Showing posts with label MATANGAZO/ MASOMO J2 YA DOMINIKA YA 23 MWAKA C TAREHE 13/10/13. Show all posts
Showing posts with label MATANGAZO/ MASOMO J2 YA DOMINIKA YA 23 MWAKA C TAREHE 13/10/13. Show all posts

Thursday, October 10, 2013

MASOMO NA MATANGAZO YA J2 YA DOMINIKA YA 23 MWAKA C TAREHE 13/10/13

JUMAPILI DOMINIKA YA 28 ya Mwaka C.
      RATIBA ZA IBADA 
KIGANGO CHA MH. ISIDORI BAKANJA- BOKO.
MISA YA KWANZA 12:15-2:00 ASUBUHI
MISA YA PILI     SAA 2:00-4:00 ASUBUHI
MISA YA TATU SAA 4:00-5:30 ASUBUHI
KIGANGO CHA MT. FRANCIS WA ASIZ-MBWENI 
MISA YA KWANZA SAA 1:10-3:00 ASUBUHI
MISA YA PILI SAA 3:00-4:30 ASUBUHI

KIGANGO CHA MT. RAFAEL-MBWENI MALINDI
SAA 1:00-3:00 ASUBUHI.
MISA YA PILI SAA 3:00-5:00

KIGANGO CHA ANTHONY WA PADUA-MBWENI TETA
MISA NI SAA 3:00-5:00.


MASOMO 

 Somo 1:2Fal.5:14-17
Naamani alishuka, akajichovya mara saba katika Yordani, sawasawa na neno lake yule mtu wa Mungu; nayo nyama ya mwili wa mtoto mchanga, akawa safi. Akamrudia yule mtu wa Mungu, yeye na mafuatano yake yote. akaja akasimama mbele yake; akasema sasa tazama, najua ya kwamba hakuna Mungu duaniani mwote, ila katika Israel, basi nakuomba upokee mbaraka kwa utumwa wako. lakina akasema, kama Bwana aishivyo, ambaye nimesimama mbele yake, sipokei kitu. Akamshurutia apokee; lakini akakataa. naamani akasema, kama sivyo, lakini mtumwa wako na apewe mzigo wa udongo wa baghala wawili; kwa maana mtumwa wako hatatoa tena sadaka ya kuteketezwa wala dhabihu kwa miungu mingine, ila kwa Bwana.

SOMO 2: 2Tim.2:8-13
Mkumbuke Yesu Kristo, aliyefufuka katika wafu, wa uzao wa Daudi kama inenavyo Injili yangu. Nami katika hiyo nimeteswa hata kufungwa kama mtenda mabaya; lakini neno la Mungu halifungwi. Kwa ajili ya hilo nastahimili mambo yote, kwa ajili ya wateule, ili wao nao waupate wokovu ule ulio katika kristo Yesu, Pamoja na utukufu wa Milele.
 Ni neo la kuaminiwa. kwa maana, kama tukifika pamoja naye, 
Tutaishi pamoja naye pia: kama tukistahimili tutamiliki pamoja naye;
Kama tukimkana yeye, yeye naye atatukana sisi, 
Yeye hudumu wa kuaminiwa. Kwa maana hawezi kujikana mwenyewe.

INJILI. :Lk.17:11-19
Yesu alipokwenda njiani kwenda Yerusalemu, alikuwa akipita katikati ya Samaria na Galilaya. Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali, wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu! Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajioshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika a mmoja wao alipoona kwamba wamepona, alirudi, huku akimtukuzaMungu kwa sauti kuu; akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa msamaria. Yesu akamjibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wako wapi? je! Hawakuonekana waliorudi kumpa Mungu Utukufu ila mgeni huyu? akamwambia, Inuka, nenda zako, Imani yako Imekuokoa.
             
  1.  Maandalizi ya Dekania Cup yanaendelea kwa upande wa tImu ya Mpira wa  Pete.


  1. tunawakumbusha vijana wote kuendelea kulipa ada kwa maendeleo ya chama chetu..... mapendo sana malipo kwa njia ya benk kwa jina na number hii :viwawa parokia ya boko account no 01524526820100 crdb bank tegeta branch
JIANDAE NA ZIARA YA UINJILISHAJI MWAKA 2014.....................

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR