Sunday, January 11, 2015

Masomo ya Tarehe 11/01/2015 mwaka B, wa Kanisa Dominika ya sikuku ya Ubatizo wa Bwana2015

11

 Januari
 Jumapili: ya Ubatizo wa Bwana.
SOMO  1. Isa. 42:1-4, 6-7

 Bwana asema: Tazama mtumishi wangu nimtegemezaye; mteule wangu, ambaye nafsi yangu imependezwa naye; nimetia roho yangu juu yake; naye atawatolea mataifa hukumu. Hatalia, wala hatapaza sauti yake, wala kuifanya isikiwe katika njia kuu. Mwanzi uliopondeka hautavunjika, wala utambi utokao moshi hautazima; atatokeza hukumu kwa kweli. Hatazimia , wala hatakata tamaa, hata atakapoweka hukumu duniani; na visiwa vitaingojea sheria yake. Mimi, Bwana, nimekuita katika haki, nami nitakushika mkono, na kukulinda, na kukutoa uwe agano la watu, na nuru ya mataifa; kuyafunua macho ya vipofu, kuwatoa gerezani waliofungwa, kuwatoa wale walioketi gizani katika nyumba ya kufugwa.

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR