Showing posts with label tafakari nasi... Show all posts
Showing posts with label tafakari nasi... Show all posts

Wednesday, November 7, 2012

Tafakari Nasi.....


Vijana Wakatoliki inatubidi tuisha kwa tafakari na mifano ya watakatifu wakubwa kama vile  Francis wa Assisi ambao Mungu
aliwatukuza kutokana na bidii yao ya kuwahubiria wakristo ili waishi vema ujumbe wa Injili.
 “Tuirejee Injili, la sivyo Kristo hataishi miongoni mwetu”  Kuirejea Injili ni
kumkubali Yesu wa  Nazareti kufanya makao mwetu kwa kuishi maisha ya umaskini wa roho,
kujitoa kwa wote huku tukijiweka katika daraja ya chini, kujitolea kwa ajili ya wenzetu, n.k.
Kama ilivyosalamu yetu..ya mapendo..,kijana akijawa na mapendo ya dhati kwa Yesu, alijitoa kikamilifu kuishi Injili, basi yeye atakuwa ni kijana wamfano na kuwarekibisha wengine,
Kurejea kwenye Injili ni jambo la msingi kwa maisha ya kikristo, kadhalika kuna mambo ambayo
nayo ni muhimu sana katika dunia yetu ya leo.

Je Ujana wako unauishi kwa  kukosa imani. ni  dhahiri kuwa wapo vijana wengi waliopoteza imana na mwelekeo wa maisha, je mkiwa kama Kijana Mkatoliki umeyakabidhi maisha yako kwa huyu Yesu wa Nazaerti? 
Maisha yetu yote  ni ya hangaiko kwa ajili ya Yesu wa Nazareti. hapo ndipo utaweza
kutambua mapenzi ya Mungu kupitia matukio mbalimbali. Katika ulimwengu huu wenye
kubadilika kwa kasi, Kijana mkatoliki unaweza kusaidia katika kukabiliana na mabadiliko haya ili
kukidhi mahitaji yetu ya kiimani.

Jiulize Maswali yafuatayo kisha tuandikie comment yako unaweza pia kutuandika katika E mail yetu viwawaboko@yahoo.com

1) Je nimeweza kubaini nini kutokana na tafakari yangu juu ya maisha ya Utume

2) Ni nini hasa ambacho naweza kuiga ambacho kinaendana kabisa na maisha yangu,
  uhusiano wangu na Mungu na wa watu wengine?
3)Ni kwa namna gani maisha na ujumbe wa Watakatifu unatusaidia  vilivyo kumfuasa
Kristo?

4)Napata ujumbe gani? Huo ujumbe nitauishi vipi katika maisha yangu ya kila siku?

“Endapo punje ya ngano haitadondoka ardhini na kufa, haitazaa, lakini ikifa, huzaa sana
                                     matunda” Yn. 12: 24

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR