Showing posts with label Mosomo ya jumapili ya nne ya Kwaresima. Show all posts
Showing posts with label Mosomo ya jumapili ya nne ya Kwaresima. Show all posts

Sunday, March 15, 2015

Dominika ya 4 ya Kwaresima tarehe 15/03/2013(Masomo ya Jumapili)

15

 Marchi
 Jumapili ya 4 ya Kwaresima Masomo ya Mwaka "B".
Mwanzo

Furahi, Jerusalemu, mshangilie ninyi nyote mmpendao; furahini, ninyi nyote mliao kwa ajili yake, mpate kunyonya, na kushibishwa kwa maziwa na faraja.
SOMO  1: 2Nya. 36:14- 16, 19-23
Somo katika kitabu cha pili cha Mambo ya Nyakati.
Wakuu wote wa makuhani, na watu,wakakosa mno sawasawa na machukizo yote ya mataifa; wakainajisi nyumba ya Bwana aliyoitakasa katika Yerusalemu. Naye Bwana, Mungu wa baba zao akatuma kwao kwa mikono wajumbe wake, akiondoka mapema, na kutuma; kwa sababu aliwahurumia watu wake, na makao yake; lakini walidhiaki wajumbe wa Mungu, na kuyadharau maneno yake; na kuwacheka manabii wake, hata alipozidi ghadhabu ya Bwana juu ya watu wake, hata kusiwe na kuponya.
wakaiteketeza nymba ya Mungu wakaubomoa ukuta wa Yerusalemu, wakayateketeza kwa moto majumba yake yote, wakaviharibu vyombo vyake vyote vya thamani. Na wale waliookoka na upanga akawachukua mpaka Babeli; wakamtumikia yeye na wanawe hata kulipoingia milki ya Uajemi; ili kulitimiza neno la Bwana kwa kinywa cha Yeremia, hata nchi itakapofurahia sabato zake; kwa maana siku zote ilipokaa ikiwa ilishika sabato, kutimiza miaka sabini.
Ikiwa katika mwaka wa kwanza wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, ili kwamba neno la Bwana alilolisema kwa kinywa cha Yeremia lipate kutimizwa. Bwana akamwamsha roho yake Koreshi, mfalme wa Uajemi, hata akapiga mbiu katika ufalme wake wote, akaiandika pia akisema. Koreshi, mfalme wa Uajemi asema hivi; Bwana, Mungu wa mbinguni, amenipa falme zote za dunia; naye ameniagiza nimjengee nyumba katika Yerusalemu, ulioko Yuda. Basi kila mtu katika nyinyi nyote mlio watu wake, Bwana, Mungu wake, na awe pamoja naye, na akwee.

WIMBO WA KATIKATI. 
Zab. 19:7-10. 
Kiitikio. Ulimi wangu na ugandamane 
            Na kaakaa la kichwa changu, nisipokumbuka..

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR