Thursday, December 25, 2014

alhamisi 25/12/2014 mosomo ya sherehe ya kuzaliwa bwana noel

Alhamisi, 25 Desemba 2014
Sherehe ya Kuzaliwa Bwana (Noeli)

Isa 52: 7-10;
Zab 97: 1-6;
Ebr 1:1-6;
Yn 1: 1-18

NENO lilinenwa; Mungu asiyefahamika alilifanya lifahamike, furahini!

Leo Kanisa pamoja na viumbe vyote vyajawa na furaha kwani vimefanywa upya na kuwa kiumbe kipya kwa njia ya kuzaliwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo. “Neno” basi na uwe mwanga (Mwa. 1:3), lililoleta uumbaji sasa limeongelewa tena, kupitia kuzaliwa kwa Bwana wetu na Mkombozi wetu. Mwanga (Yn. 1:8), sasa anang’ara katika giza. Mwanga, atoaye mwanga kwa kila mtu amekuja ulimwenguni. Mungu asiyefahamika, sasa amefanywa afahamike, Baba sasa anajidhihirisha mwenyewe, kupitia mwanae wa kiume, Yesu. Neno alifanyika mwili na akakaa kwetu.

Umwilisho au Noeli ni sherehekeo la furaha hii – Mungu wetu anakuwa mwili na anakuja kukaa ndani yetu wanadamu. Tukio hili lilikuwa kubwa sana kiasi cha dunia ya Magharibi kiutamaduni imefanya karne yake katika vipindi viwili vya nyakati kwa mwaka wa kuzaliwa kwake: BC (Kabla ya Kristo) and AD (Anno Domini,kutoka kilatini ni katika Mwaka wa Bwana). Tukio hili liliufanya ulimwengu ufurahi , malaika walifurahi kwa Utukufu kwa Mungu, waliomba kwaajili ya amani duniani kwa watu. Ingawa ukaribisho wa Bwana Yesu haukuwa wa furaha sana ulimwenguni. Mkombozi hakuwa na nafasi ya kuzaliwa, bali katika uhakika, katika moja ya vijiji vidogo Bethlehemu. Hakuwa na tafrija ya ukaribisho, isipokuwa tu kwa baadhi ya wanyama katika hali ya ukimya na baadae wachungaji wachache waliomuabudu Yeye. Mfalme Herode alimchukulia mtoto kuwa kama ni tishio, alitaka mtoto Yesu auwawe. Katika miaka ya mbeleni, mkombozi wetu alikanwa, alivamiwa na kusurubiwa. Na kwa hayo yote aliyoyapokea, mkombozi pekee alirudisha huruma, huruma na upendo. Leo, Yesu amezaliwa kati yetu tena, katika hali yetu ya kumkana na hali ya dhambi; Yeye amezaliwa Bethrehemu ya hali ya ubinafsi, umimi, mateso, vita, unyonyaji, nakadharika. Je, sisi tupo kama wachungaji, waliokwenda kwa Yesu na kuzitoa heshima zao au tupo kama Herode, aliyemchukua Yesu kuwa kama ni tishio la uhuru wetu, katika hangaiko la kutafuta starehe? Je, tunakwenda kufurahi pamoja na wachungaji au kupanga mabaya kama Herode?

Katika milongo miwili iliyopita, dunia yetu imekuwa nzuri sana kwa wanadamu pamoja na uwepo wa kimungu wa Mungu mwenyewe. Ndani yake pia, wengi wametamani kuwa katika giza. Leo Yesu anahitaji azaliwe ndani yetu, awe Neno linenwalo, mwanga unaoondoa giza lote. Je, tupo tayali kujitoa wenyewe kwake Yeye? Je, tupo tayali kuufahamu mwanga huo? Je, tupo tayali kuupokea upendo wake?

Sala: Bwana Yesu, nakuhitaji Wewe uzaliwe ndani yangu leo, Nakuhitaji Wewe unijaze kwa mwanga Wako na kuondoa giza lote ndani yangu, Ninahitaji kunena juu yako katika maneno na maisha yangu. Amina.

"Kwa sababu ya heshima na utume wao, wazazi wakristo wanao wajibu wa pekee wa kuwalea watoto wao katlka sala, wakiwaingiza katlka ugunduzi wa polepole wa siri ya Mungu na mazungumzo ya binafsi naye. "Ni hasa katika familia ya kikristo, ikitajirishwa kwa neema na msaada wa sakramentl ya ndoa, kwamba toka miaka ya awali kabisa watoto budi wafundishwe, kufuatana na imanl ile waliyopewa katika Ubatizo wawe na elimu ya Mungu, kumwabudu na kuwapenda jirani zao"" – Baba Mtakatifu Yohani Paulo II, Wosia wa Kitume Familiaris Consortio (WAJIBU WA FAMILIA YA KIKRISTU KATIKA ULIMWENGU WA KISASA)- 60.

VIWAWABOKO
www.viwawaboko.blogspot.com

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR