Wednesday, March 20, 2013

IBADA YA MATAWI

Katika mwaka wa Kanisa wa madhehebu mbalimbali ya Ukristo, Jumapili ya matawi inaadhimishwa jinsi Yesu Kristo alivyoingia Yerusalemu ili kufa na kufufuka kwa wokovu wa binadamu wote. Siku hiyo alishangiliwa na umati kwa kutumia matawi, ndiyo asili ya jina.
Ndiyo mwanzo wa Juma kuu linaloadhimisha matukio makuu ya historia ya wokovu kadiri ya imani ya Wakristo.
Tangu mwaka 1985 siku hiyo Kanisa Katoliki linaadhimisha pia "Siku ya kimataifa ya vijana"

Kulikuwa Jumapili ya Matawi hasubihi, na kijana wa familia moja alikuwa amepatwa na mafua, na hivyo hakuweza kwenda Kanisani pamoja na wana familia wengine. Aliachwa nyumbani. Basi wana familia waliporuri kutoka sherehe za Jumapili walifika nyumbani na matawi yao. Yule kijana akawauliza umaana wa matawi yale. Mama akamjibu, “Umati ulimshangia Yesu akipita kwa kuinua ya matawi juu. Basi yule kijana akajibu kwa mshangao, Jumapili ya pekee ambao sikuweza kwenda Kanisani, na Yesu anakuja binafsi!” Kwa sherehe za Jumapili hii ya Matawi, Kanisa huadhimisha ukubusho wa Bwana Yesu wakati aliingia Yerusalemu mahali atakapokamilisha fumbo la Pasaka, yaani, mateso, kufa na kufufuka kwake. Kwa maandamano ya matawi Jumapili hii, tunaanza rasmi Wiki Takatifu tukielekea Pasaka. Maandamano yenyewe humshangilia Yesu, ambaye hivi punde kwa kifo na ufufuko wake, atarudi kwenye utukufu wa Baba. Jumapili ya Matawi ina pande mbili, yaani pande moja ya furaha na nyingine ya mateso. Tunaona kwanza Yesu akiingia Yerusalemu kwa shangwe na furaha, na pia hivi punde atateswa. Yule anayeingia Yerusalemu kwa shangwe, ndiye pia atayehukumiwa na umati afe msalabani kwa ajili ya dhambi zetu. Hivyo Yesu ndiye mfano maalum wa kutuonyesha jinsi safari yetu ya imani itakapokuwa hapo mwisho, yaani kujinyenyekesha na kuteswa hadi kukubali kufa msalabani, ili Mungu atufufue siku ya mwisho.

Kwenye Injili juu ya Mateso ya Bwana iliyoandikwa na Mtk. Luka tunashirikishwa kwenye mchezo wa kuwiga juu wa ukombozi wetu, lakini mchezo wenyewe ni wa hali ya juu sana. Yesu ndiye anayechukua mahali pa katikati kwenye mchezo huu. Mtk. Luka anatuonyesha kwamba Yesu anateseka na kufa asipokuwa na kosa hata moja (Lk 23:4, 14-15, 22). Yesu anateswa na kuuawa na hadui zake ambao sio Warumi, lakini Mayahudi wenzake (Lk 22: 3,31,53). Maandishi ya Luka juu ya mateso na kufa kwa Yesu umaana wake hasa ni Habari Njema juu ya huruma na usamaho wa Mungu Baba. Hivyo Injili yenyewe ni kama mujiza wa vile Baba huendelea kuonyesha huruma wake kwa wote. Hivyo Yesu anaponya sikio la askari aliyekatwa na Petro; Yesu anamwangalia Petro kwa huruma wakati alimkana mara tatu; na Yesu anamuhurumia mwizi aliyekuwa amehukumiwa kufa msalabani. Kwenye mateso yake huko gethsemani, wakati alikuwa akichekelewa na umati na mateso yake yote msalabani, Yesu ni ishara ya Mungu baina ya watu wake; na pia kama chombo kinachoonyesha upendo na huruma wa Mungu. Kuna ujumbe gani tungepeleka nyumbani Jumapili hii? 1) Tunapotafakari juu ya mateso na kifo cha Bwana, tuyaone pia kwenye maelfu ya watu wetu barani Afrika wanaoteswa na kufa bila kosa lolote. Pia tukumbuke mateso yetu binafsi. 2) Kwenye mateso ya Yesu tunaonyeshwa kwamba Mungu katika upendo na huruma wake hawezi kutuacha peke. Pia tunagundua kwamba hapo mwisho, mateso yatageuzwa kuwa furaha, na kifo kuwa maisha mapya. 3) Tukumbuke kwamba ni kwa ajili ya dhambi zetu Yesu anahukumiwa kufa msalabani, na ni kwa ajili ya upenda na huruma wa Mungu tunapata maondoleo ya dhambi tukitubu na kuungama dhambi zetu.


 ABEL R. REGINALD.

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR