Tuesday, April 11, 2017

TAMASHA LA VIJANA DEKANIA YA MT. GASPER

TAMASHA LA VIJANA DEKANIA YA MT. GASPER Vijana wa Dekania ya Mt. Gasper Del Bufallo walikutana Tarehe 26/11/2016, katika Tamasha lao la kufunga Mwaka, Tamasha hilo lilianza kwa Ibada ya Misa Takatifu iliyoongozwa na Padre Mlezi wa Dekania Pd. Dominic Soloma. Baada ya Ibada ilifuata Semina na Michezo Mbali Mbali

BONYEZA HAPA KUDOWNLOAD PICHA ZOTE

Thursday, March 24, 2016

Wednesday, March 23, 2016

KWANINI WAZEE WA ZAMANI WALIISHI MIAKA MINGI: YAJUE MADHARA YA MAFUTA YAKUPIKIA

CHAKULA ni moja ya mahitaji muhimu katika mwili wa mwanadamu, kwa ajili ya kuupatia nguvu, kulinda na kujenga mwili. Kwa kawaida, vyakula vingi anavyokula mwanadamu vinaandaliwa kwa kutumia mafuta ya kupikia, hali inayosababisha wapishi wengi kushindwa kuandaa vyakula kama hawana mafuta ya kupikia.
Mafuta ya kupikia yana faida na madhara kulingana na aina na wingi wa mafuta. Hata hivyo, kwa kawaida, mafuta yasiyokuwa na viwango vya ubora hupatikana kwa bei nafuu, na ndiyo hayo ambayo hupendwa kutumiwa na familia nyingi kutokana na uwezo wa kipato.
Kutokana na hali ngumu ya maisha inayozikabili familia nyingi nchini, wengi wetu hatujali aina ya vyakula tulavyo, wala vyakula tunavyonunua vina viambato gani na kiasi gani. Wengi tunaangalia gharama na upatikanaji wa bidhaa, basi.
Ni mafuta gani bora yanayofaa kupikia chakula?
Ili kuwa makini na afya zetu, ni vizuri kutafuta na kuchagua mafuta ya kupikia kwa umakini na busara zaidi. Kama nilivyodokeza hapo juu na katika machapisho mengine ya FikraPevu kwamba ulaji wa mafuta una faida na hasara zake. Moja ya madhara ya ulaji wa mafuta bila uangalifu, ni kutofanya kazi vizuri kwa ubongo pamoja na kuziba mishipa ya damu.
Katika soko la mafuta ya kupikia nchini, kuna aina nyingi tu za mafuta. Hata hivyo, kisayansi mafuta yote hayo ymegawanyika katika sehemu kuu mbili tu. Mosi, ni mafuta ya kupikia yanayotokana na asili ya wanyama, na pili, ni mafuta yanayotokana na mimea ya asili.
Mafuta yenye asili ya wanyama
Mafuta yenye asili ya wanyama, kwa asili, huwa yameganda katika joto la kawaida. Mafuta haya ni pamoja na anayotokana na nyama iliyonona na nyama ya nundu. Mafuta ya samli, siagi, jibini na maziwa yenye mafuta.
Aina hii ya mafuta ina athari kwa mtumiaji, ikiwa ni pamoja na kupata magonjwa ya moyo, kuwa na uzito uliozidi na unene uliokithiri, huweza kusababisha ugonjwa wa kisukari na kadhalika. Kwa hiyo, ni muhimu kiafya, kila binadamu akajitahidi kupunguza utumiaji wa aina hii ya mafuta yenye asili ya wanyama.
Mafuta yatokanayo na mimea
Mafuta mengi yatokanayo na mimea huwa hayagandi na muda wote yanakuwa katika hali ya kimiminika katika joto la kawaida. Kwa kawaida, mafuta haya haya, tofauti nay ale ya wanyama, yana ‘lehemu.’
Aina ya mafuta aina hii yanayotokana na mimea ya asili, ni pamoja na mafuta ya soya, ufuta, karanga, alizeti, mawese, pamba, nazi, korosho, kweme na mbegu za maboga.
Katika afya ya sayansi, mafuta haya ndiyo bora zaidi kwa kupikia kwa sababu husaidia kuboresha afya ya mwili. Hata hivyo, pamoja na kuwa mafuta bora zaidi, inashauriwa kuyatumia kwa kiasi kidogo.
‘Lehemu’ ni nini na ina madhara gani mwilini?
‘Lehemu’ ni moja ya kiambata kinachopatikana kwenye mafuta ya kupikia, ambacho kitaalamu inajulikana kwa jina la ‘Cholesterol.’ Kiambata hiki hupatikana kwa wingi kwenye mafuta ya kupikia yanayotokana na asili ya wanyama.
Kiambata hiki, pamoja na kusababisha madhara makubwa ya kiafya, lakini kinahitajika mwilini kwa kiasi kidogo. Kwa kawaida kiambata hiki kinatakiwa kiwe chini ya 200mg/dl. Hata hivyo, ni vigumu kwa binadamu kujitambua ni kiasi gani cha kiambata hiki kilichoko mwilini mwake hadi pale atakapoonana na Daktari na kupima.
Moja ya madhara ya kuwa na kiasi kikubwa cha lehemu mwilini, ni kuwa na mkusanyiko wa mafuta katika mishipa ya damu, hali inayoweza kusababisha damu kushindwa kupita kwa urahisi katika mishipa ya mwanadamu.
Hali hiyo ikimpata mwanadamu, huweza kusababisha tatizo la shinikizo kubwa la damu na ugonjwa wa moyo. Hatari nyingine ni mafuta kuziba mishipa midogo ya damu yenye mawasiliano ya moja kwa moja na moyo au ubongo, hali inayoweza kusababisha ugonjwa wa kiharusi pamoja na kifo.
Nini kifanyike ili kujilinda na athari hizo za kiafya zinazosababishwa na lehemu?
Kwanza kabisa punguza matumizi ya nyama, mayai, jibini na maziwa yasiyotolewa mafuta kabla ya kutumiwa. Jiepushe kula maini, moyo, firigisi na figo. Kama mtu anaiishi katika mazingira ambayo nyama nyekundu kama vile ya ng'ombe ndiyo mboga kuu, basi mtu huyo anapaswa kuhakikisha kwamba kiasi cha nyama nyekundi kinacholiwa hakizidi nusu kilo kwa wiki.
Ongeza matumizi ya vyakula vyenye makapi-mlo kwa wingi, kama vile nafaka zisizokobolewa kwa mfano unga wa dona, ulezi, uwele, mtama, vyakula vya jamii ya kunde, mbogamboga na matunda. Kwa kawaida vyakula vyenye makapi-mlo kwa wingi, huwa havina mafuta mengi.
Ni muhimu pia kwa binadamu kujiepusha na ulaji wa mafuta yanayotokana na wanyama, kujiepusha na ulaji wa nyama zilizonona na kuwa na mafuta mengi, kuepuka ulaji wa ngozi ya kuku na siagi pia.
Mazoezi ya mwili angalau dakika 30 kila siku, ni muhimu kwa aina yoyote ya ulaji wa mafuta bila kujali kwamba yana asili ya wanyama au mimea. Inahauriwa mazoezi hayo yawe yale ynayomtoa mtu jasho jingi, kama vile kukimbia kila siku umbali fulani wa kilomita.

CHAD VS TANZANIA LEO ANGALIA

Click here kuangalia live

Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) siku ya kesho Jumatano itakuwa na mtihani mwingine mgumu ugenini dhidi ya Chad katika pambano la mzunguko wa tatu hatua ya makundi kuwania tiketi ya kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika-CHAN 2017.
Chad hoping to stun Tanzania N'DjamenaMichezo miwili ya kwanza kwa kikosi cha Stars haikuwa na matokeo mazuri, chini ya kocha aliyepita M-holland, Marti Nooij, Stars ilichapwa 3-0 na Misri, Alexandria, na mechi iliyofuata ambayo ilikuwa ni ya kwanza kwa kocha mzawa, Charles Boniface Mkwassa ilimalizika kwa suluhu dhidi ya Nigeria katika uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
CHAD NI YA 114 KWA UBORA DUNIANI, YA 22 AFRIKA…
Mshindani wa tatu wa Stars ni Chad, taifa ambalo halijawahi kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika. Wakati, Stars ilifuzu kwa fainali za Afrika mwaka 1980 (miaka 36 iliyopita) Chad ni taifa ambalo linajijenga kwa maana ya hawakushiriki mara kadhaa hatua kama hii ya kufuzu kwa sababu ya kuandaa kizazi kipya.
Nimetazama wastani wa umri wa wachezaji wa Chad, kiukweli wanaonekana kupevuka sana kiumri, sijui kimpira watakuwaje. Stars ilijilinda vizuri dhidi ya Misri kwa dakika 60, lakini kufikia dakika ya 69 timu ilikuwa imechapwa magoli 3-0, dhidi ya Nigeria, Mkwassa alijitahidi kuifanya timu ishambulie na kujilinda vizuri.
Achilia mbali bao la kujifunga kwa timu pinzani, bado hakuna mchezaji ye yote yule wa Stars aliyefanikiwa kufunga goli katika michuano hiyo hadi sasa . Lalini kuna mengi yamebadilika katika timu ya Mkwassa kuelekea mchezo wa Jumatano hii.
Mbwana Samatta anashikilia tuzo ya ufungaji bora wa klabu barani Afrika, pia ndiye mshindi wa tuzo nyingine binafsi ya mchezaji bora wa mwaka uliopita Afrika, akiwa tayari amefunga magoli mawili katika michezo minne ya ligi kuu ya Ubelgiji akiwa na klabu ya Genk aliyojiunga nayo mapema mwaka huu akitoka kushinda ubingwa wa Afrika upande wa klabu akiwa na TP Mazembe ya DR Congo.
Samatta anataraji kwa mara nyingine kuongoza safu ya mashambulizi ya Stars, lakini safari hii kwa mara ya kwanza akiwa na beji ya unahodha katika bega lake la kushoto. Wachezaji wengi wa Chad wana umri kati ya miaka 27 hadi 32, bila shaka watakuwa na uzoefu wa kucheza nyumbani katika michezo ya kimataifa.
Kama ilivyokuwa kwa Misri 3-0 Stars, Chad pia waliibana sana Nigeria katika mchezo wao wa kwanza, lakini walijikuta wakipoteza mechi hiyo ya ugenini wakati muda ‘umekwenda,’ walifungwa 2-0. Mechi yao ya pili walicheza nyumbani na Misri, walichapwa 5-1 matokeo ambayo yamewafanya kuwa mkiani mwa kundi wakiwa bila pointi yoyote.
Uwezo wao kimbinu bado uko chini ndiyo maana licha ya kuonekana kujilinda vizuri wakilazimishwa wanakubali kufungwa. Hata Stars hucheza vizuri lakini timu zote zinakutana zikiwa na viwango vya kukaribiana, umakini mdogo, makosa yasiyo na ulazima katika ngome kutaiangusha timu yeyote katika mchezo huu kwa kuwa Chad wana washambuliaji wazoefu wanaocheza nje ya nchi yao.
Nadjim Haroun ndiye kiungo mchezesha timu wa Chad, anacheza timu ya daraja la chini Ubelgiji, huyu ndiye aliyefunga goli lao pekee katika michuano hiyo hadi sasa.
Jinsi ya kupanga mashambulizi na kupiga pasi za mwisho bado ni tatizo kwa Taifa Stars lakini bado kuna nafasi ya washambuliaji wetu kufunga walau magoli mawili katika mchezo huu, ni namna watakavyochezeshwa na kupewa mipira ya mwisho na viungo kutaangaza ubora wao.
Thomas Ulimwengu na mwendo wake wa kasi na nguvu akitokea upande wowote ule, Samatta (binafsi ningependa aanze na nahodha msaidizi, John Bocco) wanaweza kuwafanya walinzi wote wa Chad kuwa na hofu.
Katika ngome, Chad hawana mchezaji wa kulipwa, wengi wanacheza ligi yao ya ndani kwa maana hiyo kwa namna yeyote watapata wakati mgumu kuwazima washambuliaji wetu watatu wafungaji (Tom, Samatta na Bocco)
Tishio kubwa kwa Stars na nafikiri kocha Mkwassa atapaswa kuchanga vizuri karata zake ni katika safu ya kiungo. Marius Mbalam kiungo mchezesha timu ya Belfort ya France National, Azrack Mahamat anayecheza Platanias ya ligi kuu ya Ugiriki, Sanaa Altama wa Petrolut ya ligi kuu ya Romania na Sylvain Idangar wa AS Lyon ya Ufaransa ni viungo muhimili wa mbinu za kocha Mcameroon, Rigoberb Song.
Song, mchezaji wa zamani wa Cameroon na timu nyingi mashuhuri barani Ulaya anaweza kuwapanga viungo watatu kati ya wanne hao. Azrack ana miaka 27, Marius ana miaka 28, Idangar ana miaka 32 na kijana pekee ni Sanaa mwenye miaka 25.
Umri wao umepevuka lakini bado kuna nafasi ya vipaji vya ligi kuu Bara kuchanua katika idara hii kama tu wachezaji wetu vijana kama Himid Mao, Jonas Mkude, Deus Kaseke, Salum Abubakary na wengineo watacheza kwa ari ya kusaka ushindi kama ilivyokuwa dhidi ya Nigeria na Algeria (kufuzu WC) jijini, Dar fs Salaam.
Kukaba, kucheza faulo za kitaalamu, kumiliki mpira, pasi timilifu, kutengeneza nafasi na kupiga pasi za mwisho kutaisaidia sana safu ya mashambulizi, na bila shaka timu itafunga magoli ya kutosha kama viungo watatimiza mambo hayo niliyoyataja.
Ngome ya Stars mara nyingi imekuwa ikiiangusha timu, rejea sare ya ajabu dhidi ya Algeria, Novemba mwaka jana, washambuliaji walifunga magoli mawili maridadi sana lakini safu ya ulinzi ikaruhusu magoli mawili ya kuchukiza sana.
Wengi walichukizwa na mabadiliko ya Mkwassa, kumtoa Mudathir Yahya na kumuingiza Said Ndemla wakati timu ikiongoza 2-0, lakini Mwinyi Hajji alihusika katika goli la kwanza la Algeria kwa kupiga pasi ‘mkaa’, na safu yote ya ulinzi ilihusika katika goli la kusawazisha la Algeria kutokana na umakini wao mdogo, na kujipanga vibaya.
Magoli 8 ya Shomari Kapombe katika VPL msimu huu akicheza katika beki 2, kiwango cha juu cha kupandisha mashambulizi kutoka kwa Mwinyi katika beki 3, uwezo wa kujipanga wa David Mwantika katika beki ya kati, na ukabaji wa nguvu wa Kelvin Yondani katika beki 4, vyote havitakuwa na maana kama timu itafungwa tena magoli ya kizembe.
Nahodha wa Chad, Ezechiel N’Douassel, 27, anayechezea klabu ya Sfaxien ya Tunisia, kijana Rodrigue Ninga, 22 anayekipiga Montpellier ya Ufaransa ni washambuliaji ambao wataitumia nafasi yoyote watakayopewa na walinzi wa Stars.
Washambuliaji hawa wanacheza vizuri mipira ya juu, pia ni wamaliziaji wazuri hivyo kuanzia kwa golikipa, Ally Mustapha hadi kwa walinzi wake watapaswa kucheza na kuondosha vizuri mipira ya juu itakayoelekezwa golini kwao.
Song alikuwa mlinzi mahiri wa kati, wakati Mkwassa alifahamika kama ‘master’ wakati wake wa uchezaji kama kiungo wa dimba la kati. Chad hushambulia ikicheza nyumbani, lakini Stars ni timu isiyo na utamaduni wa kujilinda kokote inapocheza.
Kuwa na Samatta, Tom na Bocco aliye katika kiwango, kunaweza kumkumbusha Song mambo mengi wakati wa uchezaji wake na hivyo kuingiza timu yake katika umbo la kujilinda. Mkwassa angependa washambuliaji wake wachezeshwe kama yeye alivyokuwa akiwachezesha washambuliaji nyakati zake za uchezaji ili kumshinda Song.
Lakini bado pasi za mwisho hakuna katika timu, pasi za namna ile ya umbali mrefu ambayo ilipigwa na kiungo Henry Joseph kwenda kwa mshambulizi Danny Mrwanda, ambaye alifunga mbele ya Song wakati Stars ilipopata goli la kuongoza dhidi ya Cameroon (ugenini, 2009-Kufuzu WC 2010 na CHAN 2010)
Kila la heri Taifa Stars, ushindi una maana kubwa sana kwa kuwa Misri watacheza mara mbili na Nigeria wiki hii, hivyo pointi 6 dhidi ya Chad zinaweza kuifanya Stars kuwa juu ya timu mojawapo kati ya Misri na Nigeria kabla ya kurejeana nazo.














Belgians hunt Islamic State suspect after blasts kill 30 airport


Belgian police are hunting an Islamic State suspect seen with two supposed suicide bombers shortly before they struck Brussels Airport in the first of two attacks that also hit the city's metro, killing at least 30 and wounding over 200.
The blasts on Tuesday claimed by the Syrian-based militants four days after the arrest in Brussels of a prime suspect in November's Paris attacks, sent shockwaves across Europe and around the world, with authorities racing to review security at airports and transit systems, and drawing an outpouring of solidarity.
"We can and we will defeat those who threaten the safety and security of people all around the world," said U.S. President Barack Obama. Donald Trump, the front-runner for the Republican nomination to succeed Obama in November's election, suggested suspects could be tortured to avert such attacks.
Brussels police mounted an operation in the north of the city, turning up another bomb, an Islamic State flag and bomb-making chemicals in an apartment in the borough of Schaerbeek.
Local media said authorities had followed a tip from a taxi driver who believed he may have driven the bombers to the airport.
Investigators said they were focusing on a man in a hat who was caught on CCTV pushing a laden baggage trolley at the airport with two others they believed were the bombers. An unused explosive device was later found at the airport and a man was seen running away from the terminal after the explosions.
Security experts believed the blasts, which killed about 20 on a metro train running through the area that houses European Union institutions, were probably in preparation before Friday's arrest of locally based French national Salah Abdeslam, 26, whom prosecutors accuse of a key role in the Nov. 13 Paris attacks.
He was caught and has been speaking to investigators after a shootout at an apartment in the south of the city a week ago, after which another Islamic State flag and explosives were found. It was unclear whether he had knowledge of the new attack or whether accomplices may have feared police were closing in.
Islamic State said in a statement that "caliphate soldiers, strapped with suicide vests and carrying explosive devices and machineguns" struck Zaventem airport and Maelbeek metro station.
It was not clear, however, that the attackers used vests. The suspects were photographed pushing bags on trolleys, and witnesses said many of the airport dead and wounded were hit mostly in the legs, possibly indicating blasts at floor level.
MAN IN THE HAT
Officials said the final death tolls remained uncertain from the carnage in the morning rush hour, around 8 a.m. (03:00 a.m. EDT) at the airport and shortly after 9 a.m. on the metro.
"A photograph of three male suspects was taken at Zaventem. Two of them seem to have committed suicide attacks. The third, wearing a light-colored jacket and a hat, is actively being sought," prosecutor Frederic Van Leeuw told a news conference.
The two men in dark clothes wore gloves on their left hands only. One security expert speculated they might have concealed detonators. The man in the hat was not wearing

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR