Showing posts with label tafakari ya unjili ya siku ya alhamisi 12/2/2015. Show all posts
Showing posts with label tafakari ya unjili ya siku ya alhamisi 12/2/2015. Show all posts

Thursday, February 12, 2015

Alhamisi, 12 Februari 2014 Juma la 5 la Mwaka

"Asali itokayo Mwambani"

Mwa 2:18-25;
Zab 128:1-5;
Mk 7:24-30;

Imani huamisha milima

Katika Injili ya leo, Yesu anamfukuza pepo kutoka kwa binti wa mwanamke Mkanaani. Yesu, hapa, alijionyesha kama mwanga wa mataifa. Wayahudi walimkataa Kristo, lakini watu wa mataifa wali mkaribisha na wakamwamini. Mwanamke wa Kikanaani, alikuwa mgeni kwa jamii ya Israeli, lakini imani yake katika Yesu ilkua zaidi kuliko imani ya Wayahudi. Imani ya mwanamke huyu ilikuwa kubwa. Hata katika tusi dhahiri ya Yesu, ambaye alimwita 'mbwa,' yeye aliibuka kama mwanamke wa imani kubwa, ambayo haiwezi kulinganishwa na yoyote ya Wayahudi. Hii ilikuwa kama ile ya kumpima Ibrahimu. Je, una imani kama mwanamke wa Kikanaani?

Maombi: Bwana, Nisaidie kuongeza Imani yangu kwako Amina!

Bonyeza LIKE kwa ukurasa wetu
www.facebook.com/viwawaboko

tarehe 18/02/2015, ni jumatano ya majivu tuanze kujianda kwa safari ya ukombozi........

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR