Showing posts with label kongamano la ujirani mwema. Show all posts
Showing posts with label kongamano la ujirani mwema. Show all posts

Friday, October 31, 2014

MAFUNZO YA WALIMU WA WALIMU wa UJASILIAMALI


 Mafunzo ya walimu wa walimu "Training of Trainers" kuhusu ujasiliamali yatatolewa kwa Halmashauri za VIWAWA za Parokia za BOKO na BUNJU siku ya Tarehe 08/11/2014 kwenye ukumbi wa Masista wa Karmeli Boko. Mafunzo yamepangwa kuanza saa 2:00 asubuhi. Pamoja na viogozi hao kijana yoyote mwenye nia na anayependa kuhudhuria anakaribishwa.

Tofauti na mafunzo mengine ya Ujasilimali ambayo hufundisha mfano: - jinsi ya kuzalisha bidhaa mbalimbali, mafunzo haya yatalenga katika kumwezesha kijana kutambua na kuzitumia mbinu zifuatazo: -

  • Je unataka kuzifahamu "Sifa 12 za mjasilimali mwenye mafanikio?"
  • Je unafahamu "Kanuni saba ambazo humuungoza mjasiliamali?"
  • Je unafahamu kuwa "biashara/ huduma/ bidhaa inao mzunguko wa maisha  na Ipo misingi ya kubadili biashara/ bidhaa husika iwapo haileti faida yoyote?".
  • Je ungependa "kubuni biashara mpya kabisa?"
  • Je ungependa kufahamu jinsi ya "Kuchagua bidhaa au huduma gani iwe biashara yako?"
  • Jifunze "Mbinu za kuingiza biashara/ bidha/ huduma sokoni"
  • Jifunze kuhusu "Vyanzo vya mitaji"
  • Jifunze kujiandalia mchanganuo wa biashara yako kwa kutumia "Njia rahisi ya kutayarisha mchanganuo wa biashara"

Hizi ni baadhi ya elimu utakazopata katika mafunzo haya na pia mengine mengi katika mfululizo wa mafunzo siku zijazo. Kumbuka Biashara inaishi, hukua na hubadilika, hivyo katika kila hatua mbinu muafaka zinahitajika ili isife.

 Mafunzo haya yamegawanyika kama ifuatavyo: - 40% nadharia na 60% jinsi ya kutenda. Kijana ukitoka katika mafunzo haya ya awali utajengwa kuwa mwalimu ambaye utashiriki kuongeza timu ya walimu wa ujasiliamali. Pia utaweza kubuni biashara yako mwenyewe na jinsi ya kuiingiza kwenye soko lenye ushindani mkali.

Mwana halmashauri, na kijana USIKOSE fursa hii adimu kwa gharama nafuu sana Jiandikishe sasa. Kwa mawasiliano piga simu namba 0713 900 905,0784 799 455, 0765 755 519 na0714 118 788


Mapendo…..



Thursday, October 30, 2014

Semina ya Awali (ujasiriamali na kijana)

Tarehe 08/11/2014, Halmashauri za VIWAWA, Parokia ya Boko na Bunju, Watakuwa na Semina Elekezi ya Ujasiriamali, Itakayofanyikia kwenye ukumbi wa masista Wakarmel Boko
Semina Hii itaanza saa 2:00 Asubuhi, na itaongozwa na Mkufunzi wetu, Mr. Aloyce Dinho, zaidi ya hawa viongozi pia tunawakaribisha vijana wengine wenye uelewa wa elimu ya ujasiriamali au wale ambao tayari wanafanya ujasiriamali.
unaweza kuwasiliana nasi kupitia number hii 0713 900 905. bonyeza hapa endelea kusoma hapa>>>>>>>

Monday, October 13, 2014

VIKAO VYA MAANDALIZI (KONGAMANO LA UJIRANI MWEMA


VIKAO VYA MAANDALIZI (KONGAMANO LA UJIRANI MWEMA.

Baada ya ya kukutana na wadai na walezi wetu kwa malengo ya kuboresha Kongamano letu, Jumapili ijayo ya tarehe 19/10/2014, tutakuwa na kikao cha kwanza ambacho kitawahusicha wajumbe wote wa Halmashauri ya VIWAWA parokia ya Bunju na Boko, kikao hichi kitafanyikia Parokiani Bunju mara baada ya misa ya Pili ni Muhimu ukiwa mjumbe kuhuzuria, pia Ticketi za ushiriki zitaanza kupatikana hiyo siku tarehe 19/10/2014, kwa Wahazini wote wa Ngazi ya Parokia, Kigango na Jumuiya kwa Tshs 18,000 tu wahi mapema upate ticketi yako. nafasi ni kwa vijana 140 tu

Monday, October 6, 2014

KONGAMANO NA UJIRANI MWEMA

Kongamano hili litakuwa la Mkesha washiriki watatakiwa kuwasili Parokiani Boko siku ya Ijumaa tarehe 28/11/2014 saa tisa alasiri,na tunatarajia kuwa na semina na midahalo kwa usiku mzima, jumamosi ya tarehe 29/11/2014, saa kumi alasiri washiriki wote watarejea majumbani kwao baada ya kushibishwa kwa semina, midaho na michezo.

Washiriki kwenye Kongamano hili ni Vijana wote wenye Umri kuanzia miaka kumi na nane(18) wa Parokia ya Boko, Bunju na  Vijana wengine kutoka kwenye Parokia Mbali mbali za Jimbo kuu la Dar es  .
MWAKA WA FAMILIA.
Inafurahisha kuona kwamba, wazee wawili na vijana wawili wanakutanishwa na Yesu. Hii
inaonesha kwamba, Yesu ana uwezo wa kukutanisha na kuunganisha vizazi, kwani Yeye ni
chemchemi ya upendo inayovuka ubinafsi, upweke na masikitiko. Baba Mtakatifu anasema,
familia katika hija ya maisha yao wanashirikishana na kumegeana mambo mengi mema:
chakula na mapumziko; kazi za nyumbani, starehe, sala, safari na hija ya maisha ya kiroho
pamoja na matendo ya huruma.
Pale panapokosekana upendo, hapo hukosekana furaha , Upendo wa kweli
unabubujika kutoka kwa Kristo kwa njia ya Neno lake ambalo ni mwanga katika mapito ya
waamini; anawapatia Mkate wa maisha ya uzima wa milele, unaowasaidia waamini kupambana
na changamoto za maisha ya kila siku.
Baba Mtakatifu Francisko kama sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya Sinodi Maalum ya
Maaskofu kwa ajili ya Familia itakayoadhimishwa Mwezi Oktoba 2014 mjini Vatican, kwa
kuongozwa na kauli mbiu "Changamoto za kichungaji kuhusu familia mintarafu Uinjilishaji"
ameandika barua kwa familia zote duniani ili kukazia dhamana ya Kanisa kuendelea kutangaza
Injili kwa kukabiliana kinaga ubaga na changamoto mpya zinazohusu familia.
Baba Mtakatifu anasema, maandalizi haya yanawahusu Watu wote wa Mungu kwa kuhakikisha
kwamba, wanashiriki kikamilifu kwa kutoa mawazo pamoja na kusindikiza mchakato mzima kwa
njia ya sala, jambo muhimu sana kutoka kwa familia zote. Sinodi hii ni maalum kwa ajili ya: wito
na utume wa Kanisa na Jamii; matatizo yanayowakabili wanandoa; maisha ya kifamilia, elimu
na malezi kwa watoto; dhamana na utume wa familia katika maisha ya Kanisa.
Hivyo nakualika kijana mwenzangu uungane nasi hiyo siku katika kuyachambua haya kwa kina anza sasa kufanya maandalizi

ELIMU YA UJASIRIAMALI.
Elimu ya ujasiriamali katika nchi yetu haina ‘umri’ mkubwa kama zilivyo taaluma nyingine zikiwamo lugha, historia, siasa na sayansi. Hii ni kutokana na historia ya nchi yetu hasa baada ya kupata uhuru, kwamba tuliamua kufuata siasa ya ujamaa na kujitegemea kupitia Azimio la Arusha.
Siasa ya ujamaa na kujitegemea haikushadidia ujasiriamali kwa vile ulifananishwa na ubepari ambao ulichukuliwa kama unyama. Wale wote waliokuwa wanajihusisha na shughuli za kijasiriamali hasa biashara katika kipindi hicho walionekana kama ‘wanyama’ au watu ambao walikuwa wamechepuka kutoka katika njia kuu ambayo ilikuwa inaaminiwa na jamii kubwa wakati huo.
Wafanyakazi serikalini walikuwa hawaruhusiwi kujihusisha na biashara na kwamba shughuli za ujasiriamali zilionekana kufanywa na watu ambao hawakuwa na elimu ya kutosha kupata ajira, na wageni hasa kutoka Bara la Asia kama vile Wahindi.
Hata hivyo, kutokana na hali halisi ya maisha katika nchi yetu na duniani kwa jumla, kwenye miaka ya katikati ya 2000, taifa lilianza utaratibu wa kuingiza elimu ya ujasiriamali katika elimu ingawa haikuwekewa kipaumbele sana. Kwa sasa elimu ya ujasiriamali imekuwa kama wimbo wa taifa, siyo shuleni na vyuoni bali hata katika sekta ambazo si rasmi kama ambavyo tumekuwa tukishuhudia matangazo mbalimbali juu ya kuendesha elimu ya ujasirimali katika makundi mbalimbali ya jamii yetu.
Kutokana na wanajamii na taifa kwa jumla kuanza kuona elimu ya ujasiriamali kama mwarobaini wa matatizo yanayowakabili kama vile ajira na umaskini, lengo la la Kongamano letu  ni kuelezea umuhimu wa elimu ya ujasiriamali katika Chama chetu cha VIWAWA  kama njia mojawapo yenye kuonyesha jinsi elimu ya ujasiriamali inavyoweza kuisaidia jamii na taifa katika kuleta maendeleo.
Ujasiriamali ni mchakato au hali waliyonayo baadhi ya watu ya kutaka mafanikio yanayoshadadiwa na moyo wa ushindani, kujiamini, uwezo binafsi wa kukabiliana na kutatua changamoto zilizopo ikiwa ni pamoja na uthubutu wa kukabiliana na changamoto ambazo wakati mwingine huweza kuathiri maisha yao katika kipindi cha mpito.
Kumekuwa na mjadala wa muda mrefu kama ujasiriamali hufundishwa au mtu huzaliwa nao ingawa si lengo la kongamano letu si kujikita katika mjadala huo, kwa kuwa tunaelewa nguvu iliyonayo elimu katika kuyatengeneza maisha ya mwanadamu.
Tunaamini kuwa vijana wana maono na matamanio yao katika maisha kama walivyo watu wazima ingawa watu hawa wawili wanaweza kutofautiana hapa na pale kutokana na sababu za umri, mazingira, wakati na uzoefu katika maisha.
Elimu ya ujasiriamali katika Vyama au kikundi  hujenga msingi mzuri wa kujiamini miongoni mwa vijana na hivyo kuwafanya wayakabili maisha bila woga, jambo ambalo litawafanya kufanya kazi zao wanazozipenda kwa umahiri, weledi na kujiamini zaidi.
hivyo basi nakusi sana kuungana nasi katika kupata elimu hiyo, tunatarajia pia kuunda vikundi vya ujasiriamali kwa vijana watano watano na kuwapatia wataalamu watakao wasimamia.
kwa maelezo zaidi tuandikie kupitia viwawaboko@yahoo.com au piga 0713 900 905


NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR