Sunday, February 1, 2015

Tafakari ya Jumapili ya 4 ya Masomo ya Mwaka B tarehe 01/02/2015

Mwandishi wa kitabu cha Kumbukumbu la Torati ambamo tunapata somo la kwanza
anatualika kutambua kuwa Mungu haachi kutimiza ahadi yake ya kale kwamba atamtuma Nabii atakayetangaza hukumu zake kwa haki, atakayesema yale ya Bwana na kama atasema kinyume atakufa. Manabii wengi walitangaza ujumbe wa Mungu lakini hasa katika zama zetu Mungu anasema nasi kwa njia ya Masiha kama ambavyo Wayahudi walielewa ujumbe huo wa Neno la Mungu.

Masomo ya Tarehe 01/02/2015, Jumapili: Dominika ya 4 ya Mwaka "B".

01

February

 Jumapili: Dominika ya 4 ya Mwaka "B".
SOMO  1. Kumb. 18:15-20

 Bwana, Mungu wako, atakuondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zako kama nilivyo mimi; msikilizeni yeye. Kama vile ulivyotaka kwa Bwana, Mungu wako, huko horebu, siku ya kusanyiko, ukisema, nisisikie tena sauti ya Bwana, Mungu wangu, wala nisiuone tena moto huo mkubwa, nisije nikafa. Bwana akaniambia, wametenda vyema kusema walivyosema . Mimi nitawaondoshea Nabii miongoni mwa ndugu zao mfano wako wewe, nami nitatia maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru. Hata itakuwa, mtu asiyesikiliza maneno yangu atakayosema yule kwa jina langu, nitalitaka kwake. Lakini Nabii atakayenena neno kwa kujikinai kwa jina langu, ambalo sikumwagiza kulinena, au atakayenena katika jina la miungu mingine, nabii yule atakufa.

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR