Friday, October 4, 2013

vijana washiriki adhimisho la Siku ya Kimataifa ya Amani



Mamia ya watu vijana, Jumatano walikusanyika katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya amani , chini ya Mada: Elimu kwa ajili ya amani . Tarehe rasmi ya adhimisho hili kwa kila mwaka, ni 21 Septemba , na iliwekwa kwa lengo la kupata muda wa kutafakari kwa makini zaidi, manufaa ya amani badala ya migongano, na hivyo kutoa wito kwa jumuiya na jamii nzima duniani ipende amani na kusitisha ghasia zote.

Vijana waliokusanyika katika makao Makuu ya Umoja wa Mataifa walipata muda wa kushirikishana uzoefu katika kazi kwa ajili ya amani katika jumuiya zao duniani kote.

Sherehe hizi zilizinduliwa kwa mlio wa maalum wa Kengele, iliyopigwa katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa kuashiria amani, na pia kama sehemu ya kuwakumbuka waliouawa na walio nusurika katika vita, pamoja na kuchagiza uwekaji chini silaha pale ambako vita vinaendelea. Ni mlio wa kengele ya amani, na wimbo wa amani.

Redio Umoja wa Mataifa imeripoti kwamba, wakati wa tukio hilo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, alisema, siku hii ni siku ya kutafakari na kusisitiza imani katika maisha yasiyoandamana na ghasia, pamoja na kutoa wito wa kusitisha mapigano kote duniani. Akitrejea kauli mbiu ya mwaka huu kama "Elimu kwa ajili ya amani", Bwana Ban amesema elimu ndiyo silaha yenye nguvu zaidi. Na kila mtoto anastahili kupata elimu, ili ajifunze maadili yatakayokuza jamii zenye kuvumiliana na kuheshimu tofauti za watu wengine wanaoishi nao.

Katika Siku hii ya kimataifa ya amani, tuahidi kufundisha watoto wetu thamani ya kuvumiliana na kuheshimiana. Tukiipa elimu kipaumbele, tunaweza kupunguza umaskini na kutokomeza njaa, ili tuweze kujenga jamii zenye nguvu na bora zaidi kwa ajili ya wote.

Naye rais mpya wa Baraza Kuu John William Ashe, amesema hafla ya kupiga kengele ya amani ni muhimu kukumbusha majukumu ya Umoja wa Mataifa katika kuhakikisha ulimwengu wenye amani zaidi.

Tunapoisikia kengele hii ikilia, tukumbuke kuwa ni Umoja wetu wa Mataifa ndio ulioiweka siku hii ya kimataifa ya amani, katika kuzifanya nchi zote wanachama kuitambua na kutafakari kuhusu umuhimu wa amani, katika ulimwengu ambao umejaa mifano ya kila siku ya umwagaji damu, ghasia na vita. Ni siku ambayo tunajitoa kushirikiana kuendeleza amani.

TAREHE 4/10 SIKU YA MT. FRANCISKO

Papa awasili Assis.


Baba Mtakatifu Ijumaa hii (04/10/2013), amefanya ziara ya kichungaji kwenye mji wa asili wa Mtakatifu Francisko wa Assisi na kuadhimisha pamoja na maelfu ya waumini na wahujaji maadhimisho ya Sikukuu ya Mtakatifu Francisko inayosheherekewa kila tarehe nne ya mwezi Oktoba. Itakumbukwa kwamba Mtakatifu Francisko wa Assisi ndiye mtakatifu Msimamizi wa Italia.

Alipowasili mjini Assisi Papa alipokelewa na rais wa Senate ya Italia, mh. Pietro Grasso, na rais wa kanda ya Umbria, Mh. Catiuscia Marini. Alishuka kwenye ndege akiwa amejibebea begi lake leusi mkononi huku maelfu ya waumini na mahujaji wakipiga kelele za furaha wakisema: Viva il Papa. Naye Papa alirudisha salamu hizo kwa tabasamu na ishara za kuwabariki wote waliokuwa wakimkaribisha.

Wengi wa wahujaji wamesafiri kutoka mbali na wamekesha usiku kucha nje ya viwanja vya kanisa kuu la Mtakatifu Francisko na madhabahu ya Mtakatifu Maria, malkia wa Malaika, huku wakingojea kwa hamu na gamu kukutana naye Papa Francisko.

Baada ya salamu hizo Papa alielekea moja kwa moja kwa miguu kwenye kituo cha watoto na vijana walemavu cha Seraphicum ambako aliongea nao huku akiwakumbatia na kuwabusu kwa mapendo na maneno ya kuwatia moyo. Kwenye kuta za nje za kituo hicho cha watoto kulikuwa kumeandikwa maneno haya: “Papa Francisko, myenyekevu kati ya wanyenyekevu” na “Unamgusa Mungu aliye Hai, unaishi ukiabudu”

Kituo cha Seraphicum kilianzishwa na mwenyeheri Ludovik da Casoria mnamo tarehe 17 mwezi Septemba mwaka 1871, kama kumbukumbu ya makovu au stigmata ambayo Yesu alimshirikisha mtumishi wake Francis wa Assisi, kama ishara ya mateso ya Yesu ambayo wanashirikishwa pia walemavu. Kwa sasa hivi kituo hicho kina jumla ya walemavu 60 wanaotunzwa humo.

Alipowasili kwenye kituo cha Seraphicum Baba Mtakatifu alipokelewa na mwakilishi wake nchini Italia, Mons. Adriano Bernadini, na Askofu wa Assisi, Mons. Domenico Sorrentino. Papa aliandamana na Markadinali nane, washauri wake aliowateua hivi karibuni kwa ajili ya kutekeleza marekebisho ndani ya utendaji kazi wa vatikani, na kwa ajili ya kuboresha uongozi wa Kanisa pote ulimwenguni.

Papa alipokuwa anasalimiana na watoto na vijana wa Seraphicum wauguzi wengine walibeba juu kwa juu bango lenye maandishi: Francisko, jenga nyumba yangu- maneno ambayo yanasemekana kusemwa na Yesu mwenyewe kama mwaliko kwa Mtakatifu Francisko, aliyeacha vyote na kumfuata Kristo baada ya kuyasikia, alipokuwa akisali kwenye kanisa la Mtakatifu Dominiko, zaidi ya miaka mia nane iliyopita.

MSIMAMO WA DEKANIA CUP" GASPER"13








MSIMAMO WA LIGI YA DEKANIA GASPER 13





PAROKO CUP 13 :KUNDI A
TIMUMechiImeshindaImefungwaSare Magoliwaliofungwapoint

Damu Takatifu Tegeta21015 2 4
St.Gasper Mbezi21 0120 4
St. Dominico Mbezi201124 1
St.Nicolaus Kunduchi201103 1


MSIMAMO WA LIGI YA DEKANIA GASPER 13





PAROKO CUP 13 :KUNDI
TIMUMechiImeshindaImefungwaSare Magoliwaliofungwapoint

BMMK - Bunju110042 3
St. Andrew Bahari Beach110010 3
Mh. Isidori -Boko202025 0

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR