Monday, November 24, 2014

Changamkieni Uinjilishaji wa kina kwa furaha na unyofu wa moyo Ungana nasi tena 2015, Kiabakari - Musoma.


Askofu Beatus Kinyaia wa Jimbo la Mbulu

Beatus Kinyaia ateuliwa kuwa Askofu Mkuu wa jimbo kuu Katoliki la Dodoma.

Hatimaye leo baba Mtakatifu Papa Francisco amempandisha kutoka  askofu hadi kuwa askofu Mkuu askofu Beatus Kinyaiya, O.F.M. Cap (pichani) wa jimbo kuu Katoliki la Dodoma.


Askofu Beatus Kinyaiya alizaliwa Mei 9, 1957. Akapata daraja takatifu la Upadre katika shirika la Kimisionari la Wafranciscan Minor  tarehe 25 juni, 1989.


Aliteuliwa kuwa askofu wa jimbo Katoliki la Mbulu tarehe 22 Aprili, 2006, nakusimikwa/ wekwa wakfu rasmi na Kardinali Polycarp Pengo  kuwa askofu wa jimbo la Mbulu tarehe 2 Julai 2006.


Leo tarehe 06 Novemba, 2014 ameteuliwa kuwa askofu Mkuu wa Jimbo Kuu katoliki la Dodoma ambalo nalo limepandishwa hadhi na kuwa jimbo kuu.

Atasimikwa rasmi kuanza utume wake huo mpya katika jimbo hilo mwezi wa Januari, 2015.

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR