Friday, March 29, 2013
IBADA YA ALHAMISI KUU-POPE FRANCIS
Nimewapeni mfano, nanyi hudumianeni kwa ukarimu na upendo!
Katika mahubiri yake kwa vijana hawa, amewashirikisha upendo ulioneshwa na Yesu Kristo, Siku ya Alhamisi kuu, alipoweka mavazi yake kando, akaanza kuwaosha mitume wake miguu, kitendo ambacho kilimshangaza Mtume Petro, kiasi cha kutaka kukataa katu katu kuoshwa miguu na Yesu, lakini akafafanuliwa maana yake, kiasi kwamba, akaweza hata kuridhika na uamuzi uliotolewa.
Yesu ambaye ni Mwalimu na Bwana, Nafsi ya Pili ya Fumbo la Utatu Mtakatifu, ndiye aliyetekeleza kitendo hiki cha unyenyekevu, ambacho kilikuwa kinafanywa na watumwa! Akawaachia mfano wa kuigwa na kuendelezwa, kwa kutambua kwamba, uongozi ni huduma hasa kwa wanyonge na wale wanaosukumizwa pembezoni mwa Jamii.
Ni mwaliko wa kumegeana upendo unaobubujika kutoka kwa Kristo, aliyewapenda watu wake upeo kiasi cha kuyamimina maisha yake pale juu Msalabani. Huduma ya upendo, iwachangamotishe waamini na watu wenye mapenzi mema kujikita katika msamaha na upatanisho unaopaswa kububujika kutoka katika undani wa mtu mwenyewe.
Baba Mtakatifu Francisko anasema, kama Padre na Askofu wa Roma, anajisikia kuwajibika kuwaonjesha huruma na upendo wa Kristo kwa njia ya huduma inayopata chimbuko lake kutoka katika moyo wake na wala si jambo la kutaka kujionesha mbele ya watu.
Kwa maneno machache, hii ni imani katika matendo, inayowachangamotisha waamini na watu wenye mapenzi mema, kusaidiana kwa hali na mali; wakiungana kwa pamoja kutafuta mafao ya wengi. Huduma ya upendo ni changamoto endelevu inayotolewa na Yesu aliyekuja kutumikia na kuyamimina maisha yake kwa ajili ya ukombozi wa wengi.
Subscribe to:
Posts (Atom)
-
Mkoa wa Njombe ni moja kati ya mikoa Tanzania, ukiwa umeanzishwa rasmi mwaka 2012. Umepakana na mikoa ya jirani ya Morogoro, Ruvuma, Mbeya...
-
Shujaa wetu: Franz Wesinger-Mhandisi aliyejenga kanisa Katoliki Mbulu Kanisa la Mbulu ndilo kanisa kubwa kuliko yote Tanzania na la ...
-
Isidore Bakanja, ambaye alitoa maisha yake kwa ajili ya imani ya Kikristo, Akiongozwa na maisha rahisi kama layman Katoliki wakati wa mauaj...