Showing posts with label Masomo ya 29 JUNI JUMAPILI YA 14 YA MWAKA "A" 2014 (KIJANI). Show all posts
Showing posts with label Masomo ya 29 JUNI JUMAPILI YA 14 YA MWAKA "A" 2014 (KIJANI). Show all posts

Thursday, June 26, 2014

MASOMO YA 29 JUNI JUMAPILI YA 14 YA MWAKA "A" 2014 (KIJANI)

29
   JUNI 
 JUMAPILI YA 14 YA MWAKA "A"
2014 (KIJANI)


RATIBA ZA IBADA
KIGANGO CHA BOKO.
IBADA YA MISA YA KWANZA 12:15 – 1:45 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 2:00 – 3:50 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA TATU SAA 4:00-5:20 ASUBUHI
KIGANGO CHA MBWENI.
IBADA YA MISA YA KWANZA 1:15 – 2:55 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 3:00 – 4:50 ASUBUHI
KIGANGO CHA MT. RAFAEL.
IBADA YA MISA YA KWANZA 1:00 – 2:55 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 3:00 – 4:50 ASUBUHI
KIGANGO CHA ANTHONY WA PADUA – MBWENI MPIJI.
IBADA YA MISA NI 3:00 – 5:00ASUBUHI

SOMO 1:Zek.9:9-10


Furahi sana, Ee binti Sayuni; Piga kelele, Ee binti Yerusalemu; Tazama, mfalme wako anakuja kwako; Ni mwenye haki, naye ana wokuvu; ni mnyenyekevu, amepanda Punda; naam, mwana-punda, mtoto wa Punda. Na gari la vita nitaliondoa liwe mbali na Efraimu, na Farasi awe mbali na Yerusalemu, na upinde wa vita utaondolewa mbali; naye atawahubiri mataifa yote habari za amani; na mamlaka yake yatakuwa toka bahari hata bahari, na toka mto hata mwisho wa dunia.



SOMO 2:1Rum. 8:9, 11-13

Roho wa Mungu anakaa ndani yetu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na roho wa Kristo, huyo si wake. Lakini ikiwa roho wake yeye aliyemfufua Yesu katika wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Kristo Yesu katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, kwa roho wake anayekaa ndani yenu. Basi, kama ni hivyo, ndugu, tu wadeni, si wa mwili tuishi kwa kufuata mambo ya mwili; kwa maana kama mkiishi kwa kufuata mambo ya mwili, mwataka kufa; bali kama mkiyafisha matendo ya mwili kwa roho, mtaishi.



INJILI: Mt.11:25-30

Wakati ule Yesu alijibu, akasema, Nashukuru, Baba, Bwana wa mbingu na Nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako. Akasema, nimekabidhiwa vyote na Baba yangu; wala hakuna amjuae mwana, ila Baba; wala hakuna amjuae Baba, ila mwana, na ye yote ambaye mwana apenda kumfunulia. Nyoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kuelemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni laini; na mzigo wangu ni mwepesi.



 MATANGAZO

mara baada ya misa ya pili saa 4:00 asubuhi, Parokiani Boko, mazoezi ya washiriki wa ziara ya taendelea;

Jumanne tarehe 1/7/2014 tunatarajia kuanza safari ya kuelekea Dareda, na tutainjilisha hapo kwa siku nne na tarehe 5/7. tutaelekea parokia ya BM-mpalizwa mbinguni Sanu ....tarehe 6/7 tutaenda parokia ya Daudi na endabashi na tarehe 7/7 tutaenda Mbuga ya Wanyama ya Ngorongoro,,,,,Sisi ni Askari kamili wa Yesu tuzidi kuombeana tuweze kwenda kumtangaza huyu Yesu ambaye ndiye Njia ya Uzima na Ukweli katika Maisha yetu sisi Vijana.......Mapen

Tunawatikia Dominika njema, Amani ya Bwana Iwe nasi.........Mapendo sana,,,,,,,

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR