Tuesday, May 21, 2013

JUMAPILI

MATANGAZO 

   JUMAPILI TAREHE 24/05/2013
KIGANGO CHA BOKO:
MISA YA 1 SAA 12:15-2:00
MISA YA 2 SAA 2:00-4:00
MISA YA 3 SAA 4:00-5:30
MIKUTANO.
Halmashauri ya Walei Kigango cha Boko watakuwa na kikao mara baada ya misa ya 2, Wajumbe wa mkutano huo ni viongozi wote wa JNNK, Kanda na Wenyeviti wote wa vyama vya kitume. ukiwa mjumbe usikose kwa maandeleo ya Kigango chetu.

JUMAPILI TAREHE 24/05/2013
KIGANGO CHA MT. RAFAEL MBWENI MALINDI:
MISA YA 1 SAA 1:00-3:00
MISA YA 2 SAA 3:00-5:00

MIKUTANO.

JUMAPILI TAREHE 24/05/2013
KIGANGO CHA MBWENI:
MISA YA 1 SAA 1:15-3:00
MISA YA 2 SAA 3:10-5:00

MIKUTANO.

Miaka 10 tangu Mwenyeheri Maria de Mattias alipotangazwa kuwa Mtakatifu

Miaka 10 tangu Mwenyeheri Maria de Mattias alipotangazwa kuwa Mtakatifu: Wanovisi wanne waweka nadhiri za kwanza Jimboni Dodoma



Shirika la Masista Waabuduo Damu Takatifu ya Yesu linaadhimisha Kumbu kumbu ya Miaka 10 tangu Baba Mtakatifu Yohane Paulo wa pili alipomtangaza Mwenyeheri Maria de Mattias kuwa Mtakatifu hapo tarehe 18 Mei 2003. Itakumbukwa kwamba, ni Papa Pio wa XII aliyemtangaza kuwa Mwenyeheri kunako mwaka 1950.

Kumbu kumbu ya miaka kumi tangu Mtakatifu Maria de Mattias kutangazwa kuwa Mtakatifu imesherehekewa na Masista Waabuduo Damu Takatifu ya Yesu kwa: Makongamano, Ibada ya Misa Takatifu na Mafungo ya kiroho.

Shirika la Masista Waabuduo Damu Takatifu ya Yesu nchini Tanzania limeadhimisha Kumbu kumbu hii kwa Ibada ya Misa Takatifu iliyoongozwa na Askofu Gervas Nyaisonga wa Jimbo Katoliki Dodoma katika Kikanisa cha Makao Makuu ya Shirika hili, nchini Tanzania sanjari na Wanovisi wanne kuweka nadhiri zao za kwanza. Hawa ni Sr. Immaculata Sayumwe, Sr. Leticia Kisena, Sr. Maria Mrema pamoja na Sr. Theresia Mwendwa.

Katika Ibada ya Misa Takatifu, Askofu Nyaisonga amewataka watawa kulinda na kutunza thamani ya maisha na wito sanjari na kuienzi Damu Azizi ya Kristo mto wa rehema na chemchemi ya huruma na upendo wa Mungu kwa watu wake. Amewataka watawa kujiamini kwa kuwa Mwenyezi Mungu anaendelea kutembea pamoja nao katika hija ya maisha na imani. Watawa wanatakiwa kukumbuka kwamba, nadhiri zao ni bendera ya ushindi na mwenge unaowaangazia wengine nuru katika maisha.

Ibada hii ya Misa Takatifu imehudhuriwa na viongozi wa Kanisa, Watawa na Waamini walei kutoka ndani na nje ya Jimbo Katoliki la Dodoma.

Papa azindua katika Smartphone-habari za Fides

Papa azindua katika Smartphone-habari za Fides



Shirika la habari za kimissionari la Fides, limetangaza kwamba, habari zake zitapatikana katika lugha nane, kupitia mpango wa smartphones, unayoitwa "Missio", ambao unaopatikana bil malipo yaani bure.
Huduma hii ilizinduliwa na Papa Fransisko wakati alipokutana na Wakurugenzi wa Mashirika ya Kipapa ya Kitume ya Kitaifa ya Missioni na pamoja na wafanyakazi wa Fides, Ijumaa iliyopita , Mei 17 mjini Vatican.
Papa Francesco ilizindua utoaji wa habari huo kwa kubofya juu ya iPad, kama alivyombwa na Padre Andrew Small, OMI, Mkurugenzi wa Kitaifa wa Mashirika ya Mashirika ya Kipapa ya Misioni nchini Marekani.
Ukurasa huu wa Utume wa uinjilishaji , utakuwa unatoa habari za Kanisa zilizotolewa kupitia tovuto ya habari za Vatican "news.va", pia kuna picha, sinema na homilia za Papa, habari ya Kanisa katika ulimwengu na zitakuwa zikitolewa katika lugha nane.
Padre Small katika uzinduzi huo alimwambia Baba Mtakatifu,kwamba wanalenga kuiweka Injili, ndani ya mfuko wa kila kijana ulimwenguni ,maneno yaliyomgusa Papa Fransisko wakati akibofya kifungo kilichoandikwa juu yake maneno “sisi ni wainjilishaji”.
Katika siku yake ya kwanza ya kuzinduliwa kwa ukurasa huu, jumla ya watu 1,140 wa kutoka nchi 27 tofauti, waliutembelea ukurasa huo. Padre Small anasema lengo letu ni kuwasaidia watu kuiona dunia kupitia macho ya imani". Ukurasa huu unapatikana katika iTunes App na Google Play , ambamo ujumbe wa uinjlishaji, unatolewa katika lugha nane: Kiingereza, Kihispania, Kiitaliano, Kijerumani, Kifaransa, Kireno, Kichina na Kiarabu.Karibuni nyote.

Imani katika sala, unyenyekevu, na moyo wa ushujaa hutenda miujiza

Imani katika sala, unyenyekevu, na moyo wa ushujaa hutenda miujiza



Sala ujasiri nyenyekevu na uthabiti, hufanikisha miujiza: Papa alieleza hili, mapema Jumatatu wakati akiongoza Ibada ya Misa, katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta la mjini Vatican. Ibada iliyohudhuriwa na wafanyakazi mbali mbali ilikuwa ni Homilia ya Papa kwa wafanyakazi hao, ilirejea Liturujia ya Neno la siku, kifungu cha Injili ambamo wafuasi wa Yesu walishindwa kumponya kijana mdogo mgonjwa, na Yesu aliwajibu kwamba wameshindwa kumponya kijana huyo kwa sababu wana imani haba. Baba wa Kijana huyo kwa imani thabiti, aliomba msaada kwa Yesu. Na Yesu anawaambia kila kitu kinawezekana kwa anayeamini.
Papa Francesco alieleza, mara nyingi wapo wanaopenda kuwa wafuasi wa Yesu, lakini hawapendi kuhatarisha mengine wanaoyoyaamini na hivyo imani yao kwa Kristu inakuwa ni imani nusunusu, hawana imani nae kikamilifu. Papa alieleza na kuhoji kwa nini hali hi ya kutosadiki kikamilifui? Na alitoa jibu kwamba, wao wana amini kwamba, ni moyo wenyewe usiotaka kujifunua wazi, moyo unabaki umefungwa , lakini katika ukweli wake moyo huo unaotamani kuwa na imani thabiti.

Hivyo basi, binadamu anaushinikiza moyo kutojifunua na wala kujiweka chini ya maongozi ya Yesu, kama ilivyokuwa wakati ule, wanafunzi wa Yesu walimwuliza kwa nini, hawakuweza kumponya kijana, na Bwana aliwajibu kwamba aina mapepo yaliyomshambulia kijana huyo, hayawezi kutolewa nje na jambo lolote , isipokuwa kwa sala tu.
Papa alieleza na kusema, ingawa tunamtolea sala Bwana,ndani mwetu tuna kigugumizi cha imani. Hatuna imani thabiti na yule tunayemtolea maombi yetu lakini twayatolea maombi hayo kama majaribio au mazoea ya kusali. Ili Bwana aweze kuyaitikia maombi yetu, twapaswa kusadiki kwamba kile tunachomwomba Bwana atakifanikisha. Na hii ni kuwa na imani thabiti katika nguvu ya sala, ni kusadiki kw unyenyekevu kwamba, Yesu ni nguvu na anaweza kufanya muujiza.
Kuomba muujiza wa uponyaji , au kuomba mabadiliko katika mahusiano ni lazima kuambatane na sala thabiti inayotuhusisha sisi sote. Papa Francisko alieeleza na kutolea mfano wa tukio hilo lilitokea huko Argentina, ambako : mtoto wa miaka 7 aliugua na madaktari kutoa masaa machache ya maisha. Baba yake, fundi umeme, mtu wa imani, akiwa kama amepagawa na habari hii ya maisha ya mtoto wake kufika ukingoni, alipanda basi na kwenda katiak madhabahu ya Mama Bikira Maria ya Lulijan, umbali wa 70 km mbali, ambako alisali na kumlilia Mungu ayaokoe maisha ya mwanae na Mungu alisikia sala yake na aliporejea nyumbani alimkuta mtoto wake akiwa amepona. :

Papa alihitimisha homilia yake akisema tunahitaji kuomba kwa moyo wa imani na ushujaa zaidi kwamba Mungu anaweza kila jambo. Hakuna anayeweza kusema ni peke yake ni jasiri wa maombi, bali kila mmoja ni jasiri, kinachotakiwa ni kuwa na Imani kwa Bwana. Papa alieleza na kuwataka wote watoleee sala zao kwa imani thabiti kwa ajili ya watu wengi ambao wanakabiliwa katika vita, wakimbizi wote na wote wnaokabiliwa na hali ngumu za maisha zilizo nje ya uwezo wao akisemam twapaswa kusema, Bwana, naamini na msaada wangu utatoka kwako leo hii. .

GENERAL MEETING TYCW BOKO Parish- 01/06/2013

Tanzania Young Catholic Workers - Boko Parish

Praise JESUS ​​CHRIST:

          RE: NOTICE OF CHANGE OF DATE OF GENERAL MEETING TYCW parish

  Boko parish leadership you want to inform, all of TYC officials splicing level, region and community that the general meeting, which was to be conducted on 02.06.2013, now will be held on 01.06.2013, on Saturday, in the hall Sister, Boko parish. Time is starting at nine in the morning until ten at evening.

Each member is required to contribute Tshs 3,500 for lunch.

It is a very important meeting for the development of our mission, struggling to reach the whole of the five leaders of an existing level.

   Love .....................

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR