Showing posts with label masomo ya dominika ya 29 ya mwaka C. Show all posts
Showing posts with label masomo ya dominika ya 29 ya mwaka C. Show all posts

Thursday, October 17, 2013

JUMAPILI DOMINIKA YA 29 ya Mwaka C. Tarehe 20/10/2013

JUMAPILI DOMINIKA YA 29 ya Mwaka C.
      RATIBA ZA IBADA 
KIGANGO CHA MH. ISIDORI BAKANJA- BOKO.
MISA YA KWANZA 12:15-2:00 ASUBUHI
MISA YA PILI     SAA 2:00-4:00 ASUBUHI
MISA YA TATU SAA 4:00-5:30 ASUBUHI
KIGANGO CHA MT. FRANCIS WA ASIZ-MBWENI 
MISA YA KWANZA SAA 1:10-3:00 ASUBUHI
MISA YA PILI SAA 3:00-4:30 ASUBUHI

KIGANGO CHA MT. RAFAEL-MBWENI MALINDI
SAA 1:00-3:00 ASUBUHI.
MISA YA PILI SAA 3:00-5:00

KIGANGO CHA ANTHONY WA PADUA-MBWENI TETA
MISA NI SAA 3:00-5:00.


MASOMO 

 Somo 1:Kut.17:8-13
Wakati huo Waameleki walitokea, wakapigana na Israel huko Refidimu. Musa akamwambia Yoshua, Tuchagulie watu, ukatoke upigane na waameleki; kesho nitasimama juu ya kilele kile, na ile fimbo ya Mungu nitakuwa nayo mkononi mwangu. Basi Yoshua akafanya kama Musa alivyomwambia, akapigana na Amaleki; na Musa na Haruni na Huri wakapanda juu ya kile kilima. Ikiwa Musa alipoinua mkono wake, Israel walishinda; na aliposhusha mkono wake, Amaleki walishinda. lakini mikono ya Musa ilikuwa mizito; bali wakatwa jiwe, wakaliweka chini yake akalikalia. Haruni na Huri wakaitegemeza mikono yake, mmoja upande huu na mmoja upande huu; mikono yake ikathibitika hata jua lilipokuchwa. Yoshua akamwaangamizaAmaleki na watu wake kwa ukali wa upanga.

SOMO 2: 2Tim.3:14 - 4:2
Wewe ukae katika mambo yale uliyofundishwa na kuhakikishwa, kwa maana unajua ni akina nani ambao ulijifunza kwao; na ya kuwa tangu utoto umeyajua maandiko matakatifu, ambayo yanaweza kukuhekimisha hata upate wokovu kwa Imani iliyo katika Kristo Yesu. kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema. nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, atakayehukumu waliohai na waliokufa; kwa kufunuliwa kwake na kwa ufalme wake; lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho.

INJILI. :Lk.18:1-8
Yesu aliwaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu siku zote, wala msikate tamaa. Akasema, palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu. Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea endea , akisema, nipatie haki na adui wangu. Naye kwa muda alikata tamaa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu, lakini kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima. Bwana akasema, sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu. Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao? Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?
             
  1.  Maandalizi ya Dekania Cup yanaendelea kwa upande wa tImu ya Mpira wa  Pete jumamosi tarehe 19 wanacheza kutauta mshindi wa tatu dhidi ya bunju.


  1. tunawakumbusha vijana wote kuendelea kulipa ada kwa maendeleo ya chama chetu..... mapendo sana malipo kwa njia ya benk kwa jina na number hii :viwawa parokia ya boko account no 01524526820100 crdb bank tegeta branch
JIANDAE NA ZIARA YA UINJILISHAJI MWAKA 2014.....................

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR