Wednesday, January 28, 2015

UJUMBE WA KWARESIMA MWAKA HUU 2015: IMARISHENI MIOYO YENU!

Kanisa litakianza kipindi cha Kwaresima hapo tarehe 18 Februari 2015 kwa kupakwa majivu, mwaliko wa kutubu na kumwongokea Mwenyezi Mungu. Ujumbe wa Baba Mtakatifu kwa kipindi cha Kwaresima kwa mwaka 2015 unaongozwa na kauli mbiu "Imarisheni mioyo yenu" kwa kutambua kwamba, kila mtu anapendwa na Mwenyezi Mungu na anamfahamu kila mtu kwa jina na hata pale mwanadamu anapokengeuka, Mungu bado anamtafuta.

Dhamana na nafasi ya Baba kwenye Familia

Baba Mtakatifu Francisko, Jumatano tarehe 28 Januari 2015 ameendelea na Katekesi yake kuhusu Familia, kwa kuangalia: utu, dhamana na nafasi ya Baba wa familia, jina ambalo Wakristo wamefundishwa na Yesu mwenyewe kumwita Mwenyezi Mungu; jina lenye utajiri mkubwa wa mahusiano katika jamii.

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR