Showing posts with label Kipindi cha Kwaresima: Masomo ya Jumapili ya pili (2) Mwaka B wa Kanisa.. Show all posts
Showing posts with label Kipindi cha Kwaresima: Masomo ya Jumapili ya pili (2) Mwaka B wa Kanisa.. Show all posts

Friday, February 27, 2015

Masomo ya Jumapili ya Pili ya Kwaresima Mwaka B (Tarehe 01/03/2015)

01

 Marchi
 Jumapili ya 2 ya Kwaresima Masomo ya Mwaka "B".
SOMO  1: Mwa. 22:21- 2, 9a, 10-13, 15-18

Somo katika kitabu cha Mwanzo.
Mungu alimjaribu Ibrahimu, akamwambia, Ee Ibrahimu! Naye akasema, Mimi hapa. Akasema, Uchukue mwanao, mwana wako wa pekee, umpendaye, Isaka, ukaende zako mpaka nchi ya Moria, ukamtoe sadaka ya Kuteketezwa huko juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia. Wakafika mahali pale alipoambiwa na Mungu. Ibrahimu akanyosha mkono wake, akakitwaa kisu ili amchinje mwanawe. Ndipo malaika wa Bwana akamwita kutoka mbinguni, akasema, Ibrahimu! Ibrahimu! Naye akasema, Mimi hapa. Akasema, usimnyoshee kijana mkono wako, wala usimtendee neno; kwa maana sasa ninajua ya kuwa unamcha Mungu, iwapo hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee. Ibrahimu akainua macho yake, akaangalia, na tazama, Kondoo mume yuko nyuma yake, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi Ibrahimu akaenda akamtwaa huyo kondoo, akamtoa awe sadaka ya kuteketeza badala ya mwanae. Malaika wa Bwana akamwita Ibrahimu mara ya pili kutoka mbinguni, akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema Bwana, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee, katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga uliopo pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao; na katika uzao wako mataifa yote duniani watajibarikia; kwa sababu umetii sauti yangu.

WIMBO WA KATIKATI. Zab. 116:10, 15-19. 
K. Nitaenenda mbele za Bwana
         Katika nchi za walio hai..

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR