Wednesday, March 23, 2016

KWANINI WAZEE WA ZAMANI WALIISHI MIAKA MINGI: YAJUE MADHARA YA MAFUTA YAKUPIKIA

CHAKULA ni moja ya mahitaji muhimu katika mwili wa mwanadamu, kwa ajili ya kuupatia nguvu, kulinda na kujenga mwili. Kwa kawaida, vyakula vingi anavyokula mwanadamu vinaandaliwa kwa kutumia mafuta ya kupikia, hali inayosababisha wapishi wengi kushindwa kuandaa vyakula kama hawana mafuta ya kupikia.
Mafuta ya kupikia yana faida na madhara kulingana na aina na wingi wa mafuta. Hata hivyo, kwa kawaida, mafuta yasiyokuwa na viwango vya ubora hupatikana kwa bei nafuu, na ndiyo hayo ambayo hupendwa kutumiwa na familia nyingi kutokana na uwezo wa kipato.
Kutokana na hali ngumu ya maisha inayozikabili familia nyingi nchini, wengi wetu hatujali aina ya vyakula tulavyo, wala vyakula tunavyonunua vina viambato gani na kiasi gani. Wengi tunaangalia gharama na upatikanaji wa bidhaa, basi.
Ni mafuta gani bora yanayofaa kupikia chakula?
Ili kuwa makini na afya zetu, ni vizuri kutafuta na kuchagua mafuta ya kupikia kwa umakini na busara zaidi. Kama nilivyodokeza hapo juu na katika machapisho mengine ya FikraPevu kwamba ulaji wa mafuta una faida na hasara zake. Moja ya madhara ya ulaji wa mafuta bila uangalifu, ni kutofanya kazi vizuri kwa ubongo pamoja na kuziba mishipa ya damu.
Katika soko la mafuta ya kupikia nchini, kuna aina nyingi tu za mafuta. Hata hivyo, kisayansi mafuta yote hayo ymegawanyika katika sehemu kuu mbili tu. Mosi, ni mafuta ya kupikia yanayotokana na asili ya wanyama, na pili, ni mafuta yanayotokana na mimea ya asili.
Mafuta yenye asili ya wanyama
Mafuta yenye asili ya wanyama, kwa asili, huwa yameganda katika joto la kawaida. Mafuta haya ni pamoja na anayotokana na nyama iliyonona na nyama ya nundu. Mafuta ya samli, siagi, jibini na maziwa yenye mafuta.
Aina hii ya mafuta ina athari kwa mtumiaji, ikiwa ni pamoja na kupata magonjwa ya moyo, kuwa na uzito uliozidi na unene uliokithiri, huweza kusababisha ugonjwa wa kisukari na kadhalika. Kwa hiyo, ni muhimu kiafya, kila binadamu akajitahidi kupunguza utumiaji wa aina hii ya mafuta yenye asili ya wanyama.
Mafuta yatokanayo na mimea
Mafuta mengi yatokanayo na mimea huwa hayagandi na muda wote yanakuwa katika hali ya kimiminika katika joto la kawaida. Kwa kawaida, mafuta haya haya, tofauti nay ale ya wanyama, yana ‘lehemu.’
Aina ya mafuta aina hii yanayotokana na mimea ya asili, ni pamoja na mafuta ya soya, ufuta, karanga, alizeti, mawese, pamba, nazi, korosho, kweme na mbegu za maboga.
Katika afya ya sayansi, mafuta haya ndiyo bora zaidi kwa kupikia kwa sababu husaidia kuboresha afya ya mwili. Hata hivyo, pamoja na kuwa mafuta bora zaidi, inashauriwa kuyatumia kwa kiasi kidogo.
‘Lehemu’ ni nini na ina madhara gani mwilini?
‘Lehemu’ ni moja ya kiambata kinachopatikana kwenye mafuta ya kupikia, ambacho kitaalamu inajulikana kwa jina la ‘Cholesterol.’ Kiambata hiki hupatikana kwa wingi kwenye mafuta ya kupikia yanayotokana na asili ya wanyama.
Kiambata hiki, pamoja na kusababisha madhara makubwa ya kiafya, lakini kinahitajika mwilini kwa kiasi kidogo. Kwa kawaida kiambata hiki kinatakiwa kiwe chini ya 200mg/dl. Hata hivyo, ni vigumu kwa binadamu kujitambua ni kiasi gani cha kiambata hiki kilichoko mwilini mwake hadi pale atakapoonana na Daktari na kupima.
Moja ya madhara ya kuwa na kiasi kikubwa cha lehemu mwilini, ni kuwa na mkusanyiko wa mafuta katika mishipa ya damu, hali inayoweza kusababisha damu kushindwa kupita kwa urahisi katika mishipa ya mwanadamu.
Hali hiyo ikimpata mwanadamu, huweza kusababisha tatizo la shinikizo kubwa la damu na ugonjwa wa moyo. Hatari nyingine ni mafuta kuziba mishipa midogo ya damu yenye mawasiliano ya moja kwa moja na moyo au ubongo, hali inayoweza kusababisha ugonjwa wa kiharusi pamoja na kifo.
Nini kifanyike ili kujilinda na athari hizo za kiafya zinazosababishwa na lehemu?
Kwanza kabisa punguza matumizi ya nyama, mayai, jibini na maziwa yasiyotolewa mafuta kabla ya kutumiwa. Jiepushe kula maini, moyo, firigisi na figo. Kama mtu anaiishi katika mazingira ambayo nyama nyekundu kama vile ya ng'ombe ndiyo mboga kuu, basi mtu huyo anapaswa kuhakikisha kwamba kiasi cha nyama nyekundi kinacholiwa hakizidi nusu kilo kwa wiki.
Ongeza matumizi ya vyakula vyenye makapi-mlo kwa wingi, kama vile nafaka zisizokobolewa kwa mfano unga wa dona, ulezi, uwele, mtama, vyakula vya jamii ya kunde, mbogamboga na matunda. Kwa kawaida vyakula vyenye makapi-mlo kwa wingi, huwa havina mafuta mengi.
Ni muhimu pia kwa binadamu kujiepusha na ulaji wa mafuta yanayotokana na wanyama, kujiepusha na ulaji wa nyama zilizonona na kuwa na mafuta mengi, kuepuka ulaji wa ngozi ya kuku na siagi pia.
Mazoezi ya mwili angalau dakika 30 kila siku, ni muhimu kwa aina yoyote ya ulaji wa mafuta bila kujali kwamba yana asili ya wanyama au mimea. Inahauriwa mazoezi hayo yawe yale ynayomtoa mtu jasho jingi, kama vile kukimbia kila siku umbali fulani wa kilomita.

CHAD VS TANZANIA LEO ANGALIA

Click here kuangalia live

Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) siku ya kesho Jumatano itakuwa na mtihani mwingine mgumu ugenini dhidi ya Chad katika pambano la mzunguko wa tatu hatua ya makundi kuwania tiketi ya kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika-CHAN 2017.
Chad hoping to stun Tanzania N'DjamenaMichezo miwili ya kwanza kwa kikosi cha Stars haikuwa na matokeo mazuri, chini ya kocha aliyepita M-holland, Marti Nooij, Stars ilichapwa 3-0 na Misri, Alexandria, na mechi iliyofuata ambayo ilikuwa ni ya kwanza kwa kocha mzawa, Charles Boniface Mkwassa ilimalizika kwa suluhu dhidi ya Nigeria katika uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
CHAD NI YA 114 KWA UBORA DUNIANI, YA 22 AFRIKA…
Mshindani wa tatu wa Stars ni Chad, taifa ambalo halijawahi kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika. Wakati, Stars ilifuzu kwa fainali za Afrika mwaka 1980 (miaka 36 iliyopita) Chad ni taifa ambalo linajijenga kwa maana ya hawakushiriki mara kadhaa hatua kama hii ya kufuzu kwa sababu ya kuandaa kizazi kipya.
Nimetazama wastani wa umri wa wachezaji wa Chad, kiukweli wanaonekana kupevuka sana kiumri, sijui kimpira watakuwaje. Stars ilijilinda vizuri dhidi ya Misri kwa dakika 60, lakini kufikia dakika ya 69 timu ilikuwa imechapwa magoli 3-0, dhidi ya Nigeria, Mkwassa alijitahidi kuifanya timu ishambulie na kujilinda vizuri.
Achilia mbali bao la kujifunga kwa timu pinzani, bado hakuna mchezaji ye yote yule wa Stars aliyefanikiwa kufunga goli katika michuano hiyo hadi sasa . Lalini kuna mengi yamebadilika katika timu ya Mkwassa kuelekea mchezo wa Jumatano hii.
Mbwana Samatta anashikilia tuzo ya ufungaji bora wa klabu barani Afrika, pia ndiye mshindi wa tuzo nyingine binafsi ya mchezaji bora wa mwaka uliopita Afrika, akiwa tayari amefunga magoli mawili katika michezo minne ya ligi kuu ya Ubelgiji akiwa na klabu ya Genk aliyojiunga nayo mapema mwaka huu akitoka kushinda ubingwa wa Afrika upande wa klabu akiwa na TP Mazembe ya DR Congo.
Samatta anataraji kwa mara nyingine kuongoza safu ya mashambulizi ya Stars, lakini safari hii kwa mara ya kwanza akiwa na beji ya unahodha katika bega lake la kushoto. Wachezaji wengi wa Chad wana umri kati ya miaka 27 hadi 32, bila shaka watakuwa na uzoefu wa kucheza nyumbani katika michezo ya kimataifa.
Kama ilivyokuwa kwa Misri 3-0 Stars, Chad pia waliibana sana Nigeria katika mchezo wao wa kwanza, lakini walijikuta wakipoteza mechi hiyo ya ugenini wakati muda ‘umekwenda,’ walifungwa 2-0. Mechi yao ya pili walicheza nyumbani na Misri, walichapwa 5-1 matokeo ambayo yamewafanya kuwa mkiani mwa kundi wakiwa bila pointi yoyote.
Uwezo wao kimbinu bado uko chini ndiyo maana licha ya kuonekana kujilinda vizuri wakilazimishwa wanakubali kufungwa. Hata Stars hucheza vizuri lakini timu zote zinakutana zikiwa na viwango vya kukaribiana, umakini mdogo, makosa yasiyo na ulazima katika ngome kutaiangusha timu yeyote katika mchezo huu kwa kuwa Chad wana washambuliaji wazoefu wanaocheza nje ya nchi yao.
Nadjim Haroun ndiye kiungo mchezesha timu wa Chad, anacheza timu ya daraja la chini Ubelgiji, huyu ndiye aliyefunga goli lao pekee katika michuano hiyo hadi sasa.
Jinsi ya kupanga mashambulizi na kupiga pasi za mwisho bado ni tatizo kwa Taifa Stars lakini bado kuna nafasi ya washambuliaji wetu kufunga walau magoli mawili katika mchezo huu, ni namna watakavyochezeshwa na kupewa mipira ya mwisho na viungo kutaangaza ubora wao.
Thomas Ulimwengu na mwendo wake wa kasi na nguvu akitokea upande wowote ule, Samatta (binafsi ningependa aanze na nahodha msaidizi, John Bocco) wanaweza kuwafanya walinzi wote wa Chad kuwa na hofu.
Katika ngome, Chad hawana mchezaji wa kulipwa, wengi wanacheza ligi yao ya ndani kwa maana hiyo kwa namna yeyote watapata wakati mgumu kuwazima washambuliaji wetu watatu wafungaji (Tom, Samatta na Bocco)
Tishio kubwa kwa Stars na nafikiri kocha Mkwassa atapaswa kuchanga vizuri karata zake ni katika safu ya kiungo. Marius Mbalam kiungo mchezesha timu ya Belfort ya France National, Azrack Mahamat anayecheza Platanias ya ligi kuu ya Ugiriki, Sanaa Altama wa Petrolut ya ligi kuu ya Romania na Sylvain Idangar wa AS Lyon ya Ufaransa ni viungo muhimili wa mbinu za kocha Mcameroon, Rigoberb Song.
Song, mchezaji wa zamani wa Cameroon na timu nyingi mashuhuri barani Ulaya anaweza kuwapanga viungo watatu kati ya wanne hao. Azrack ana miaka 27, Marius ana miaka 28, Idangar ana miaka 32 na kijana pekee ni Sanaa mwenye miaka 25.
Umri wao umepevuka lakini bado kuna nafasi ya vipaji vya ligi kuu Bara kuchanua katika idara hii kama tu wachezaji wetu vijana kama Himid Mao, Jonas Mkude, Deus Kaseke, Salum Abubakary na wengineo watacheza kwa ari ya kusaka ushindi kama ilivyokuwa dhidi ya Nigeria na Algeria (kufuzu WC) jijini, Dar fs Salaam.
Kukaba, kucheza faulo za kitaalamu, kumiliki mpira, pasi timilifu, kutengeneza nafasi na kupiga pasi za mwisho kutaisaidia sana safu ya mashambulizi, na bila shaka timu itafunga magoli ya kutosha kama viungo watatimiza mambo hayo niliyoyataja.
Ngome ya Stars mara nyingi imekuwa ikiiangusha timu, rejea sare ya ajabu dhidi ya Algeria, Novemba mwaka jana, washambuliaji walifunga magoli mawili maridadi sana lakini safu ya ulinzi ikaruhusu magoli mawili ya kuchukiza sana.
Wengi walichukizwa na mabadiliko ya Mkwassa, kumtoa Mudathir Yahya na kumuingiza Said Ndemla wakati timu ikiongoza 2-0, lakini Mwinyi Hajji alihusika katika goli la kwanza la Algeria kwa kupiga pasi ‘mkaa’, na safu yote ya ulinzi ilihusika katika goli la kusawazisha la Algeria kutokana na umakini wao mdogo, na kujipanga vibaya.
Magoli 8 ya Shomari Kapombe katika VPL msimu huu akicheza katika beki 2, kiwango cha juu cha kupandisha mashambulizi kutoka kwa Mwinyi katika beki 3, uwezo wa kujipanga wa David Mwantika katika beki ya kati, na ukabaji wa nguvu wa Kelvin Yondani katika beki 4, vyote havitakuwa na maana kama timu itafungwa tena magoli ya kizembe.
Nahodha wa Chad, Ezechiel N’Douassel, 27, anayechezea klabu ya Sfaxien ya Tunisia, kijana Rodrigue Ninga, 22 anayekipiga Montpellier ya Ufaransa ni washambuliaji ambao wataitumia nafasi yoyote watakayopewa na walinzi wa Stars.
Washambuliaji hawa wanacheza vizuri mipira ya juu, pia ni wamaliziaji wazuri hivyo kuanzia kwa golikipa, Ally Mustapha hadi kwa walinzi wake watapaswa kucheza na kuondosha vizuri mipira ya juu itakayoelekezwa golini kwao.
Song alikuwa mlinzi mahiri wa kati, wakati Mkwassa alifahamika kama ‘master’ wakati wake wa uchezaji kama kiungo wa dimba la kati. Chad hushambulia ikicheza nyumbani, lakini Stars ni timu isiyo na utamaduni wa kujilinda kokote inapocheza.
Kuwa na Samatta, Tom na Bocco aliye katika kiwango, kunaweza kumkumbusha Song mambo mengi wakati wa uchezaji wake na hivyo kuingiza timu yake katika umbo la kujilinda. Mkwassa angependa washambuliaji wake wachezeshwe kama yeye alivyokuwa akiwachezesha washambuliaji nyakati zake za uchezaji ili kumshinda Song.
Lakini bado pasi za mwisho hakuna katika timu, pasi za namna ile ya umbali mrefu ambayo ilipigwa na kiungo Henry Joseph kwenda kwa mshambulizi Danny Mrwanda, ambaye alifunga mbele ya Song wakati Stars ilipopata goli la kuongoza dhidi ya Cameroon (ugenini, 2009-Kufuzu WC 2010 na CHAN 2010)
Kila la heri Taifa Stars, ushindi una maana kubwa sana kwa kuwa Misri watacheza mara mbili na Nigeria wiki hii, hivyo pointi 6 dhidi ya Chad zinaweza kuifanya Stars kuwa juu ya timu mojawapo kati ya Misri na Nigeria kabla ya kurejeana nazo.














Belgians hunt Islamic State suspect after blasts kill 30 airport


Belgian police are hunting an Islamic State suspect seen with two supposed suicide bombers shortly before they struck Brussels Airport in the first of two attacks that also hit the city's metro, killing at least 30 and wounding over 200.
The blasts on Tuesday claimed by the Syrian-based militants four days after the arrest in Brussels of a prime suspect in November's Paris attacks, sent shockwaves across Europe and around the world, with authorities racing to review security at airports and transit systems, and drawing an outpouring of solidarity.
"We can and we will defeat those who threaten the safety and security of people all around the world," said U.S. President Barack Obama. Donald Trump, the front-runner for the Republican nomination to succeed Obama in November's election, suggested suspects could be tortured to avert such attacks.
Brussels police mounted an operation in the north of the city, turning up another bomb, an Islamic State flag and bomb-making chemicals in an apartment in the borough of Schaerbeek.
Local media said authorities had followed a tip from a taxi driver who believed he may have driven the bombers to the airport.
Investigators said they were focusing on a man in a hat who was caught on CCTV pushing a laden baggage trolley at the airport with two others they believed were the bombers. An unused explosive device was later found at the airport and a man was seen running away from the terminal after the explosions.
Security experts believed the blasts, which killed about 20 on a metro train running through the area that houses European Union institutions, were probably in preparation before Friday's arrest of locally based French national Salah Abdeslam, 26, whom prosecutors accuse of a key role in the Nov. 13 Paris attacks.
He was caught and has been speaking to investigators after a shootout at an apartment in the south of the city a week ago, after which another Islamic State flag and explosives were found. It was unclear whether he had knowledge of the new attack or whether accomplices may have feared police were closing in.
Islamic State said in a statement that "caliphate soldiers, strapped with suicide vests and carrying explosive devices and machineguns" struck Zaventem airport and Maelbeek metro station.
It was not clear, however, that the attackers used vests. The suspects were photographed pushing bags on trolleys, and witnesses said many of the airport dead and wounded were hit mostly in the legs, possibly indicating blasts at floor level.
MAN IN THE HAT
Officials said the final death tolls remained uncertain from the carnage in the morning rush hour, around 8 a.m. (03:00 a.m. EDT) at the airport and shortly after 9 a.m. on the metro.
"A photograph of three male suspects was taken at Zaventem. Two of them seem to have committed suicide attacks. The third, wearing a light-colored jacket and a hat, is actively being sought," prosecutor Frederic Van Leeuw told a news conference.
The two men in dark clothes wore gloves on their left hands only. One security expert speculated they might have concealed detonators. The man in the hat was not wearing

MADHARA YA KUANGALIA VIDEO ZA NGONO(PORNOGRAPH)

Madhara Yanayosababishwa na Ponografia
HABARI ya kila aina kuhusu ngono inapatikana kwa urahisi kupitia televisheni, sinema, video za muziki, na Internet. Je, ni kweli kwamba habari hizo chungu nzima za ponografia hazina madhara, kama watu wengi wanavyotaka tuamini?*
Jinsi Ponografia Inavyowaathiri Watu Wazima
Hata watetezi waseme nini, ponografia inaathiri sana maoni ya watu kuhusu ngono na maadili. Watafiti kwenye Hazina ya Taifa ya Utafiti na Uelimishaji wa Jamii walikata kauli kwamba “kutazama ponografia kunaweza kuwafanya watazamaji wafanye ngono potovu.” Ripoti hiyo inasema “imani ya kwamba wanawake husababisha na hufurahia ubakaji, na kwamba wabakaji ni watu wa kawaida imeenea sana miongoni mwa wanaume wenye zoea la kutazama ponografia.”
Watafiti fulani wanasema kwamba kuzoea kutazama ponografia kunaweza kuathiri uwezo wa kufurahia na kufanya ngono katika ndoa. Dakt. Victor Cline, mtaalamu wa kutibu watu wanaotawaliwa na mambo ya ngono, ametambua kwamba watu wanaotazama ponografia huendelea tu bila kuacha. Mtu anayeanza kutazama ponografia kidogo-kidogo, asipoacha mwishowe anaweza kuwa na zoea la kusoma habari na kutazama picha chafu zaidi za ponografia. Cline anadai kwamba zoea hilo linaweza kuongoza kwenye matendo mapotovu ya ngono. Wanasayansi wanaochunguza tabia za wanadamu wanakubaliana na jambo hilo. Dakt. Cline anaripoti kwamba “upotovu wowote wa ngono unaweza kuanza hivyo . . . na kwamba mtu hawezi kuacha hata akisumbuliwa sana na dhamiri.” Hatimaye, huenda mtu anayetazama ponografia akajaribu kufanya mambo yasiyo ya adili aliyoona, na mara nyingi matokeo huwa mabaya.
Tatizo hilo linaweza kuanza hatua kwa hatua bila kutambuliwa, asema Cline. Aongeza: “Huongezeka na kuenea kama kansa. Kwa kawaida zoea hilo halikomi, wala haliwezi kutatuliwa kwa urahisi. Haishangazi kwamba mara nyingi wanaume waliozoea kutazama ponografia hawakubali kwamba wana tatizo, na ni kawaida kwa wenzi wa ndoa kukosana, nyakati nyingine kutalikiana, na hata mahusiano mengine ya karibu huharibika kwa sababu hiyo.”
Jinsi Vijana Wanavyoathiriwa
Takwimu zinaonyesha kwamba watazamaji wengi wa ponografia ni wavulana wenye umri wa kati ya miaka 12 na 17. Kwa kweli, wengi wao hujifunza masuala ya ngono hasa kupitia ponografia. Hilo lina matokeo mabaya sana. Ripoti moja yasema kwamba “ponografia hazionyeshi kamwe mimba za matineja na magonjwa yanayoambukizwa kingono kama UKIMWI, na hilo hutokeza wazo la uwongo la kwamba mambo yanayoonyeshwa katika ponografia hayana madhara.”
Watafiti fulani husema kwamba kutazama ponografia kunaweza pia kuathiri ukuzi wa kawaida wa ubongo wa mtoto. Dakt. Judith Reisman, mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya Vyombo vya Habari, akata kauli: “Uchunguzi wa athari za sauti na picha za ponografia katika utendaji wa kawaida wa ubongo unaonyesha kwamba kutazama ponografia huathiri kabisa uwezo wa kawaida wa kufikiri. Pia hudhuru ubongo wa watoto unaoathiriwa kwa urahisi kwa sababu hufanya wasione mambo kihalisi na hudhuru afya yao ya kiakili na ya kimwili, na huwazuia kupata furaha.”
Jinsi Mahusiano Yanavyoathiriwa
Ponografia huathiri mitazamo na tabia. Ujumbe wake unavutia hasa kwa sababu si halisi na hivyo unaifanya ionekane kuwa yenye kusisimua zaidi kuliko mambo halisi. (Ona sanduku “Utakubali Ujumbe Gani?”) “Watu wanaotazama ponografia hutarajia mambo yasiyo halisi ambayo huharibu mahusiano,” yasema ripoti moja.
Ponografia inaweza kuwafanya wenzi wa ndoa wakose kuwa wanyofu na wakose kuaminiana, sifa ambazo ni muhimu katika ndoa. Kwa sababu ponografia hutazamwa hasa faraghani, mara nyingi humfanya mtu atumie hila na uwongo. Wenzi wa ndoa huhisi kwamba wamesalitiwa. Hawaelewi kwa nini mwenzi wao havutiwi nao tena.
Madhara ya Kiroho
Ponografia husababisha madhara mabaya ya kiroho. Inaweza kuwa kizuizi kikubwa kwa mtu anayetaka kuwa na uhusiano na Mungu.* Biblia huhusianisha hamu ya ngono na tamaa na ibada ya sanamu. (Wakolosai 3:5) Mtu anayetamani kitu huwa na hamu kubwa sana ya kukipata hivi kwamba kinakuwa jambo kuu maishani mwake kuliko vitu vingine vyote. Kwa kweli, wale ambao wamezoea ponografia hutanguliza tamaa zao za ngono badala ya Mungu. Kwa hiyo wanazifanya kuwa sanamu yao. Amri ya Yehova Mungu inasema: “Usiwe na miungu mingine ila mimi.”—Kutoka 20:3.
Ponografia huharibu mahusiano yenye upendo. Mtume Petro, ambaye alikuwa amefunga ndoa, aliwahimiza waume Wakristo wawaheshimu wake zao. Mungu hatasikiliza sala za mume anayekosa kufanya hivyo. (1 Petro 3:7) Je, mtu anayetazama picha chafu za wanawake faraghani anamheshimu mke wake? Mke angehisije akigundua? Na Mungu ambaye “ataleta hukumuni kila kazi” na ambaye “huzipima roho” angeonaje? (Mhubiri 12:14; Mithali 16:2) Je, mtu anayetazama ponografia anaweza kumtarajia Mungu asikilize sala zake?
Ponografia hukazia kutosheleza tamaa za mtu binafsi kwa vyovyote vile. Kwa hiyo, kutazama ponografia ni kukosa upendo. Hudhoofisha uwezo wa Mkristo wa kudumu akiwa safi kiadili na kuwa mwadilifu mbele za Mungu. “Haya ndiyo mapenzi ya Mungu,” akaandika mtume Paulo, “kwamba mjiepushe na uasherati; kwamba kila mmoja wenu apaswe kujua jinsi ya kupata umiliki wa chombo chake mwenyewe katika utakaso na heshima, si katika hamu yenye tamaa ya ngono . . . , kwamba yeyote asifikie hatua ya kudhuru na kuziingilia haki za ndugu yake.”—1 Wathesalonike 4:3-7.
Ponografia huwatumia vibaya hasa wanawake na watoto. Huwavunjia heshima na pia huwashushia hadhi na kuwanyima haki zao. Yule anayetazama ponografia hushiriki na kuunga mkono matumizi hayo mabaya ya wanawake na watoto. ‘Hata mtu akijiona kuwa mwema kadiri gani,’ wasema watafiti Steven Hill na Nina Silver, ‘anapotazama au kukubali ponografia, anakuwa asiyejali au hata mwenye chuki kuelekea mtu anayedai eti anamjali.’
Kuacha Zoea la Kutazama Ponografia
Vipi ikiwa unapambana na zoea la kutazama ponografia? Je, kuna lolote unaloweza kufanya ili kuacha zoea hilo? Biblia hutoa tumaini! Kabla ya kumjua Kristo, baadhi ya Wakristo wa awali walikuwa waasherati, wazinzi, na wenye pupa. Hata hivyo, Paulo alisema, “lakini mmeoshwa mkawa safi.” Hilo liliwezekanaje? Paulo ajibu: “Mmetakaswa . . . kwa roho ya Mungu wetu.”—1 Wakorintho 6:9-11.
Usipuuze kamwe nguvu za roho takatifu ya Mungu. “Mungu ni mwaminifu,” yasema Biblia, “naye hatawaacha nyinyi mshawishwe kupita vile mwezavyo kuhimili.” Kwa kweli, ataandaa njia ya kutokea. (1 Wakorintho 10:13) Kusali kwa bidii—kumwambia Mungu shida zako daima—kutakuwa na matokeo mazuri. Neno lake hutia moyo hivi: “Umtwike BWANA mzigo wako naye atakutegemeza.”—Zaburi 55:22.
Bila shaka, lazima utende kupatana na sala zako. Unahitaji kuazimia kutoka moyoni kukataa ponografia. Rafiki unayemtumaini au mshiriki wa familia anaweza kukusaidia sana, akikupa utegemezo na kitia-moyo unachohitaji ili kushikamana na azimio lako. (Ona sanduku “Kupata Msaada.”) Kukumbuka kwamba hatua hiyo itampendeza Mungu kwaweza kukusaidia uendelee kushikamana na azimio lako. (Mithali 27:11) Kwa kuongezea, kujua kwamba kutazama ponografia kunamchukiza Mungu kwaweza pia kukuchochea uache zoea hilo. (Mwanzo 6:5, 6) Haitakuwa rahisi, lakini unaweza kufaulu. Unaweza kuacha zoea la ponografia!
Kwa kweli, ni hatari kutazama ponografia. Inadhuru na kuharibu. Inawapotosha wale wanaoitayarisha na pia wale wanaoitazama. Huwashushia heshima wanaume na wanawake, ni hatari kwa watoto, na ni zoea ambalo linapasa kupingwa.

SPIKA WA BUNGE AFANYA MAAMUZI MAPYA YA KUWANGOA


Dar es Salaam. Spika John Ndugai amefanya mabadiliko ya wajumbe 27 wa
Kamati za Kudumu za Bunge yaliyowangoa wenyeviti watano, huku mmoja
akipoteza nafasi yake ya Mwenyekiti wa Bunge.

Hatua hiyo imekuja wakati kukiwa na tuhuma za rushwa dhidi ya wabunge wa
baadhi ya kamati na kusababisha baadhi kujiuzulu ujumbe wakishinikiza
uchunguzi ufanyike ili waliohusika wawekwe hadharani na kuchukuliwa hatua.

Taarifa iliyotolewa na Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliacho cha
Bunge inasema Spika Ndugai amefanya mabadiliko hayo kwa kuzingatia
mahitaji mapya na changamoto zilizojitokeza baada ya kuunda kamati hizo
siku 59 zilizopita.

Waliongolewa uenyekiti ni Richard Ndassa, ambaye alikuwa Kamati ya
Uwekezaji na Mitaji (PIC), Dk Mary Mwanjelwa (Kamati ya Ardhi, Maliasili
na Mazingira), Martha Mlata (Kamati ya Nishati na Madini).

Waliovuliwa umakamu mwenyekiti ni Dk Raphael Chegeni (Kamati ya Huduma
za Maendeleo ya Jamii) na Kangi Lugola (Kamati za Hesabu za Serikali).

Mabadiliko haya yamefanywa chini ya Kanuni ya 116(3) ya Kanuni za
Kudumu za Bunge ambayo inatoa mamlaka ya kuteua wabunge kuunda kamati
mbalimbali za Bunge,” inasema taarifa hiyo.

Kwa kuhamishwa kutoka kamati wanazoziongoza, wabunge hao wamepoteza
nafasi zao za uenyekiti, wakati Mwanjelwa, ambaye alipata nafasi ya
Mwenyekiti wa Bunge kutokana na kuwa mmoja wa wenyeviti wa kamati hizo,
amepoteza wadhifa huo wa kuwa mmoja wa wenyeviti watatu ambao humsaidia
Spika kuongoza shughuli za Bunge.

Sifahamu chochote, alisema Dk Mwanjelwa, mmoja wa wenyeviti watatu wa
Bunge, alipoulizwa na Mwananchi kuhusu mabadiliko hayo.

Ninachoweza kusema uamuzi wa Spika ndiyo wa mwisho, ila sina
ninachofahamu kuhusiana na mabadiliko haya. Yaani ndiyo nimesoma kwenye
mtandao muda si mrefu kabla hamjanitafuta.

Taasisi za Serikali zinazotuhumiwa kutoa fedha kwa wajumbe wa Kamati za
Bunge, ambazo zina jukumu la kuzisimamia, ni Shirika la Nyumba (NHC),
Bima ya Afya (NHIF), Shirika la Umeme (Tanesco) na Mamlaka ya Udhibiti
wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura).

Meneja Mawasiliano na Uhusiano wa Ewura, Titus Kaguo alisema suala la
taasisi yake kutoa rushwa kwa wabunge limewashangaza, na wanasubiri
vyombo vya uchunguzi kutoa matokeo kuhusu tuhuma hizo.

Matokeo ya uchunguzi kuhusu tuhuma hii ndiyo ambayo yanaweza kuanika
bayana kama kweli tunahusika au lah. Ni jambo ambalo hata sisi
limetushangaza, alisema.

Kutokana na mabadiliko hayo, kamati ambazo viongozi wake wameondolewa
zitalazimika kufanya uchaguzi wa viongozi.

Kamati zinazotakiwa kupata wenyeviti wapya ni ya Nishati na Madini,
Uwekezaji wa Mitaji ya Umma na Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii
ambayo itatakiwa kufanya uchaguzi wa mwenyekiti na makamu wake, wakati
zitakazochagua makamu ni ya Hesabu za Serikali ya Mitaa (LAAC) na ya
Huduma na Maendeleo ya Jamii.

Waliohamishwa wazungumza

Akizungumzia suala hilo, Dk Chegeni alisema wajumbe wawili wa kamati
yake, Zitto Kabwe (Kigoma Mjini) na Hussein Bashe (Nzega Mjini),
wamemuandikia Spika barua za kujiondoa kwenye nafasi zao ili kupisha
uchunguzi wa rushwa.

Wajumbe wa kamati wamesikitishwa na taarifa hizi na kwa pamoja tumeamua
kuchukua hatua. Tumemuandikia Spika barua ya kupisha uchunguzi ili
kujiridhisha na madai yaliyobainishwa. Wajumbe wote waliohudhuria kikao
cha leo wamesaini,” alisema Dk Chegeni.

Zitto aliiambia Mwananchi kuwa amemuandikia Spika barua ya kujiondoa,
akitaka uchunguzi ufanyike na atakayehusika achukuliwe hatua kali.

Bashe alithibitisha kujiondoa akitaka uchunguzi ufanyike na watuhumiwa
wote watajwe kwa majina ili hatua zichukuliwe.

Utumishi wangu kwa kamati uko palepale nisingependa kuhamishwa lakini
watuhumiwa wajulikane,” alisema Bashe.

Akizungumzia taarifa zilizochapishwa na gazeti moja jana, Dk Chegeni
alisema: Si kweli. Hata huyo katibu anayeelezwa kutumwa hakuwa nasi
mpaka mwisho wa ziara pale Bima ya Afya. Alitoa udhuru kuwa mwanaye
anaugua na akaruhusiwa kuondoka mapema tu. Leo (Jana) kamati imewauliza
wajumbe na makatibu wote na wamekana kuhusika.

Baada ya kujiridhisha na kutohusika kwa wajumbe wake, Dk Chegeni alisema
kamati imepitisha maazimio matatu, ambayo ni kutaka uchunguzi ufanyike
ili ofisi ya Spika ijiridhishe, watakaobainika wachukuliwe hatua za
kikanuni na kisheria, na gazeti lililoandika habari hiyo lithibitishe
tuhuma hizo na likishindwa liiombe msamaha kamati.

Jana (juzi) nilitumwa na mwenyekiti wangu nihudhurie kikao Spika
kilichokuwa kifanyike saa 5:00 asubuhi, lakini kiliahirishwa. Leo (jana)
hajahudhuria kikao chetu na kanijulisha kuwa anahudhuria kikao hicho
kikichoahirishwa jana (juzi). Sina taarifa za mahojiano na Takukuru,
alisema Lolencia Bukwimba akimzungumzia Ndassa.

Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi alisema hajajiuzului ujumbe wa
kamati kama habari zilivyoenea, lakini yeye pamoja na wajumbe wenzake wa
Kamati ya Huduma za Jamii wamemtaka Spika awaeleze kilichotokea kwa kuwa
ndiye kiongozi wao.

Kwa mfano mimi nijiuzulu nini wakati si mtuhumiwa? alihoji.

Nikijiuzulu, maana yake naacha kazi za kibunge.

Alisema anashangaa habari kama hizo zinatokea wapi wakati hajasikia kama
kuna mbunge yeyote aliyehojiwa dhidi ya tuhuma hizo.

Kuhusu tuhuma za rushwa, Mbilinyi alisema si rahisi kwa kitu hicho
kutokea kwa kuwa wabunge hawawezi kuwatuma makatibu wa kamati kufuata
fedha za rushwa.
Kwa sababu huwa tunawaona kama wapelelezi, hivyo si rahisi mtu
akamuamini kiasi cha kumtuma akamchukulie mzigo, alisema.

Pia alisema kwa wakati huu ambao Bunge ni changa, haiwezi kuwa rahisi
wakakubaliana kuchukua rushwa kwa kuwa bado wabunge hawajafahamiana vizuri.

Mbunge wa Jimbo la Bukene, Selemani Zedi alisema hajapata taarifa rasmi
za kuhamishwa kutoka kamati ya PIC kwenda ya Katiba.

Nitawajibika kwenye kamati nitakayopangwa kwa sababu spika anayo
mamlaka ya kunipanga popote,alisema.

Kuhusu vitendo vya rushwa, alivitaka vyombo husika kufanya uchunguzi ili
atakayebainika kuhusika achukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria.

Mwaka 2012, wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini walituhumiwa kupokea
hongo kutoka kwenye makampuni ya mafuta ili waunge mkono azimio la
kushinikiza aliyekuwa katibu mkuu wa wizara husika, Eliackim Maswi
angolewe.

Wakati huo, Spika Anne Makinda aliahidi kuwapeleka watuhumiwa kwenye
Kamati ya Maadili na Haki za Bunge ili wachunguzwe na kuahidi kuwa
matokeo ya ripoti hiyo angeiwasilisha bungeni.

Siku hiyo, Spika Makinda pia alitangaza kuivunja kamati ya nishati.

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR