Tuesday, March 22, 2016

MJUE TEMBO (NDOVU) MNYAMA MKUBWA

Ndovu au TemboNdovu au tembo ni aina za wanyama wenye umbo kubwa kupita wanyamapori wote. Watoto wake wakizaliwa hufikia kg 100 na ndovu mzima huwa na uzito wa tani 2 hadi 5; kimo ni hadi m 4.
Kibiolojia ni mamalia. Sehemu ya pekee mwilini ni mwiro ambao hali halisi ni pua la tembo lililorefuka na kufanya kazi pia kama mkono wake yaani kwa kutumia mwiro ndovu hushika vitu na kufanya utafiti kwa kugusagusa.

Pembe-jino zake zinatafutwa sana kama mapambo na biashara ya pembe za ndovu imeshakuwa hatari kabisa kwa ndovu wote kwa sababu wanawindwa mno. Hivyo kwa mapatano ya kimataifa biahsara ya pembe hizi imepigwa marufuku.







Kwa jumla kuna spishi tatu za Tembo ambao wanafanana lakini hawazai pamoja. Tembo-nyika ambao ni wakubwa kuliko wengine.
Tembo wa Asia ni wadogo kwa Tembo Nyika lakini anazoea wanadamu kwa hiyo katika nchi kama Uhindi au Uthai hutumiwa kama mnyama wa kazi akibeba mizigo au watu. Zamani spishi hii ilitumiwa hata vitani. Kwa mfano jemadari Hanibal wa Karthago alishambulia Dola la Roma kwa msaada wa Tembo wa kijeshi waliovuka milima ya Alpi.
Tembo-misitu, Tembo huyu asili yake ni  Afrika lakini wataalamu wamethibitisha ni spishi tofauti. Hufikia kimo cha mita 2 tu anaishi hasa katika misitu ya Kongo.

Spishi za Afrika

  • Loxodonta africana, Ndovu-nyika (African Bush Elephant)
  • Loxodonta cyclotis, Ndovu-misitu (African Forest Elephant)

Spishi ya Asia

  • Elephas maximus, Ndovu wa Asia (Asian Elephant)
  •   Tembo hula  majani. Kwa chakula hiki ambacho ni kigumu hutegemea meno yao.
    itaendelea

WAJUE MAMEYA WA MANISPAA ZA ILALA, KINONDONI NA TEMEKE JIJI LA DAR ES SALAAM





Meya
                      HON. CHARLES KUYEKO
                    ILALA MUNICIPAL
                               MAYOR


Image result for meya wa temeke 2016
 HON. CHAUREMBO ABDALAH JAFAR
                TEMEKE MUNICIPAL
                          MAYOR

MEYA MPYA WA JIJI LA DAR ES SALAAM NI MH. ISAYA CHACHA

  Kaimu Mkurugenzi Jiji la Dar es Salaam Bi. Sara Yohana amemtanganza Mhe. Isaya Chacha Diwani wa Kata ya Vijibweni (CHADEMA) kutoka Manispaa ya Temeke kuwa Meya Mpya wa Jiji hilo.
 
Kaimu Mkurugenzi huyo alimtangaza Isaya kuwa mshindi mara baada ya uchaguzi huo kufanyika leo  jijini Dar es Salaam ambapo mshindi alipata kwa kura 84 dhidi ya mgombea kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bw.Yenga Yusuph ambaye alipata kura 67 wakati kura 7 ziliharibika katika uchaguzi huo.

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR