Wednesday, February 18, 2015

Masomo ya Jumatano ya Majivu

18

 FEBRUARY
 Kipindi cha Kwaresima: Jumatano ya Majivu. Mwaka "B".
SOMO  1: Yoe. 2:12 - 18

 Somo katika kitabu Cha Nabii Yoel
Lakini hata sasa, asema Bwana, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, na kwa kufunga, na kwa kulia , na kwa kuomboleza; rarueni mioyo yenu, wala si mavazi yenu, mkamrudie Bwana, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, naye haghairi mabaya. N'nani ajuaye kwamba hatarudi na kugeuka, na kutuachia baraka nyuma yake, naam, sadaka ya unga, na sadaka ya kinywaji, kwa Bwana, Mungu wenu?
Pigeni tarumbeta katika Sayuni, takaseni saumu, kusanyeni kusanyiko kuu; kusanyeni watu, litakaseni kusanyiko, kusanyeni wazee, kusanyeni watoto, na hao wanyonyao maziwa; Bwana arusi na atoke, chumbani mwake, na bibi arusi katika hema yake.
 Hao makuhani, wahudumu wa Bwana, na walie kati ya patakatifu na madhabahu na waseme, Uwaachilie watu wako, Ee Bwana, Wala usiutoe urithi wako upate aibu, hata mataifa watawale juu yako; kwani wasema kati ya watu, Yuko wapi Mungu wao?
 Hapo ndipo Bwana alipoona wivu kwa ajili ya nchi yake, akawahurumia watu wake. 

WIMBO WA KATIKATI. Zab. 51:1-4, 10-12, 15. 
K. Utuhurumie, ee Bwana kwa kuwa tumetenda dhambi 

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR