Friday, June 21, 2013

MSALABA WA YESU

Msalaba wa Yesu ni msalaba ule ambao Yesu Kristo alisulubiwa juu yake huko Yerusalemu kwa mamlaka ya Ponsio Pilato labda tarehe 7 Aprili 30 BK.
Adhabu hiyo kali ilianza huko Uajemi na kuenea hadi Dola la Roma ambalo liliitumia hasa katika maeneo ya pembeni.
Tukio hilo, pamoja na ufufuko wa Yesu unaosadikiwa na Ukristo kutokea siku ya tatu (Jumapili ya Pasaka), ndio kiini cha imani ya dini hiyo mpya iliyotokana na ile ya Uyahudi.

Kwa Wakristo fumbo hilo la Pasaka ndilo kilele cha historia ya wokovu inayotangazwa na Biblia ya Kikristo.
Fumbo hilo lilisababisha kazi nyingi za sanaa, hasa uchoraji.
Na tunatakiwa kuyafananisha mahangaiko ya maisha yetu kama msalaba wa Yesu tukiwa na imani kuwa mwisho tutaufikisha na tutafariki na kurudi kwa Mungu Baba hapo tutapata raha ya milele pamoja na Watakatifu wote.

ziara ya Mbulu tarehe 26June13

Tumsifu Yesu Kristo,
YAH:SAFARI YA ZIARA YA UINJILISHAJI PAROKIA YA DAUDI JIMBO LA MBULU MKOANI MANYARA.
Husika na kichwa cha habari hapo juu, siku ya jumatano tarehe 26/06/2013, VIWAWA wataanza safari ya kuelekea Jimbo la Mbulu Mkoani Manyara.
Kwanza tunatoa shukrani kwa Wazazi, Walezi, Viongozi wa JNNK kwa ushirikiano mkubwa waliotupatia kwa kuwachangia Vijana na kuwaruhusu kushiriki katika ziara hii.
Safari itaanzia Parokiani Boko saa kumi na moja asubuhi, na tunatarajia kwenda kupumzika katika mji wa Karatu Mkoani Arusha, Siku ya Alhamisi tarehe 27/06/13 tutaenda Ngorongoro na mchana tutafanya ziara katika Parokia ya Endabashi, Jioni tutaenda Parokia ya Mt. Francisco wa Asizi –Kijiji cha Daudi hapo tutakaa mpaka tarehe 29/06/2013. Jumapili Tarehe 30/06/2013 tutaenda Parokia ya Mt. Yosefu Mfanyakazi(JIMBONI), na kushiriki Ibada ya Misa Takatifu na baadaye kukutana na Vijana wenzetu. Jioni tutaanza safari na tutapumzika Karatu na tarehe 01/-7/2013, saa kumi na moja asubuhi tutaanza safari ya kurudi Dar es salaam.
Tuzidi kuombeana katika kufanikisha ziara hii ya kitume. Tunamwomba Mungu aongoze safari yetu, malaika mikaeli mlinzi wa safari atuongoze.
Mapendo..................................................

MSIMAMO WA LIGI YA PAROKO CUP LEO



Matokeo ya mechi ya Kundi A tarehe 21/06/2013




Kigango cha Mbweni 0 Kigango cha Mt. Gasper 2




Matokeo ya mechi ya Kundi B tarehe 19/06/2013




Kigango cha Mt anthony wa Padua Mbweni Mpiji 3 Kigango cha Mt.Maria del Mathias 3





MSIMAMO WA LIGI YA Paroko cup 2013





PAROKO CUP 13 :KUNDI A
TIMUMechiImeshindaImefungwaSare Magoliwaliofungwapoint

Mt.Gasper Boko11002 0 3
Mbweni10 1002 0
Damu Takatifu Boko000000 0


MSIMAMO WA LIGI YA Paroko cup 2013





PAROKO CUP 13 :KUNDI
TIMUMechiImeshindaImefungwaSare Magoliwaliofungwapoint

ANTHONY WA PADUA100133 1
MARIA DEL MATHIAS100133 1
RAFAEL000000 0

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR