Thursday, October 16, 2014

Je! unataka kushiriki kwenye mafunzo ya ujasiriamali

VIJANA WALIOPO TAYARI KUSHIRIKI KATIKA  SEMINA YA UJASIRIA MALI NA KUPATA MAFUNZO KWA VIKUNDI WAANZE KUJIANDIKISHA.
Kulekea kwenye Kongamano la Vijana wa Parokia ya Bunju na Boko, Tunawakaribisha vijana wote waliopo tayari kwenye ujasiriamali na wale ambao wanataka kuanza kufanya ujasiria mali, Mafunzo haya yataanza sanjari na semina ya mwaka wa familia, ambapo vijana watapata kujua na kujifunza mambo mbali mbali kuhusiana na familia, lakini kubwa zaidi ni mafunzo au elimu ya ujasiriamali itakayofundishwa na Ndugu, Dhino, tukiwa na malengo yakuwabanua vijana mawazo, na kuwajengea mbinu na misingi mizuri katika ujasiriamali, na baada ya kongamano hilo tunatarajia kuunda vikundi vidogo vidogo vya ujasiriamali ambavyo vitaendelea kupata mafunzo haya na kuanzia miradi mbali mbali.
Ukiwa wewe ni mjasiriamali au unaelimu ya ujasiriamali basi tunaomba uwasiliane nasi kwa anuani pepe yetu: abyshine3@gmail.com au piga simu 0713 900 905 tuweze kufanya maandalizi ya awali, Mungu azidi kuwabariki

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR