Friday, August 16, 2013

Ungana nasi Kuanzia kesho hadi Jumapili Parokiani Boko

kesho kuanzia saa mbili asubuhi Viwawa wa Parokia ya Boko wataanza sherehe za jubile ya miaka kumi ya Parokia yetu, Sherehe hizi zitaanza kwa semina ambazo zitatolewa na Fratel na Padre Ngowi mada zitakuwa ni Jitambue Kijana mkatoliki na Makuzi ya Vijana pia kutakuwa na mechi kali ya fainal ya Ligi ya Paroko cup ambayo itatanguliwa na upigiji wa Penalt ambao utafanywa na Baba Paroko, Paroko Msaidi na Padre Mlezi wa Viwawa, Pia wenyeviti wote wa jumuiya za Parokia yetu watapiga Penalt.

usiku vijana watapata nafasi ya kuonyesha vipaji vyao kwa show mbali mbali na tutapata muda wa kupreview ziara ya mbulu na kuangalia yale matukio muhimu ya kukumbukwa kwenye tamasha la mwaka jana \.

yote ni kwa upendo na Mungu amutuchagua sisi tuwe mfano basi tuwatumikie mwengine na kuwaonyesha njia.................karibuni sana

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR