Tuesday, June 24, 2014

Majambazi wamua Sister wa Parokia ya Makoka

MTAWA AUAWA DAR ES SALAAM

Mtawa mmoja wa kanisa katoliki aliyefahamika kwa jina moja la sister Kapuli ameuwawa kwa kupigwa risasi kichwani na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi katika eneo la River side Ubungo jijini Dar es Salaam na kutoweka na pochi ya sister huyo inayodaiwa kuwa na fedha ambazo kiasi chake hakikufahmika mara moja.
Sr Kapuli wa parokea ya Makoka jijini Dar es Salaam ameuwawa kwa kupigwa risasi kichwani na watu watatu wanaodaiwa kuwa ni majambazi baada ya kufuatiliwa nyendo zao wakitokea katika benki ya CRDB ambayo tawi lake halikufahamika mara moja wakati akimsubiri Sr Mwenzie aliyeshuka katika gari walilokuwa wamepanda lenye namba za usajili T 213 CJZ Toyota VX kwa ajili ya kwenda kuulizia bidhaa fulani dukani katika eneo hilo la Riverside Ubungo jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa waendesha bajaji bw godfrey severine ambaye amenusurkakatika tukio hilo bada ya bajaji yake kupigwa risasi kadhaa amesema watu hao walifyatua risasi kadhaa zilizosababisha taharuki kwa wananchi ambao walikuwa wakikimbia hovyo na hivyo kupata upenyo wa kutoweka katika eneo hilo.

No comments:

Post a Comment

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR