezo, na anamuomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema aipokee na kuilaza mahala pema peponi Roho ya Marehemu Ben Hamis Kikoromo, Amina.

Aidha Rais Kikwete ametuma Salamu za Rambirambi kwa Wanahabari kote nchini ambao kwa hakika msiba wa Ben Kiko utakuwa umewagusa kwa karibu. Hata hivyo amesema kuondoka kwa Ben Kiko kusiwe chanzo cha wao kukata tamaa, bali kifo chake hakina budi kuwa chachu katika kujituma zaidi, na wawe tayari kuiga yote mazuri aliyoyafanya Marehemu enzi za uhai wake hapa duniani hususan katika Taaluma ya Uandishi wa Ha

Chelsea, Arsenal safi

*Liverpool waoga kichapo kwa Newcastle
Chelsea wameendeleza rekodi ya kutofungwa baada ya kuwachapa QPR 2-1, Arsenal wakavuna pointi tatu na mabao matatu bila majibu kwa Burnley huku Liverpool wakipoteza mechi.
Chelsea sasa wanaongoza kwa tofauti ya pointi nne, baada ya kufikisha 26 katika michezo 10, wakiwa mbele ya Southampton. Diego Costa alirejea dimbani baada ya kukosekana katika mechi nne zilizopita, lakini hakufunga bao.
QPR walicheza vyema na kuwabana wenyeji, kwani hadi dakika ya 74 mabao yalikuwa 1-1, Chelsea wakaja kubahatika kwa bao la penati la Eden Hazard dakika moja baadaye na kutoka na ushindi. Bao jingine lilifungwa na Oscar wakati la QPR lilifungwa na Charlie

ncastle
Kocha Jose Mourinho amesema hakufurahia ushindi huo akisema timu yake hawakucheza vizuri, tofauti na alivyotarajia. Kocha wa QPR, Harry Redknapp alisononeshwa na penati iliyotolewa, akisema haikuwa haki.
Katika mechi nyingine Arsenal wamewafurahisha washabiki wao kwa kuwatandika Burnley 3-0 kwa mabao mawili ya Alexis Sanchez ambaye kwa msimu huu amefikisha 10 wakati furaha nyingine ilikuwa kwa beki kinda Calum Chambers aliyefunga bao lake la kwanza tangu aanze kuchezea timu ya wakubwa.
Theo Walcott alicheza kwa mara ya kwanza tangu alipoumia Januari, akichukua nafasi ya Alex Oxlade-Chamberlain dakika 10 kabla ya mechi kumalizika na Arsene Wenger anasema alivyocheza ni dhahiri atarudi kwenye hali yake ya kawaida mapema.
Newcastle wameendelea kufufuka ambapo wamefanikiwa kuwalaza Liverpool 1-0, hali inayozidi kumfedhehesha kocha wa Liverpool, Brendan Rodgers na kumpa ahueni kubwa yule wa Magpies, Alan Pardew.
Bao pekee la mchezo lilifungwa na Perez Guiterez katika dakika ya 73, ukiwa ni ushindi wa tatu mfululizo wakati Liverpool wamefikisha mechi mbili bila ya kufunga hata bao moja. Watu walikuwa wakimwangalia Mario Balotelli awe mkombozi wa Liver, lakini sasa amefikisha mechi nane pasipo kuzifumania nyavu.

1414871851910_wps_16_Chelsea_Manager_Jose_Mour

Siku kuu ya Watakatifu Wote!

Tunakuletea habari njema ya furaha tunapotafakari pamoja Neno la Mungu katika sherehe ya Watakatifu wote. Mama Kanisa akitaka kuhitimisha mwaka wa Kanisa kwa furaha anaona ni vema awaoneshe watoto wake lengo la maisha ya kikristu yaani ni kuelekea maisha ya utakatifu, maisha ya ya milele mbinguni. 

Kumbe, Mama Kanisa amependa kila tarehe 1Novemba ya kila mwaka, sherehe hii iadhimishwe katika Kanisa zima la ulimwengu. Adhimisho hili ni mwaliko kwetu kuchuchumalia maisha yanayotimiza mapenzi ya Mungu, maisha ya ufufuko ambayo Mtume Paulo anatuambia daima akisema basi mkishafufuliwa mkayatazame yaliyo ya juu!

Mpendwa, yafaa kutambua watakatifu ni akina nani? Watakatifu ni wale wanaokaa na Mungu katika kiti chake cha enzi kadiri tusomavyo katika kitabu cha Ufunuo. Ni marafiki wa kweli au tunaweza kusema ni marafiki wa dhati au wa kina. Katika lugha yangu ya kihaya Watakatifu tunaweza kuwalinganisha na “Abatahanju” yaani wale ambao huingia ndani ya nyumba mpaka sebule ya nyuma na hata jikoni.

Ni wale ambao hula chakula pamoja na mkuu wa familia, na hivi wanafurahi pamoja na Mungu Baba huko mbinguni. Ni wale ambao Injili ilikuwa chakula chao cha kila siku walipokuwa duniani na walijikabidhi katika mikono ya Mungu na kuwa mali yake. Ni wale walioishi heri nane mafundisho ya Kristu aliyoyatoa pale mlimani. Ni wale ambao walitunza neema ya UTAKASO waliyoipokea wakati wa Ubatizo.

Ni wale ambao walimpenda Mungu kwa moyo wao wote, kwa akili yao yote na kwa nguvu zao zote na kisha wakampenda jirani aliyeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu. Ni wale ambao katika ubinadamu wao walikubali mateso wakitambua na kujua siri ya furaha watakayoipata milele. Sasa wanafurahia matunda ya msalaba wa Kristu. Kwa kifupi ni wale walioshika vema amri kuu ya mapendo.

Ili basi nasi tuweze kufikia hali hiyo iliyo heri na furaha upeo, somo la kwanza linaweka mwaliko kwa watu wote kuwa, ili mmoja aweze kupokea heri za milele yaani utakatifu, ni lazima kufua mavazi katika Damu ya Mwanakondoo. Ni lazima kukinywea kikombe kimoja cha Damu Takatifu iliyo thamani ya wokovu kwa wote. Ndiyo kusema ni kuishi kwa kutimiza mapenzi ya Mungu.

Kwa kufua mavazi katika Damu ya Mwanakondoo kunamwondoa mtu katika dhiki ya dhambi na dhiki ya upungufu wa upendo mkamilifu. Mmoja ananyakuliwa toka taabu ya ulimwengu geugeu na kuvikwa mavazi meupe ndiyo utakaso mkamilifu unaowezesha kuimba baraka na utukufu na hekima na shukrani na heshima na uweza na nguvu zina Mungu wetu hata milele na milele. Amina. Huu ni wimbo wa sifa kwa Mungu ambao unaweza kuimbwa na walio wake, ndiyo watakatifu.

Katika Injili ya Mathayo tunapata mafundisho ya Yesu mlimani yaani Heri Nane. Bwana anaonesha njia ya kufikia utakatifu, njia ya kuishi mapenzi ya Mungu. Anaainisha namna ya kufika mbinguni, akisema, wanaheri wale walio maskini wa roho maana ufalme wa mbinguni ni wao. Wanaheri wenye upole maana watairithi nchi. Anazidi kukazia utakaso wa roho akisema heri wenye moyo safi maana hao watamwona Mungu. Hizi ni baadhi ya heri nane za mlimani njia kamilifu ya kufikia utakatifu.

Kwa kuzitafakari heri nane tunaweza kusema mambo makuu mawili ni lazima katika kufikia utakatifu. Jambo la kwanza ni kujitenga na chachu ya ulimwengu. Kumbuka Bwana anasali na kusema tuko ulimwenguni lakini sisi si wa ulimwengu. Hii yamaanisha kujitenga na kile kinachopingana na injili ya Bwana, na hivi kuwa maskini wa roho. Kumbe mkristu anapaswa ajisikie daima kinyume na mawimbi ya ulimwengu yanayopingana na Injili. Jambo la pili ni lile la kupokea kikombe cha mateso daima na kulitangaza jina la Bwana.

Mateso haya hugeuka na kuwa furaha katika maisha ya mkristu sasa anapoishi na baadaye. Mtakatifu lazima aoneshe sura ya Kristu mteswa na mwenye furaha kwa ajili ya ukombozi wa ulimwengu. Mtakatifu ni lazima amwilishe Heri Nane katika maisha yake na hivi zingae daima na kuwa kielelezo cha maisha ya upendo. >>>>
Endelea hapa

Katiba Mpya ya watanzania isome hapa

Maadhimisho ya Jubilee ya Miaka 50 ya Jimbo Katoliki Mahenge.

Jimbo Katoliki la Mahenge, Tanzania, linaadhimisha kilele cha Jubilee ya miaka 50 tangu lilipoanzishwa kunako mwaka 1964 na Marehemu Askofu Elias Mchonde aliyekuwa Askofu msaidizi wa Jimbo la Dar es Salaam akateuliwa kuwa Askofu wa kwanza wa Jimbo Katoliki la Mahenge na kuliongoza Jimbo hili kuanzia wakati huo hadi mwaka 1969 alipofariki dunia. Baadaye Jimbo limeongozwa na Askofu Nikas Kipengele tangu mwaka 1970 hadi mwaka 1971; Askofu Patrick Iteka kuanzia mwaka 1973 hadi mwaka 1993.
Askofu Agapiti Ndorobo akapewa dhamana ya kuwaongoza waamini wa Jimbo Katoliki la Mahenge tangu mwaka 1995 hadi wakati huu, Jimbo linapomwimbie Mwenyezi Mungu utenzi wa shukrani na sifa kwa kuadhimisha Jubilee ya Miaka 50 ya uwepo wake. Askofu Ndorobo ameliongoza Jimbo kwa miaka 19 sasa. Katika mahojiano maalum na Radio Vatican anabainisha: mafanikio na changamoto anazokabiliana nazo katika kuwaongoza, kuwafundisha na kuwatakatifuza Watu wa Mungu Jimboni Mahenge.Itakumbukwa kwamba, Jimbo Katoliki la Ifakara lililoanzishwa na Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI kunako mwaka 2012 na Askofu Salutaris Melchior Libena kuteuliwa akuwa Askofu wake wa kwanza ni matunda ya Jimbo Katoliki la Mahenge ambalo hapo awali lilikuwa na Parokia 38 lakini baada ya kuligawa ili kurahisisha shughuli za kichungaji kwa Watu wa Mungu, sasa Jimbo Katoliki la Mahenge lina Parokia 22, likiwa na waamini zaidi ya 215, 000 lakini hapo awali lilikuwa na waamini 487, 000.

Askofu Ndorobo anasema kwamba, katika kipindi cha miaka 50 ya uwepo wa Jimbo Katoliki la Mahenge kumekuwepo na maendeleo makubwa katika medani mbali mbali za maisha, lakini zaidi ni upendeleo kwa maskini na wale wanaosukumizwa pembezoni mwa Jamii. Kuna vituo vya kutunzia wagonjwa wa kifafa, kituo cha wagonjwa wa Ukoma pamoja na kituo cha Watoto Yatima.

Jimbo Katoliki la Mahenge linamiliki na kuendesha Sekondari 5; Vituo vya Afya na Zahanati 9 na kwamba kuna mpango mkakati wa kuanzisha Hospitali ili kujibu kilio cha watu wenye shida na mahangaiko wanaolazimika kutembea umbali mrefu ili kutafuta tiba kwa magonjwa yanayowasumbua, lengo ni kuendelea kutangaza Injili ya Uhai, kwa kutoa kipaumbele cha kwanza kwa binadamu aliyeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu.

Askofu Ndorobo anakiri kwamba, Jimbo la Mahenge limeendelea kuwa na miito mbali mbali ya maisha ya: Kipadre, Kitawa na Ndoa. Kuna vyama vya miito vinavyosaidia mchakato wa malezi ya miito ndani ya Kanisa, kwa njia ya ushuhuda wenye mvuto na mashiko, unaowachangamotisha vijana kupenda kushiriki katika maisha ya Kipadre, Kitawa na Ndoa takatifu.

Askofu Ndorobo anasema miaka 19 ya utume wake kama Askofu wa Jimbo Katoliki Mahenge amekumbana na changamoto nyingi, lakini katika mahojiano na Radio Vatican anagusia changamoto kuu mbili, yaani umuhimu wa Jumuiya Ndogo ndogo za Kikristo na Maisha ya Sala na Kisakramenti. Anasema, kwa miaka hii yote amependa kukazia umuhimu wa waamini kushiriki katika maisha ya Jumuiya ndogo ndogo za Kikristo kwani hizi ni shule ya Sala, Neno la Mungu na kielelezo cha imani tendaji.

Huu ndio mwelekeo ambao anapenda kuuendeleza hata baada ya maadhimisho ya Jubilee ya Miaka 50 ya Jimbo Katoliki Mahenge. Anasema, amependa kukazia umuhimu wa waamini kushiriki kikamilifu katika maisha ya Sala na Sakramenti za Kanisa ili waweze kujichotea neema na baraka; waweze kuonja huruma na upendo kutoka kwa Mwenyezi Mungu, tayari kufanya mabadiliko ya kina katika maisha yao, kwa ajili ya sifa na utukufu wa Mungu. Viongozi wawe ni mfano bora wa maisha ya sala na Sakramenti za Kanisa, ili wao wakiishaimarika, waweze pia kuwaimarisha ndugu zao katika imani, matumaini na mapendo.

Mwaka wa Familia na Vijana(Sinodi imeliwezesha Kanisa kuona na kusikiliza kwa dhati!)

Maadhimisho ya Sinodi maalum ya Maaskofu kwa ajili ya familia ni kielelezo cha mchakato wa Mama Kanisa kutaka kusikiliza kwa dhati kabisa furaha, matatizo na changamoto ambazo familia zinakabiliana nazo katika ulimwengu mamboleo. Ni maneno ya Kardinali Lorenzo Baldisseri, Katibu mkuu wa Sinodi za Maaskofu alipokutana na kuzungumza na Wabunge kutoka Uingereza, waliomtembelea mjini Vatican Alhamisi, tarehe 30 Oktoba 2014.

Katika mazungumzo yake, amewashirikisha wabunge hao mambo makuu yaliyojitokeza wakati wa maadhimisho ya Sinodi maalum ya Maaskofu kwa ajili ya familia pamoja na changamoto zilizoibuliwa na Mababa wa Sinodi. Kadiri ya maelezo yaliyokuwa yanatolewa na baadhi ya vyombo vya habari inaweza kudhaniwa kwamba, maadhimisho ya Sinodi, yalikuwa ni "patashika nguo kuchanika", lakini, kimsingi maadhimisho haya yalikuwa ni mang'amuzi makubwa kwa Mama Kanisa kutembea kwa pamoja na kusikiliza kwa dhati changamoto zinazojitokeza katika maisha na utume wa Kanisa kuhusiana na maisha ya ndoa na familia.

Mafanikio makubwa yaliyojitokeza katika maadhimisho haya ni utambuzi wa umuhimu wa Sinodi katika maisha na utume wa Kanisa, kwa kutambua kwamba, Kristo Mfufuka amewajalia wafuasi wake zawadi ya Roho Mtakatifu, ili kuweza kushiriki kwa ukamilifu katika maisha na utume wa Kanisa. Kanisa litaendelea kujikita katika Mafundisho yake tanzu, Maandiko Matakatifu na Mapokeo, pamoja na kuendelea kusoma alama za nyakati, ili kuweza kukabiliana na changamoto za nyakati hizi.

Kardinali Baldiserri anasema, kati ya changamoto kubwa kwa sasa ni waamini kutalikiana, mwelekeo wa ndoa za watu wa jinsia moja na ndoa za wake wengi. Changamoto hizi zimejadiliwa kwa kina na mapana katika maswali dodoso yaliyotumwa kwa waamini na watu wenye mapenzi mema, jambo ambalo limewasaidia Mababa wa Sinodi kufahamu ukweli wa maisha ya ndoa na familia katika undani wake.

Kuna baadhi ya watu wameshutumu msimamo na ukweli wa Mafundisho ya Kanisa kuhusu ndoa na familia na baadhi yao wamelishauri Kanisa kufanya maamuzi magumu kwa kuzingatia changamoto za watu wa nyakati hizi. Kardinali Baldisseri anasema, jambo la kufurahisha ni kuona kwamba, waamini wanaifahamu Injili na kanuni maadili katika maisha ya ndoa na familia, mambo ambayo hayawezi kuwekwa kando kwani ni sehemu ya vinasaba vya maisha na utume wa Kanisa. Viongozi wa Kanisa wamepewa dhamana ya kuhakikisha kwamba, wanatekeleza utume wao wa kufundisha, kuongoza na kuwatakatifuza Watu wa Mungu kadiri ya mafundisho ya Mama Kanisa.
Maadhimisho ya Sinodi maalum ya Maaskofu kwa ajili ya familia ni kielelezo cha mchakato wa Mama Kanisa kutaka kusikiliza kwa dhati kabisa furaha, matatizo na changamoto ambazo familia zinakabiliana nazo katika ulimwengu mamboleo. Ni maneno ya Kardinali Lorenzo Baldisseri, Katibu mkuu wa Sinodi za Maaskofu alipokutana na kuzungumza na Wabunge kutoka Uingereza, waliomtembelea mjini Vatican Alhamisi, tarehe 30 Oktoba 2014.

Katika mazungumzo yake, amewashirikisha wabunge hao mambo makuu yaliyojitokeza wakati wa maadhimisho ya Sinodi maalum ya Maaskofu kwa ajili ya familia pamoja na changamoto zilizoibuliwa na Mababa wa Sinodi. Kadiri ya maelezo yaliyokuwa yanatolewa na baadhi ya vyombo vya habari inaweza kudhaniwa kwamba, maadhimisho ya Sinodi, yalikuwa ni "patashika nguo kuchanika", lakini, kimsingi maadhimisho haya yalikuwa ni mang'amuzi makubwa kwa Mama Kanisa kutembea kwa pamoja na kusikiliza kwa dhati changamoto zinazojitokeza katika maisha na utume wa Kanisa kuhusiana na maisha ya ndoa na familia.

Mafanikio makubwa yaliyojitokeza katika maadhimisho haya ni utambuzi wa umuhimu wa Sinodi katika maisha na utume wa Kanisa, kwa kutambua kwamba, Kristo Mfufuka amewajalia wafuasi wake zawadi ya Roho Mtakatifu, ili kuweza kushiriki kwa ukamilifu katika maisha na utume wa Kanisa. Kanisa litaendelea kujikita katika Mafundisho yake tanzu, Maandiko Matakatifu na Mapokeo, pamoja na kuendelea kusoma alama za nyakati, ili kuweza kukabiliana na changamoto za nyakati hizi.

Kardinali Baldiserri anasema, kati ya changamoto kubwa kwa sasa ni waamini kutalikiana, mwelekeo wa ndoa za watu wa jinsia moja na ndoa za wake wengi. Changamoto hizi zimejadiliwa kwa kina na mapana katika maswali dodoso yaliyotumwa kwa waamini na watu wenye mapenzi mema, jambo ambalo limewasaidia Mababa wa Sinodi kufahamu ukweli wa maisha ya ndoa na familia katika undani wake.

Kuna baadhi ya watu wameshutumu msimamo na ukweli wa Mafundisho ya Kanisa kuhusu ndoa na familia na baadhi yao wamelishauri Kanisa kufanya maamuzi magumu kwa kuzingatia changamoto za watu wa nyakati hizi. Kardinali Baldisseri anasema, jambo la kufurahisha ni kuona kwamba, waamini wanaifahamu Injili na kanuni maadili katika maisha ya ndoa na familia, mambo ambayo hayawezi kuwekwa kando kwani ni sehemu ya vinasaba vya maisha na utume wa Kanisa. Viongozi wa Kanisa wamepewa dhamana ya kuhakikisha kwamba, wanatekeleza utume wao wa kufundisha, kuongoza na kuwatakatifuza Watu wa Mungu kadiri ya mafundisho ya Mama Kanisa.
Maadhimisho ya Sinodi maalum ya Maaskofu kwa ajili ya familia ni kielelezo cha mchakato wa Mama Kanisa kutaka kusikiliza kwa dhati kabisa furaha, matatizo na changamoto ambazo familia zinakabiliana nazo katika ulimwengu mamboleo. Ni maneno ya Kardinali Lorenzo Baldisseri, Katibu mkuu wa Sinodi za Maaskofu alipokutana na kuzungumza na Wabunge kutoka Uingereza, waliomtembelea mjini Vatican Alhamisi, tarehe 30 Oktoba 2014.

Katika mazungumzo yake, amewashirikisha wabunge hao mambo makuu yaliyojitokeza wakati wa maadhimisho ya Sinodi maalum ya Maaskofu kwa ajili ya familia pamoja na changamoto zilizoibuliwa na Mababa wa Sinodi. Kadiri ya maelezo yaliyokuwa yanatolewa na baadhi ya vyombo vya habari inaweza kudhaniwa kwamba, maadhimisho ya Sinodi, yalikuwa ni "patashika nguo kuchanika", lakini, kimsingi maadhimisho haya yalikuwa ni mang'amuzi makubwa kwa Mama Kanisa kutembea kwa pamoja na kusikiliza kwa dhati changamoto zinazojitokeza katika maisha na utume wa Kanisa kuhusiana na maisha ya ndoa na familia.

Mafanikio makubwa yaliyojitokeza katika maadhimisho haya ni utambuzi wa umuhimu wa Sinodi katika maisha na utume wa Kanisa, kwa kutambua kwamba, Kristo Mfufuka amewajalia wafuasi wake zawadi ya Roho Mtakatifu, ili kuweza kushiriki kwa ukamilifu katika maisha na utume wa Kanisa. Kanisa litaendelea kujikita katika Mafundisho yake tanzu, Maandiko Matakatifu na Mapokeo, pamoja na kuendelea kusoma alama za nyakati, ili kuweza kukabiliana na changamoto za nyakati hizi.

Kardinali Baldiserri anasema, kati ya changamoto kubwa kwa sasa ni waamini kutalikiana, mwelekeo wa ndoa za watu wa jinsia moja na ndoa za wake wengi. Changamoto hizi zimejadiliwa kwa kina na mapana katika maswali dodoso yaliyotumwa kwa waamini na watu wenye mapenzi mema, jambo ambalo limewasaidia Mababa wa Sinodi kufahamu ukweli wa maisha ya ndoa na familia katika undani wake.

Kuna baadhi ya watu wameshutumu msimamo na ukweli wa Mafundisho ya Kanisa kuhusu ndoa na familia na baadhi yao wamelishauri Kanisa kufanya maamuzi magumu kwa kuzingatia changamoto za watu wa nyakati hizi. Kardinali Baldisseri anasema, jambo la kufurahisha ni kuona kwamba, waamini wanaifahamu Injili na kanuni maadili katika maisha ya ndoa na familia, mambo ambayo hayawezi kuwekwa kando kwani ni sehemu ya vinasaba vya maisha na utume wa Kanisa. Viongozi wa Kanisa wamepewa dhamana ya kuhakikisha kwamba, wanatekeleza utume wao wa kufundisha, kuongoza na kuwatakatifuza Watu wa Mungu kadiri ya mafundisho ya Mama Kanisa.

 
Maadhimisho ya Sinodi maalum ya Maaskofu kwa ajili ya familia ni kielelezo cha mchakato wa Mama Kanisa kutaka kusikiliza kwa dhati kabisa furaha, matatizo na changamoto ambazo familia zinakabiliana nazo katika ulimwengu mamboleo. Ni maneno ya Kardinali Lorenzo Baldisseri, Katibu mkuu wa Sinodi za Maaskofu alipokutana na kuzungumza na Wabunge kutoka Uingereza, waliomtembelea mjini Vatican Alhamisi, tarehe 30 Oktoba 2014.

Katika mazungumzo yake, amewashirikisha wabunge hao mambo makuu yaliyojitokeza wakati wa maadhimisho ya Sinodi maalum ya Maaskofu kwa ajili ya familia pamoja na changamoto zilizoibuliwa na Mababa wa Sinodi. Kadiri ya maelezo yaliyokuwa yanatolewa na baadhi ya vyombo vya habari inaweza kudhaniwa kwamba, maadhimisho ya Sinodi, yalikuwa ni "patashika nguo kuchanika", lakini, kimsingi maadhimisho haya yalikuwa ni mang'amuzi makubwa kwa Mama Kanisa kutembea kwa pamoja na kusikiliza kwa dhati changamoto zinazojitokeza katika maisha na utume wa Kanisa kuhusiana na maisha ya ndoa na familia.

Mafanikio makubwa yaliyojitokeza katika maadhimisho haya ni utambuzi wa umuhimu wa Sinodi katika maisha na utume wa Kanisa, kwa kutambua kwamba, Kristo Mfufuka amewajalia wafuasi wake zawadi ya Roho Mtakatifu, ili kuweza kushiriki kwa ukamilifu katika maisha na utume wa Kanisa. Kanisa litaendelea kujikita katika Mafundisho yake tanzu, Maandiko Matakatifu na Mapokeo, pamoja na kuendelea kusoma alama za nyakati, ili kuweza kukabiliana na changamoto za nyakati hizi.

Kardinali Baldiserri anasema, kati ya changamoto kubwa kwa sasa ni waamini kutalikiana, mwelekeo wa ndoa za watu wa jinsia moja na ndoa za wake wengi. Changamoto hizi zimejadiliwa kwa kina na mapana katika maswali dodoso yaliyotumwa kwa waamini na watu wenye mapenzi mema, jambo ambalo limewasaidia Mababa wa Sinodi kufahamu ukweli wa maisha ya ndoa na familia katika undani wake.

Kuna baadhi ya watu wameshutumu msimamo na ukweli wa Mafundisho ya Kanisa kuhusu ndoa na familia na baadhi yao wamelishauri Kanisa kufanya maamuzi magumu kwa kuzingatia changamoto za watu wa nyakati hizi. Kardinali Baldisseri anasema, jambo la kufurahisha ni kuona kwamba, waamini wanaifahamu Injili na kanuni maadili katika maisha ya ndoa na familia, mambo ambayo hayawezi kuwekwa kando kwani ni sehemu ya vinasaba vya maisha na utume wa Kanisa. Viongozi wa Kanisa wamepewa dhamana ya kuhakikisha kwamba, wanatekeleza utume wao wa kufundisha, kuongoza na kuwatakatifuza Watu wa Mungu kadiri ya mafundisho ya Mama Kanisa.

Mababa wa Sinodi katika ukweli na uwazi; kwa moyo wa unyenyekevu na hekima, wameshirikishana mambo msingi ambayo yanaweza kulisaidia Kanisa kuandaa mikakati ya kichungaji kwa ajili ya watu wa ndoa na familia, ili Mama Kanisa aendelee kutangaza Injili ya Familia kwa Watu wa Mataifa. Sinodi ilipania pamoja na mambo mengine kuhakikisha kwamba, inafafanua Mafundisho ya Kanisa kuhusu maisha ya ndoa na familia mintarafu mwelekeo wa kimissionari na kichungaji.

Kanisa linatambua kwamba ni chombo cha wokovu, huruma na upendo, lina dhamana ya kuwapokea na kuwakumbatia wote, watakatifu na wadhambi wanaopaswa kutubu na kumwongokea Mwenyezi Mungu. Mababa wa Sinodi wameshirikisha kuhusu uzuri na utakatifu wa maisha ya ndoa na familia; utu na heshima ya maisha ya ndoa; mambo msingi katika maisha na utume wa Kanisa na Ulimwengu katika ujumla wake.

Dhamana ya Mama Kanisa ni kuendelea kutangaza Injili ya Familia kwa kuzingatia: ukweli na uwazi, kwa unyenyekevu na busara, huku akiwasindikiza wanafamilia wanaogelea katika shida na mahangaiko mbali mbali ya maisha. Kwa kutambua haya yote, hapa Mama Kanisa anataka kupiga hatua nyingine tena kwa kuwaalika watoto wake kutubu na kumwongokea Mungu; daima wakijitahidi kutekeleza mapenzi ya Mungu katika maisha yao; kwa kujenga na kuimarisha umoja na mshikamano wa Kanisa.

Kardinali Baldisseri anasema, huu ndio ukweli wa mchakato wa maadhimisho ya Sinodi maalum ya Maaskofu kwa ajili ya familia, kama walivyoonesha Mababa wa Sinodi na Baba Mtakatifu Francisko akaweka mkazo wa pekee kama mhimili wa umoja na mshikamano wa Kanisa, changamoto kwa waamini kukumbatia kweli za Kiinjili.

Viongozi wa Kanisa wataendelea kuwaganga na kuwaponya waamini wanaokabiliana na madonda makubwa katika maisha ya ndoa na familia, kwa kutumia kweli za Kiinjili na Huruma inayobubujika kutoka kwa Kristo na Kanisa lake. Mada zilizojadiliwa na Mababa wa Sinodi zilikuwa zinagusa maisha ya watu wengi ndiyo maana vyombo vya habari vilikuwa vinafuatilia kwa makini mchakato wa maadhimisho ya Sinodi.

Mababa wa Sinodi wamejitahidi kujikita katika mambo msingi ya maisha ya ndoa na familia; kanuni maadili, utu na heshima ya binadamu; mambo msingi ambayo yanapaswa kutolewa ushuhuda na Wakatoliki katika hija ya maisha yao ya kila siku!
Mababa wa Sinodi katika ukweli na uwazi; kwa moyo wa unyenyekevu na hekima, wameshirikishana mambo msingi ambayo yanaweza kulisaidia Kanisa kuandaa mikakati ya kichungaji kwa ajili ya watu wa ndoa na familia, ili Mama Kanisa aendelee kutangaza Injili ya Familia kwa Watu wa Mataifa. Sinodi ilipania pamoja na mambo mengine kuhakikisha kwamba, inafafanua Mafundisho ya Kanisa kuhusu maisha ya ndoa na familia mintarafu mwelekeo wa kimissionari na kichungaji.

Kanisa linatambua kwamba ni chombo cha wokovu, huruma na upendo, lina dhamana ya kuwapokea na kuwakumbatia wote, watakatifu na wadhambi wanaopaswa kutubu na kumwongokea Mwenyezi Mungu. Mababa wa Sinodi wameshirikisha kuhusu uzuri na utakatifu wa maisha ya ndoa na familia; utu na heshima ya maisha ya ndoa; mambo msingi katika maisha na utume wa Kanisa na Ulimwengu katika ujumla wake.

Dhamana ya Mama Kanisa ni kuendelea kutangaza Injili ya Familia kwa kuzingatia: ukweli na uwazi, kwa unyenyekevu na busara, huku akiwasindikiza wanafamilia wanaogelea katika shida na mahangaiko mbali mbali ya maisha. Kwa kutambua haya yote, hapa Mama Kanisa anataka kupiga hatua nyingine tena kwa kuwaalika watoto wake kutubu na kumwongokea Mungu; daima wakijitahidi kutekeleza mapenzi ya Mungu katika maisha yao; kwa kujenga na kuimarisha umoja na mshikamano wa Kanisa.

Kardinali Baldisseri anasema, huu ndio ukweli wa mchakato wa maadhimisho ya Sinodi maalum ya Maaskofu kwa ajili ya familia, kama walivyoonesha Mababa wa Sinodi na Baba Mtakatifu Francisko akaweka mkazo wa pekee kama mhimili wa umoja na mshikamano wa Kanisa, changamoto kwa waamini kukumbatia kweli za Kiinjili.

Viongozi wa Kanisa wataendelea kuwaganga na kuwaponya waamini wanaokabiliana na madonda makubwa katika maisha ya ndoa na familia, kwa kutumia kweli za Kiinjili na Huruma inayobubujika kutoka kwa Kristo na Kanisa lake. Mada zilizojadiliwa na Mababa wa Sinodi zilikuwa zinagusa maisha ya watu wengi ndiyo maana vyombo vya habari vilikuwa vinafuatilia kwa makini mchakato wa maadhimisho ya Sinodi.

Mababa wa Sinodi wamejitahidi kujikita katika mambo msingi ya maisha ya ndoa na familia; kanuni maadili, utu na heshima ya binadamu; mambo msingi ambayo yanapaswa kutolewa ushuhuda na Wakatoliki katika hija ya maisha yao ya kila siku!
Mababa wa Sinodi katika ukweli na uwazi; kwa moyo wa unyenyekevu na hekima, wameshirikishana mambo msingi ambayo yanaweza kulisaidia Kanisa kuandaa mikakati ya kichungaji kwa ajili ya watu wa ndoa na familia, ili Mama Kanisa aendelee kutangaza Injili ya Familia kwa Watu wa Mataifa. Sinodi ilipania pamoja na mambo mengine kuhakikisha kwamba, inafafanua Mafundisho ya Kanisa kuhusu maisha ya ndoa na familia mintarafu mwelekeo wa kimissionari na kichungaji.

Kanisa linatambua kwamba ni chombo cha wokovu, huruma na upendo, lina dhamana ya kuwapokea na kuwakumbatia wote, watakatifu na wadhambi wanaopaswa kutubu na kumwongokea Mwenyezi Mungu. Mababa wa Sinodi wameshirikisha kuhusu uzuri na utakatifu wa maisha ya ndoa na familia; utu na heshima ya maisha ya ndoa; mambo msingi katika maisha na utume wa Kanisa na Ulimwengu katika ujumla wake.

Dhamana ya Mama Kanisa ni kuendelea kutangaza Injili ya Familia kwa kuzingatia: ukweli na uwazi, kwa unyenyekevu na busara, huku akiwasindikiza wanafamilia wanaogelea katika shida na mahangaiko mbali mbali ya maisha. Kwa kutambua haya yote, hapa Mama Kanisa anataka kupiga hatua nyingine tena kwa kuwaalika watoto wake kutubu na kumwongokea Mungu; daima wakijitahidi kutekeleza mapenzi ya Mungu katika maisha yao; kwa kujenga na kuimarisha umoja na mshikamano wa Kanisa.

Kardinali Baldisseri anasema, huu ndio ukweli wa mchakato wa maadhimisho ya Sinodi maalum ya Maaskofu kwa ajili ya familia, kama walivyoonesha Mababa wa Sinodi na Baba Mtakatifu Francisko akaweka mkazo wa pekee kama mhimili wa umoja na mshikamano wa Kanisa, changamoto kwa waamini kukumbatia kweli za Kiinjili.

Viongozi wa Kanisa wataendelea kuwaganga na kuwaponya waamini wanaokabiliana na madonda makubwa katika maisha ya ndoa na familia, kwa kutumia kweli za Kiinjili na Huruma inayobubujika kutoka kwa Kristo na Kanisa lake. Mada zilizojadiliwa na Mababa wa Sinodi zilikuwa zinagusa maisha ya watu wengi ndiyo maana vyombo vya habari vilikuwa vinafuatilia kwa makini mchakato wa maadhimisho ya Sinodi.

Mababa wa Sinodi wamejitahidi kujikita katika mambo msingi ya maisha ya ndoa na familia; kanuni maadili, utu na heshima ya binadamu; mambo msingi ambayo yanapaswa kutolewa ushuhuda na Wakatoliki katika hija ya maisha yao ya kila siku!
Mababa wa Sinodi katika ukweli na uwazi; kwa moyo wa unyenyekevu na hekima, wameshirikishana mambo msingi ambayo yanaweza kulisaidia Kanisa kuandaa mikakati ya kichungaji kwa ajili ya watu wa ndoa na familia, ili Mama Kanisa aendelee kutangaza Injili ya Familia kwa Watu wa Mataifa. Sinodi ilipania pamoja na mambo mengine kuhakikisha kwamba, inafafanua Mafundisho ya Kanisa kuhusu maisha ya ndoa na familia mintarafu mwelekeo wa kimissionari na kichungaji.

Kanisa linatambua kwamba ni chombo cha wokovu, huruma na upendo, lina dhamana ya kuwapokea na kuwakumbatia wote, watakatifu na wadhambi wanaopaswa kutubu na kumwongokea Mwenyezi Mungu. Mababa wa Sinodi wameshirikisha kuhusu uzuri na utakatifu wa maisha ya ndoa na familia; utu na heshima ya maisha ya ndoa; mambo msingi katika maisha na utume wa Kanisa na Ulimwengu katika ujumla wake.

Dhamana ya Mama Kanisa ni kuendelea kutangaza Injili ya Familia kwa kuzingatia: ukweli na uwazi, kwa unyenyekevu na busara, huku akiwasindikiza wanafamilia wanaogelea katika shida na mahangaiko mbali mbali ya maisha. Kwa kutambua haya yote, hapa Mama Kanisa anataka kupiga hatua nyingine tena kwa kuwaalika watoto wake kutubu na kumwongokea Mungu; daima wakijitahidi kutekeleza mapenzi ya Mungu katika maisha yao; kwa kujenga na kuimarisha umoja na mshikamano wa Kanisa.

Kardinali Baldisseri anasema, huu ndio ukweli wa mchakato wa maadhimisho ya Sinodi maalum ya Maaskofu kwa ajili ya familia, kama walivyoonesha Mababa wa Sinodi na Baba Mtakatifu Francisko akaweka mkazo wa pekee kama mhimili wa umoja na mshikamano wa Kanisa, changamoto kwa waamini kukumbatia kweli za Kiinjili.

Viongozi wa Kanisa wataendelea kuwaganga na kuwaponya waamini wanaokabiliana na madonda makubwa katika maisha ya ndoa na familia, kwa kutumia kweli za Kiinjili na Huruma inayobubujika kutoka kwa Kristo na Kanisa lake. Mada zilizojadiliwa na Mababa wa Sinodi zilikuwa zinagusa maisha ya watu wengi ndiyo maana vyombo vya habari vilikuwa vinafuatilia kwa makini mchakato wa maadhimisho ya Sinodi.

Mababa wa Sinodi wamejitahidi kujikita katika mambo msingi ya maisha ya ndoa na familia; kanuni maadili, utu na heshima ya binadamu; mambo msingi ambayo yanapaswa kutolewa ushuhuda na Wakatoliki katika hija ya maisha yao ya kila siku!

Rasimu ya Tatu ya Katiba Mpya ya Tanzania

click here to download Rasimu ya Tatu  ya Katibu mpya ya Tanzania...

Msomo ya Dominika ya Kumbukumbu ya Marehemu wote, Jumapili ya Tarehe 02/11/2014

02
 November
 Jumapili: Kuwakumbuka Marehemu wote.
SOMO  1. Hek. 3:1-9

Somo katika  Hekima. 
 Roho zao mwenye haki zimo mikononi mwa Mungu, wala maumivu hayatawagusa. Machoni pa watu walio wajinga walionekana kwamba wamekufa, na kufariki kwao kulidhaniwa kuwa ni hasara yaom na kusafiri kwao kutoka kwetu kuwa ni uharibifu wao; bali wao wenyewe wamo katika Imani....
somo 2. Rum. 6:3-9 

Somo katika kitabu cha Warumi. 
Hamfahamu ya kuwa sis sote tulibatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? Bazi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya........


  INJILI.Mt. 25:31-46
Somo katika Injili ilivyoandikwa na Mathayo.

Yesu aliwaambia wanafunzi wake: hapo atakapokuja mwana wa Adamu katika utukufu wake, na Malaika Watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake; na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi; atawaweka kondoo mkono wake wa kuume na Mbuzi mkono wake wa kushoto. Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wa wake wa kuume, njooni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme, mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu; kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu mkanunywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha; nalikuwa uchi ukanivika; nalikuwa mgojwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia, ndipo mwenye haki watakapomjibu, wakisema Bwana, ni lini tulipokuona una njaa, tukakulisha au una kiu tukakunywesha,? Tena ni lini tulipokuona u mgeni, tukakukaribisha, au u uchi, tukakuvika? Ni lini tena tulipokuona u Mgojwa, au kifungoni, tukakujia? Na mfalme atajibu, akiwaambia, Amini nawaambia, Kadri mlivyomtendea mmoja wapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi. Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika Moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na Malaika zake; kwa maana, nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, usininyweshe; nalikuwa mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgojwa, na kifungoni, usije kunitazama. Ndipo hao pia watajibu, wakisema, Bwana ni lini tulipokuona wewe una njaa  , au una kiu, au u mgeni au u uchi, au mgojwa, au u kifungoni, tusikuhudumie? Naye atawajibu akisema, Amini, nawaambia, kadiri msivyomtendea mmojawapo wa hao walio wadogo hamkunitendea mimi. Na hao watakwenda  zao kuingia katika Adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele. 
Ratiba ya Ibada ya Jumapili ya tarehe 02/11/2014
Kigango cha Boko
Misa ya Kwanza- saa 12:15 Mpaka saa 1:45 Asubuhi.
Misa ya Pili        -  saa 2:00 Mpaka saa 3:50 Asubuhi.
Misa ya Tatu     -   saa 4:00 Mpaka saa 5:30 Asubuhi.

Kigango cha  Mt. Rafael Mbweni Malindi

Misa ya Kwanza   - saa 1:00 Mpaka saa 2:50 Asubuhi
Misa ya Pili            - saa 3:00 Mpaka saa 4:50 Asubuhi.

Kigango cha Mt. Fransisco wa Asizi - Mbweni
Misa ya Kwanza - saa 1:15 mpaka saa 2:50 Asubuhi.
Misa ya pili          - saa 3:00 mpaka saa 4:50 asubuhi

Kigango cha Mt. Anthony wa Padua - Mbweni Mpiji
Misa ni saa 3:00 mpaka saa 5:00 asubuhi

masomo ya Sikuku ya Watakatifu Wote 01/11/2014

01
 November
 JUMAMOSI: Sikuku ya Watakatifu Wote. 2014.
SOMO  1. Ufu. 7:2-4, 9-14

Somo katika  kitabu cha ufunuo. 
 Mimi Yohane niliona Malaika mwingine, akipanda kutoka mawio ya jua, mwenye muhuri ya Mungu aliye hai; akawapigia kelele kwa sauti kuu wale Malaika wanne waliopewa kuidhuru nchi na Bahari, akisema, Msiidhuru nchi, wala bahari, wala miti, hata tutakapokwisha kuwatia muhuri watumwa wa Mungu wetu juu ya vipaji vya nyuso zao. Nikasikia hesabu yao waliotiwa muhuri katika kila kabila ya Waisraeli, watu mia na arobaini na nne elfu.......

Somo katika kitabu cha Yohane wa kwanza. 
2. 1Yoh. 3:1-3
Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye. Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo. Na kila mwenye matumaini haya katika yeye hujitakasa; kama yeye alivyo Mtakatifu.


  INJILI.Mt. 21:33-43 
Somo katika Injili ilivyoandikwa na Mathayo.

Yesu alipowaona Makutano, alipanda mlimani; na alipokwisha kuketi, wanafunzi wake walimjia;akafumbua kinywa chake, akawafundisha, akisema, Heri walio Maskini wa Roho; Maana ufalme wa Mbinguni ni wao. Heri wenye Huzuni; maana hao watafarijika, Heri wenye upole, Maana hao watarithi nchi. Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa. Heri wenye rehema; Maana hao watapata rehema. Heri wenye moyo safi; Maana hao watamwona Mungu. Heri wapatanishi; Maana hao wataitwa wana wa Mungu. Heri wenye kuudhiwa kwa ajili ya haki; Maana ufalme wa Mbinguni ni wao. Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu. Furahini na kushangilia; kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; Kwa maana ndivyo walivyowaudhi manabii waliokuwa kabla yenu.

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR