Thursday, October 17, 2013

Katekesi ya Papa- Tunasadiki katika Kanisa moja la Kitume kwa sababu.....



Katekesi ya Baba Mtakatifu Francisko kwa mahujaji na wageni, inaendelea kuitafakari sala ya Kanisa, ya Nasadiki, Jumatano hii akitazama kifungu Nasadiki katika Kanisa moja Takatifu na la Kitume. Na alianza kwa kuwahoji mahuajii na wageni wanaofika Roma kwa ajili ya hija , iwapo wamewahi kujiuliza ina maana gani kusema , Kanisa la Mitume na umuhimu wa Mitume Petro an Paulo, ambao waliyatoa maisha yao hapa Roma , kwa ajili ya kuifikisha Injili na kuishuhudia Injili . Lakini pia akasema, kuna zaidi katika hilo....

Papa alieleza na kusisitiza kwamba Kanisa la kitume, kwa sababu, lina uhusiano kina, katika urithi wake na Mitume kwa kwanza, lile kundi dogo la wanaume kumi na wawili walioitwa na Yesu kwa majina na kuishi nae na hatimae kuwatuma nje kuhubiri mafundisho yake ( Mk 3:13-19 ).

Papa alieleza na kufafanua maana ya neno “Apostolo” Mtume , kwamba ni neno la Kigiriki lenye maana ya "aliyetumwa ", ni mtu anayepeleka ujumbe wa kufanya jambo fulani. Ni neno lenye nguvu , na Mitume waliitwa na kuchaguliwa na Yesu kuendeleza kazi yake , ya kusali na kupeleka habari njema ya upendo wa kuokoa kwa watu wote. Hivyo sala na kutangaza Injili , inakuwa ni kazi ya kwanza muhimu ya mtume.. Papa ametaja hili ni muhimu kwa sababu, mara nyingi , wengi tunafikiri, kuwa mtume ni kwenda kuihbiri injili peke yake. Sivyo, ni kufanya kazi nyingi ...
Papa alifafanua, na kurejea siku za mwanzo wa Kanisa, akisema, pia kulikuwa na matatizo na vikwazo kwa mitume kulingana na wakati wao. Na hivyo walitayarisha watu wengine kama mashemasi, katika kukabilaina na kupungukiwa na wakati wa kuomba na kutangaza Neno la Mungu. Na kama tunavyo fikiri juu waandamizi wa Mitume - Maaskofu, na pia Papa,ambao nao pia wana tatizohili la kupungukiwa na muda wa kusali na kuitangaza Injili kama warithi wa mitume. kwa muono huo, Papa Francisko amesisitiza, kila muumini wa kanisa ni mtume, kwa sababu yumo ndani ya Kanisa la kitume. Na hivyo waamini wote wanatakiwa kuwa mitume katika kazi yake ya kuihubiri Injili ya wokovu wa ulimwengu.
Papa alieleza na kutaja mambo matatu katiak mafundisho yake kwamba, Kanisa ni la kitume kwa sababu, limejengwa juu ya maombi na mahubiri ya Mitume, kwa mamlaka yalitolewa kwa mitume na Kristo mwenyewe,kama alivyoandika Mtakatifu Paulo kwa Wakristo wa Efeso (2, 19-20) .
Pili Kanisa ni la kitume kwa sababu hudumisha ukamilifu wa mafundisho ya Kristu na njia za wokovu, kwa msaada wa Roho Mtakatifu , kama inavyo eleza Kateksimu ya Kanisa. Kanisa karne hadi karne limetunza hazina hii ya thamani, ambayo ni maandiko matakatifu , mafundisho , sakramenti, huduma ya wachungaji, ili twaamini waweze kuwa waaminifu kwa Kristo na kuyashiriki maisha yake.
Na tatu Kanisa ni la kitume kwa sababu, ujumbe wake uliodmanishwa kwa mitume ni ujumbe wa injili kwa dunia nzima, unaoendelea katika njia ya historia ya ujumbe huo, ambao Yesu aliukabidhi Mitume. Yesu mwenyewe alisema, nendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi wangu, mkiwabatiza kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi . Na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote , mpaka mwisho wa ulimwengu "( Mt 28:19-20). Na hivyo Kanisa mizizi yake imo katika mafundisho ya Mitume, mashahidi wa kweli wa Kristo. Hivyo , leo tunapaswa kufurahia na kulipenda kanisa kama ni mahali pa kukutana na Bwana Mfufuka , aliyewatuma mitume wake , kuwaalika wote waliokutana nao kuufahamu ukweli wa Injili , furaha ya imani na ahadi ya maisha ya Milele, iliyotangazwa na Mitume. 

JUMAPILI DOMINIKA YA 29 ya Mwaka C. Tarehe 20/10/2013

JUMAPILI DOMINIKA YA 29 ya Mwaka C.
      RATIBA ZA IBADA 
KIGANGO CHA MH. ISIDORI BAKANJA- BOKO.
MISA YA KWANZA 12:15-2:00 ASUBUHI
MISA YA PILI     SAA 2:00-4:00 ASUBUHI
MISA YA TATU SAA 4:00-5:30 ASUBUHI
KIGANGO CHA MT. FRANCIS WA ASIZ-MBWENI 
MISA YA KWANZA SAA 1:10-3:00 ASUBUHI
MISA YA PILI SAA 3:00-4:30 ASUBUHI

KIGANGO CHA MT. RAFAEL-MBWENI MALINDI
SAA 1:00-3:00 ASUBUHI.
MISA YA PILI SAA 3:00-5:00

KIGANGO CHA ANTHONY WA PADUA-MBWENI TETA
MISA NI SAA 3:00-5:00.


MASOMO 

 Somo 1:Kut.17:8-13
Wakati huo Waameleki walitokea, wakapigana na Israel huko Refidimu. Musa akamwambia Yoshua, Tuchagulie watu, ukatoke upigane na waameleki; kesho nitasimama juu ya kilele kile, na ile fimbo ya Mungu nitakuwa nayo mkononi mwangu. Basi Yoshua akafanya kama Musa alivyomwambia, akapigana na Amaleki; na Musa na Haruni na Huri wakapanda juu ya kile kilima. Ikiwa Musa alipoinua mkono wake, Israel walishinda; na aliposhusha mkono wake, Amaleki walishinda. lakini mikono ya Musa ilikuwa mizito; bali wakatwa jiwe, wakaliweka chini yake akalikalia. Haruni na Huri wakaitegemeza mikono yake, mmoja upande huu na mmoja upande huu; mikono yake ikathibitika hata jua lilipokuchwa. Yoshua akamwaangamizaAmaleki na watu wake kwa ukali wa upanga.

SOMO 2: 2Tim.3:14 - 4:2
Wewe ukae katika mambo yale uliyofundishwa na kuhakikishwa, kwa maana unajua ni akina nani ambao ulijifunza kwao; na ya kuwa tangu utoto umeyajua maandiko matakatifu, ambayo yanaweza kukuhekimisha hata upate wokovu kwa Imani iliyo katika Kristo Yesu. kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema. nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, atakayehukumu waliohai na waliokufa; kwa kufunuliwa kwake na kwa ufalme wake; lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho.

INJILI. :Lk.18:1-8
Yesu aliwaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu siku zote, wala msikate tamaa. Akasema, palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu. Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea endea , akisema, nipatie haki na adui wangu. Naye kwa muda alikata tamaa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu, lakini kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima. Bwana akasema, sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu. Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao? Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?
             
  1.  Maandalizi ya Dekania Cup yanaendelea kwa upande wa tImu ya Mpira wa  Pete jumamosi tarehe 19 wanacheza kutauta mshindi wa tatu dhidi ya bunju.


  1. tunawakumbusha vijana wote kuendelea kulipa ada kwa maendeleo ya chama chetu..... mapendo sana malipo kwa njia ya benk kwa jina na number hii :viwawa parokia ya boko account no 01524526820100 crdb bank tegeta branch
JIANDAE NA ZIARA YA UINJILISHAJI MWAKA 2014.....................

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR