Showing posts with label SHEREHE YA KUPAA BWANA MWAKA "A" masomo dominika 01/06/2014 jumapili. Show all posts
Showing posts with label SHEREHE YA KUPAA BWANA MWAKA "A" masomo dominika 01/06/2014 jumapili. Show all posts

Thursday, May 29, 2014

SHEREHE YA KUPAA BWANA MWAKA "A" masomo dominika 01/06/2014 jumapili



01
   JUNI 
 SHEREHE YA KUPAA BWANA MWAKA "A"


RATIBA ZA IBADA
KIGANGO CHA BOKO.
IBADA YA MISA YA KWANZA 12:15 – 1:45 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 2:00 – 3:50 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA TATU SAA 4:00-5:20 ASUBUHI
KIGANGO CHA MBWENI.
IBADA YA MISA YA KWANZA 1:15 – 2:55 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 3:00 – 4:50 ASUBUHI
KIGANGO CHA MT. RAFAEL.
IBADA YA MISA YA KWANZA 1:00 – 2:55 ASUBUHI
IBADA YA MISA YA PILI 3:00 – 4:50 ASUBUHI
KIGANGO CHA ANTHONY WA PADUA – MBWENI TETA.
IBADA YA MISA NI 3:00 – 5:00ASUBUHI
ZAB:47:1-2,5-6,7-8
SOMO LA 1: Mdo. 1:1-11

Kitabu kile cha kwanza naliandika, Theofilo, katika habari ya mambo yote aliyoanza Yesu kufanya na kufundisha, hata siku ile alipochukuliwa juu, alipokuwa amekwisha kuwaagiza kwa Roho Mtakatifu wale Mitume aliowachagua; wale alowadhihirisha mafsi yake, kwa dalili nyingi, baada ya kuteswa kwake, ya kwamba yu hai, akiwatokea muda wa siku arobaini, na kuyanena mambo yaliyohusu ufalme wa Mungu. Hata alipokuwa amekutana nao aliwaagiza wasitoke Yerusalemu, bali waingoje ahadi ya Baba, ambayo mlisikia habari zake kwangu; ya kwamba Yohane alibatiza kwa maji, bali ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu baada ya siku hizi chache. basi walipokutanika , wakamuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli ufamle? Akawaambia, si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe. Lakini mtapokea nguvu, ikiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa Nchi. Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, akainuliwa, wingu likampokea kutoka machoni pao. Walipokuwa wakikaza macho mbinguni, yeye alipokuwa akienda zake, tazama watu wawili wakasimama karibu nao, wenye nguo nyeupe, wakasema Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkatazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hivyo mlivyomwona akienda zake mbinguni.

Somo 2:Efe.1:17-23

Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu awape ninyi Roho ya hekima na ya ufunuo katika kumjua yeye; macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo; na ubora wa ukuu wa uweza wake ndani yetu tuaminio jinsi ulivyo; kwa kadiri ya utendaji wa nguvu za uweza wake; aliotenda katka kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; juu sana kuliko ufamle wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajalwo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia; akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote.

INJILI:Mt. 28:16-20

Wale wanafunzi kumi na moja walikwenda Galilaya mpaka mlima ule aliowaagiza Yesu. Nao walipomwona, walimsujudia; lakini baadhi yao waliona shaka. Yesu akaja kwao, akawaambia, nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho mtakatifu; na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi sikuzote, hata ukamilifu wa dahari.

Matangazo mbali mbali
Jumapili hii tarehe 01/06/14 kutakuwa na kikao cha vijana wote wanaoshiriki ziara ya uinjilishaji parokia za Dareda, Sanu, Daudu na endabashi, kikao kitafanyikia parokiani Saa 4:00 asubuhi mara baada ya ibada ya pili.
zaidi......

jdhibitisha ushiriki wako kwenye ziara ya Dareda 01-07/07/14 kwa kulipa ada ya ushiriki sasa ni tshng 150000 lipa kwa mhazini wako jumuiya, kigango au parokia.....tunawatakia maandalizi mema.

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR