Tuesday, June 24, 2014

Mtakatifu Gaspar mtume hodari wa Damu Azizi ya Yesu, rafiki na mtetezi wa wanyonge! (precios bloods fathers in Tanzania)



Yafuatayo ni mahubiri yaliyotolewa na Padre Reginald Mrosso, Mkuu wa Shirika la Wamissionari wa Damu Azizi ya Yesu, Vikarieti ya Tanzania katika Maadhimisho ya Siku kuu ya Mtakatifu Gaspar del Bufalo, Mwanzilishi wa Shirika la Wamissionari wa Damu Azizi ya Yesu inayoadhimishwa kila mwaka ifikapo tarehe 21 Oktoba.

Katika Katekisimu Mpya ya Kanisa Katoliki tunasoma hivi “Mungu aliye mkamilifu bila mpaka na mwenye heri ndani yake mwenyewe, katika mpango wa wema wake tu, alimwumba mtu kwa hiari yake apate kumshirikisha uzima wake wenye heri. Kwa sababu hiyo, wakati wote, na mahali pote yupo karibu na mwanadamu. Humwita mwanadamu na kumsaidia ili amtafute, amjue, na ampende kwa nguvu zake zote. Anawakusanya watu wote, ambao dhambi iliwatawanya, katika umoja wa familia yake, Kanisa. Ili apate kukamilisha hayo, wakati ulipotimia alimpeleka Mwanawe kama Mwokozi na Mkombozi. Ndani ya Mwanawe na kwa njia yake anawaita watu wafanyike kuwa wana wake katika Roho Mtakatifu, na hivyo wawe warithi wa uzima wake wenye heri”.

Mtume Petro – 1Pet. 1: 13-21 – anatuita tuiishi dhamiri hii. Sisi tunayo matumaini yanayotuhimiza tuwe watakatifu. Sisi tumekombolewa si kwa fedha au dhahabu, bali kwa DAMU YA KRISTO. Hivyo tuishi kama watakatifu kwa mfano wa Mungu aliyetuita katika imani.

Hapa tunatambua kuwa Mungu amekuja kati yetu na amekaa nasi na kila mmoja wetu anaalikwa kuishi na kuutangaza uzima huu mpya. Mtakatifu Gaspari del Bufalo alitambua vizuri kabisa mpango huu wa Mungu kwa ajili ya wokovu wa mwanadamu. Aliweka katika matendo ufahamu huo akitoa ushuhuda na hata kumwaga damu yake kama Kristo kwa ajili ya ndugu zake.

Leo tunakaa hapa pamoja kusali na kutafakari juu ya ukuu huu Mungu na upendo wake kwetu lakini zaidi pia tunatafakarishwa juu ya wajibu wetu mbele ya Mungu na watu wake.

Mtakatifu Gaspari alipoanzisha Shirika alichagua tasaufi ya Damu takatifu iwe karamu yetu ikiongozwa na vipengele vikuu vine – agano, kikombe, msalaba na upatanisho. Katika adhimisho la Jubilee kuu ya Mwaka 2015 Shirika limechagua maandalizi ya adhimisho hilo kuu kwa kufanya tafakari ya kina juu ya uwepo wake na ushuhuda wake hapa duniani. Maadhimisho kuelekea Jubilei hii kuu yalianza rasmi mwaka 2013 kuelekekea 2015 kwenye kilele – mambo ambayo tunayafanya:

Mwaka wa kwanza – 2012-2013 -Kuangalia historia yetu tulikotoka na uaminifu kwa karama yake.

Mwaka wa pili – 2013-2014 - Kuangalia wakati wetu wa sasa – ni kwa jinsi gani tunaishi karama ya upatanisho katika dunia ya leo.

Mwaka wa tatu – 2014-2015 - Kuangalia utume wetu – ni kwa namna gani tunaweza kutoa jibu kwenye kilio cha damu.


Leo tunakutana katika adhimisho la sadaka takatifu ya misa tukiwa pamoja na kama taifa la Mungu linaloamini uwepo wake Mungu Baba mwenyezi. Na dhamira yetu kuu mwaka huu ni upatanisho. Tunajiuliza je upatanisho maana yake nini? Upatanisho ni tendo la uponyaji. Ni tendo linalorudisha mahusiano kati yetu na Mungu na kati yetu.

Uwepo wa Kristo umeleta wokovu wa milele. Neno wokovu linaeleza dhana ya kuwekwa huru. Kwa kutupatanisha naye, tumepewa wajibu mpya kumtumikia Mungu mzima.

Zaburi ya 85 inatukumbusha tena wajibu wetu wa kutafuta upatanisho na Mungu na watu wake. Utuponye tena Ee Mungu, mwokozi wetu…. Wokovu wake ni karibu na wenye kumcha, utukufu wake utakaa katika nchi yetu, wema na uaminifu zitakutana, haki na amani zitabusiana. Uaminifu utachipuka katika nchi, na haki itachungulia kutoka mbinguni. Naye Bwana atatoa yaliyo mema, na nchi yetu itatao mazao, haki itatangulia mbele ya Bwana, wokovu utafuata nyayo zake.

Kama walivyofanya wana wa Israeli katika sala hii, wanamkubusha Mungu fadhila zake kwao na zikijumuisha msamaha wa hatia zao. Wanatambua makosa yao na wanaomba Mungu awajenge upya tena. Hapa baada ya kutoka utumwani wanatambua ubaya wa dhambi na balaa zake na wanataka kujijenga upya na kuanza upya katika yote. Wajibu wetu leo ni kujenga na kuendeleza huo ufalme mpya wa Mungu ulioletwa kwa njia ya Kristo na kanisa lake.


Baba Mtakatifu mwenye heri Yohani Paulo II katika mojawapo ya mafundisho yake anaeleza kuwa - ukombozi wa mwanadamu umefanyika kwa Kristo kumwaga damu yake. Kwake yeye sisi tumefanywa wana – Efe. 1:3…ametuchagua kabla ya kuumbwa ulimwengu ili tuwe wake. Na kwa njia yake tumepokea neema ya kuwa wana na kuwa watakatifu. Hii zawadi ya neema imeletwa kwetu kwa njia ya Kristo.

Na kwa namna hii Mungu Baba amefanya mageuzi makubwa kwetu – ukombozi toka utumwa wa dhambi, ukombozi kwa njia ya damu yake, msamaha wa dhamhi kwa neema yake na kuwa wana katika Mwanaye. Kifo cha Kristo msalabani, tendo kuu kabisa la upendo na umoja, humwaga kwetu mwanga mkuu na kutujalia busara ya kimungu.

Katika lugha ya kibiblia – akili au ufahamu huelezwa au kuonekana katika pendo na kwa maana hiyo pendo hutuingiza katika fumbo la mapenzi yake Mungu ambapo lengo lake ni wokovu – mwisho wake ukiwa ni kuunganisha yote mbinguni na duniani chini ya Kristo. Anahitimisha akisema au tukialikwa au tukimwomba Mungu atujalie neema ya kuona, kutafuta na kutafakari mema ya mbinguni na si ya hapa duniani.

Narudia tena, sisi ambao tumepatanishwa na Damu ya Kristo tumepewa wajibu mpya.

Mtume Paulo katika - 2Kor. 5:17-21 – basi mtu akiwa katika Yesu Kristo ni kiumbe kipya. Ya kale yamepita, mapya yamefika. Hayo yote yanatoka kwa Mungu. Yeye ametupatanisha naye kwa ujumbe wa Kristo, akatukabidhi sisi kazi ya usuluhishaji. Yaani, Mungu ameipatanisha dunia naye katika Kristo, kusudi asiwahesabie watu tena makosa yao. Akaliweka neno la upatanisho ndani yetu. Basi, tumekuwa wajumbe mahali pa Kristo, kwa maana ni Mungu anayeonya kwa huduma yetu. Na ombi tunalotoa kwa jina la Kristo ndilo mpatanishwe na Mungu. Yeye amemfanya yule asiyejua dhambi kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili na sisi tuwe uadilifu wa Mungu katika yeye.

Sisi leo kama Mtakatifu Gaspari tunaalikwa kutafakari vyema nguvu ya upendo wa Kristo aliyemwaga damu yake na akatupatanisha na Mungu. Tendo hili la Mungu ni pendo takatifu na hivyo basi sisi tunaomwamini Mungu tuna lazima ya kuingia katika falsafa hii ya wokovu. Huu ni utume wa Kanisa na kila mkristo. Sisi tumesamehewa makosa yetu kwanza na Mungu. Ni wajibu, ni lazima, si hiari. Je mimi, wewe, sisi ni sababu ya upatanisho?


Ili upatanisho utokee ni lazima mambo manne yawepo; ukweli, huruma, haki na amani. Na tujiulize sote tulioko hapa leo je tunazo sifa hizo katika maisha yetu.

Kristo kwa kumwaga damu yake ametukomboa toka mauti na kutupatanisha tena na Mungu Baba. Mara nyingi tunapofikiria kuhusu sakramenti ya upatanisho tunatingwa. Huwa tunatatizwa zaidi na ubaya au ukubwa dhambi zetu. Kwa hiyo tunakata tamaa, Kwa hakika tafakari yetu ingetakiwa itambue kwanza huruma ya Mungu ambayo ni kuu kuliko dhambi zetu.

Kama tutafikiria zaidi juu ya dhambi zetu na kuogopeshwa sana kama vile hutujapatanishwa naye Kristo, basi hatuna cho chote cha kuadhimisha, au cha kusherehekea au kinachotuwajibisha. Upatanisho hautatafutwa wala kupatikana. Tafakari yetu kuu na ya kwanza ni juu ya huruma ya Mungu isiyo na mwisho, isiyopunguka, na ikiwa hivyo basi tuna kila sababu ya kufurahi na kushangilia. Tufikirie kwa mfano Injili ya Luka sura 15: kondoo aliyepotea, shilingi iliyopotea, mwana mpotevu.

Fundisho hilo ni juu ya huruma kuu ya Mungu. Hata kama tumekata tama, Mungu husamehe, Mungu hufurahi na hukamilika katika kusamehe. Kristo amekufa ili kudhihirisha pendo hilo kuu la Mungu kwetu. Huo ndio upendo kamili.

Sisi tumekombolewa kwa Damu yake Kristo. Sisi tuliokuwa na dhambi tumekombolewa. Sisi ambao hatukustahili tena upendo wake Mungu, tumetakaswa kwa neema yake. Haijalishi wingi na ukubwa wa dhambi zetu, huruma ya Mungu ni kuu zaidi. Mungu ametupatanisha naye. Hiyo ndiyo furaha yetu. Somo la Injili latukumbusha uwepo wa majaribu lakini pia ipo nguvu ya ushindi kama tukibaki pamoja na Kristo. – katika somo la Injili sala ya Yesu kuhusiana na majaribu, wafuasi wanaahidi kushiriki kikombe cha mateso. Lakini baadaye unapatikana wokovu.

wajue wamissionari wa Shirika la Damu Takatifu ya Yesu(Precious Bloods Fathers)

It was on August 15, 1815 that Saint Gaspar began the Missionaries of the Precious Blood at the abbey of San Felice in Giano, Italy.  Since that beginning, thousands of Missionaries have been inspired by the zeal of St Gaspar and have continued the apostolic work that he began.  It is in recognition of our foundation and in anticipation of the celebration of our bicentennial anniversary in 2015, that the Congregation has begun a three year observance of our founding. 

ANGALIA KOMBE LA DUNIA HAPA (WATCHING WORLD CUP LIVE STREAM LIVE HERE ALL GAMES)

BONYEZA HAPA KUANGALIA
CLICK HERE TO WATCH
MECHI KALI YA LEO IVORY COST VS BLEGIUM

Majambazi wamua Sister wa Parokia ya Makoka

MTAWA AUAWA DAR ES SALAAM

Mtawa mmoja wa kanisa katoliki aliyefahamika kwa jina moja la sister Kapuli ameuwawa kwa kupigwa risasi kichwani na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi katika eneo la River side Ubungo jijini Dar es Salaam na kutoweka na pochi ya sister huyo inayodaiwa kuwa na fedha ambazo kiasi chake hakikufahmika mara moja.
Sr Kapuli wa parokea ya Makoka jijini Dar es Salaam ameuwawa kwa kupigwa risasi kichwani na watu watatu wanaodaiwa kuwa ni majambazi baada ya kufuatiliwa nyendo zao wakitokea katika benki ya CRDB ambayo tawi lake halikufahamika mara moja wakati akimsubiri Sr Mwenzie aliyeshuka katika gari walilokuwa wamepanda lenye namba za usajili T 213 CJZ Toyota VX kwa ajili ya kwenda kuulizia bidhaa fulani dukani katika eneo hilo la Riverside Ubungo jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa waendesha bajaji bw godfrey severine ambaye amenusurkakatika tukio hilo bada ya bajaji yake kupigwa risasi kadhaa amesema watu hao walifyatua risasi kadhaa zilizosababisha taharuki kwa wananchi ambao walikuwa wakikimbia hovyo na hivyo kupata upenyo wa kutoweka katika eneo hilo.

MWAKA WA FAMILIA: Barua ya Papa Francisko kwa ajili ya Familia




  Baba Mtakatifu Francisko kama sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya Sinodi Maalum ya Maaskofu kwa ajili ya Familia itakayoadhimishwa Mwezi Oktoba 2014 hapa mjini Vatican, kwa kuongozwa na kauli mbiu "Changamoto za kichungaji kuhusu familia mintarafu Uinjilishaji" ameandika barua kwa familia zote duniani ili kukazia dhamana ya Kanisa kuendelea kutangaza Injili kwa kukabiliana kinaga ubaga na changamoto mpya zinazohusu familia.

Baba Mtakatifu anasema, maandalizi haya yanawahusu Watu wote wa Mungu kwa kuhakikisha kwamba, wanashiriki kikamilifu kwa kutoa mawazo pamoja na kusindikiza mchakato mzima kwa njia ya sala, jambo muhimu sana kutoka kwa familia zote. Sinodi hii ni maalum kwa ajili ya: wito na utume wa Kanisa na Jamii; matatizo yanayowakabili wanandoa; maisha ya kifamilia, elimu na malezi kwa watoto; dhamana na utume wa familia katika maisha ya Kanisa.

Baba Mtakatifu anazialika familia kusali na kumwomba Roho Mtakatifu ili aweze kuwaangazia Mababa wa Sinodi katika kutekeleza wajibu wao huu nyeti. Sinodi hii maalum, itafuatiwa tena na Sinodi ya kawaida ya Maaskofu itakayojadili kuhusu tema ya familia mwaka 2015 sanjari na Maadhimisho ya Siku ya Familia Kimataifa itakayofanyika mwezi septemba, mjini Philadelphia, nchini Marekani.

Baba Mtakatifu anawaalika wanafamilia pamoja na watu wote wenye mapenzi mema kusali kwa ajili ya kufanikisha matukio haya makuu ndani ya Kanisa, ili liweze kung'amua na kupata mikakati itakayosaidia familia ili kukabiliana na changamoto kadiri ya mwanga na nguvu ya Kiinjili.

Baba Mtakatifu Francisko anasema, ameitunga barua hii wakati Mama Kanisa alipokuwa anaadhimisha Siku kuu ya kutolewa Bwana Hekaluni. Ni tukio ambalo liliwakutanisha Mzee Simeoni na Anna kwa nguvu ya Roho Mtakatifu wakamtambua Yesu kuwa ni Masiha. Mzee Simeoni akamshukuru Mungu kwa kuwa ameuona wokovu na Anna kwa upande wake akasimulia matendo makuu ya Mungu licha ya uzee wake.

Inafurahisha kuona kwamba, wazee wawili na vijana wawili wanakutanishwa na Yesu. Hii inaonesha kwamba, Yesu ana uwezo wa kukutanisha na kuunganisha vizazi, kwani Yeye ni chemchemi ya upendo inayovuka ubinafsi, upweke na masikitiko. Baba Mtakatifu anasema, familia katika hija ya maisha yao wanashirikishana na kumegeana mambo mengi mema: chakula na mapumziko; kazi za nyumbani, starehe, sala, safari na hija ya maisha ya kiroho pamoja na matendo ya huruma.

Pale panapokosekana upendo, hapo kutakosekana furaha na kwamba, upendo wa kweli unabubujika kutoka kwa Kristo kwa njia ya Neno lake ambalo ni mwanga katika mapito ya waamini; anawapatia Mkate wa maisha ya uzima wa milele, unaowasaidia waamini kupambana na changamoto za maisha ya kila siku.


Kardinali Pengo aweka jiwe la msingi la Chuo Kikuu MUCO Bagamoyo!

Kanisa Katoliki nchini Tanzania linaendelea kuwekeza kikamilifu katika sekta ya elimu ili kuwasaidia watanzania kuwa na majiundo kamili ili kukabiliana barabara na changamoto za maisha, ili hatimaye, Tanzania iweze kuwa ni mahali pazuri zaidi pa kuishi.

Shirika la Roho Mtakatifu ambalo kwa miaka mingi limewekeza na kuona mafanikio makubwa katika sekta ya elimu nchini Tanzania, sasa limeanza kujielekeza katika kuanzisha Kitivo cha Sayansi kitakachokuwa chini ya Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augostino cha Tanzania, SAUT. Kitivo hiki kitajulikana kama “Marian University College”, kwa kifupi MUCO, ambacho kinajengwa kwenye mji mkongwe wa Bagamoyo, Mkoani Pwani, nchini Tanzania.

Hivi karibuni, Kardinali Polycarp Pengo, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Dar es Salaam ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa Chuo kikuu cha MUCO na kwamba, mwezi Septemba, 2014 kitaanza kuandikisha wanafunzi, wakati huo huo ujenzi wa majengo mengine ukiendelea kukamilishwa hatua kwa hatua. Katika hafla ya kuweka jiwe la msingi, Kardinali Pengo amesema, nchi ambayo haina wataalam wa sayansi, kwa hakika itachechemea katika ushindani wa maendeleo na mataifa mengine. Umefika wakati kwa watanzania kujiekeza zaidi katika masuala ya kisayansi ili kupata maendeleo endelevu yanayogusa mahitaji msingi ya binadamu: kiroho na kimwili.

Akizungumza katika tukio hili Padre Florentin Mallya, Makamu mkuu wa Shirika la Roho Mtakatifu Afrika Mashariki amesema, MUCO itaendelea kushirikiana na SAUT, hadi pale mchakato wa kukiwezesha Chuo kikuu cha MUCO kujitegemea na kuwa Chuo kikuu kamili. Kuanzishwa kwa MUCO ni kujibu kwa dhati changamoto inayotolewa na Serikali ya Tanzania kwa sekta binafsi kusaidia mchakato wa kukuza na kuendeleza sekta ya elimu hususan katika mchepuo wa sayansi, ili kujibu mahitaji makubwa yanayoendelea kujitokeza ndani na nje ya Tanzania katika masuala ya elimu.

Huu ni mwendelezo wa huduma ya elimu inayotolewa na Shirika hili katika shule zake za awali na sekondari ambazo kwa miaka mingi zimeendelea kupeta nchini Tanzania kutokana na wanafunzi wanaohitimu katika shule hizi kuwa na kiwango kikubwa cha ufaulu kwenye mitihani. Wazazi waliokuwa wanahaha kuwatafutia watoto wao mahali pazuri zaidi pa kusoma, sasa MUCO itakuwa ni jibu lao makini.

Ni kutokana na changamoto zote hizi, Shirika la Roho Mtakatifu liliomba ushirikiano na Serikali ya Tanzania ili kutekeleza azma hii kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya watanzania tangu shule za msingi hadi chuo kikuu. Shirika linapania kuendelea kutoa kiwango bora cha elimu kwa kutambua kwamba, hii ni sehemu ya Uinjilishaji wa kina unaogusa mahitaji ya mtu mzima: kiroho na kimwili. Shirika linaiomba Serikali ya Tanzania pamoja na wazazi kuendelea kuonesha mshikamano katika kufanikisha malengo ya maboresho ya elimu nchini Tanzania.

Papa: anayehukumu wengine ni mnafiki, na hujiweka katika katika nafasi ya Mungu

Baba Mtakatifu Francisko ameonya dhidi ya tabia ya kupenda kuhukumu wengine bila kutafakari hali zetu wenyewe. Kupenda kujiona sisi tu safi na yule ni mdhambi. Lakini tukumbuke kipimo kilekile tunacho tumia kuhukumu wengine, ni hichohicho kitakacho tumika kutuhukumu... Anayehukumu ndugu yake, naye atahukumiwa kwa njia hiyo hiyo. Mungu ndiye pekee "hakimu". Na mshutumiwa anaweza daima hutetewa na Yesu. Yesu, Wakili Mkuu wa Kwanza, na Wakili wa pili ni Roho Mtakatifu. Papa Francisko amesema katika hotuba yake ya wakati wa Ibada ya Misa, asubuhi Jumatatu , katika Kanisa dogo la Mtakatifu Martha, ndani ya Vatican.

Papa Francisko ameonya dhidi ya kuwa watu wa kupenda kuhukumu wengine katika nafasi mbalimbali, kimaisha,au katika uwajibikaji au mamlaka akieleza kwamba jambo kuhukumu ni hatari kwa sababu licha ya kuuumiza wengine, pia, humgeukia mwenyewe na kuishia kuwa mwathirika wa ukosefu wa huruma kwa wengine. Hiki ndicho hutokea katika kuwahukumu wengine.
Papa Francisko alitoa onyo hili, mara baada ya kusoma kifungu cha Injili kuhusu kibanzi na boriti iliyoko katika jicho, akibainisha kwamba , ni wazi inaonyesha mtu anayependa kuhukumu wenzake kuwa anafanya makosa , na huonyesha udhaifu wa mtu wa kushindwa, maana binadamu hana haki ya kumhukumu mtu mwingine kiroho, hakimu ni Mungu peke yake . Kuhukumu wengine ni "unafiki", kama Yesu alivyowaambia kwa mara kadhaa walimu wa sheria, wakati wa matukio kadhaa kwa wakati ule. Na pia ni kwa sababu Papa alieleza, binadamu hutoa hukumu yake harakaharaka, wakati hukumu ya Mungu huchukua muda.


Na hivyo , kutokana na hili , kuhukumu wengine ni makosa , kwa maneno mepesi ni kwa sababu ni kuchukua nafasi isiyokuwa yako. Na si tu ni makosa lakini pia ni kumchanganya mtu. Ni kupagawa na nia kali za kutaka kujitakatifusha, kuonekana kama safi na wengine ni wakosaji , nia zinazowasha moto wa ndani ambazo haziachi nafasi ya utulivu, wa kujitafakari wenyewe. Lakini tunaambiwa kwanza toa boriti katika jicho laki ndipo utoe kibazi kilicho ndani ya ndugu yako.

Homilia ya Papa imesisitiza , mwenye uwezo wa kutoa hukumu ni Mungu peke, na kuongeza, kile kinacho onyesha tabia ya kumtegemea Yesu,ni mfano wake wa kuto hukumu wengne.
Yesu mbele ya Baba, kamwe hakuwatuhumu wengine.Kinyume aliwatetea! Anakuwa Mtetezi wa kwanza. Kisha anampeleka mtetezi wa pili, ambaye ni Roho Mtakatifu. . Yeye ni Wakili mbele ya Baba dhidi ya mashtaka, Papa ameeleza na kuhoji Na ni nani basi mshitaki? Na kutoa jibu la Biblia,kwamba Mshitaki anaitwa Ibilisi , shetani. Na hivyo Mwisho wa Dunia, Yesu atahukumu lakini wakati huo huo ni mwombezi na mtetezi ..

Hatimaye, Papa Francisko , alisema, anayehukumu, humwinga Mkuu wa ulimwengu huu,ibilisi ambaye daima ni nyuma ya watu, akitaka kuwashtaki kwa Baba. Lakini Bwana, atatupa neema ya kumwiga Yesu, wakili na mwanasheria wetu. Na si kuwaiga wengine, ambayo mwisho wao ni huangamiza

Papa ameasa, iwapo tunataka kutembea katika njia ya Yesu, tunapaswa kuwa mawakali watetezi wale wanaotuhumiwa mbele ya Baba. Kwa namna gani tunaweza kuwa watetezi wa wengine wanaoshutumiwa, je ni kuingilia kati mara ? Hapana ni kukaa kimya na kwenda kusali na kumtetea mbele ya Bwana kama Yesu alivyofanya msalabani. Kusali kwa ajili yake na si kuhukumu. Ni vibaya kuhukumu kwa sababu, pia utahukumiwa

Papa aliwataka wote waliokuwa wakimsikiliza kukumbuka hilo siku zote , pale inapokuja hamu ya kutaka kuhukumu wengine , na kusema mabaya ya wengine, kuyashihnda majaribu hayo kwa kusali na kuomba neema ya kusamehe wengine..

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR