Saturday, April 4, 2015

Masomo ya Jumapili ya Paska "mwaka B wa Kanisa (Tarehe 05/04/2015)

05

 APRILI
 Heri ya Paska Masomo ya Mwaka "B".

SOMO  1: Mdo. 10:34, 37- 43
Somo katika kitabu cha Matendo ya Mitume.
  Petro akafumbua kinywa chake, akasema, Jambo lile ninyi mmelijua, lilionea katika Uyahudi wote likianzia Galilaya, baada ya ubatizo aliohubiri Yohane; habari za Yesu wa Nazareti, jinsi Mungu alivyomtia mafuta kwa Roho Mtakatifu na nguvu; naye akazunguka huko na huko, akitenda kazi njema na kuponya wote walioonewa na Ibilisi; kwa maana Mungu aikuwa pamoja naye. Nasi tu mashahidi wa mambo yote yaliyotendeka katika nchi ya Wayahudi na katika Yerusalemu; ambaye walimwua wakamtundika mtini. Huyo Mungu alimfufua siku ya tatu, akamjalia kudhihirika, si kwa watu wote, bali kwa mashahidi waliokuwa wamekwisha kuchaguliwa na Mungu, ndiyo sisi, tuliokula na kunywa naye baada ya ufufuka kwake kutoka kwa wafu. akatuagiza tuwahubiri watu na kushuhudia ya kuwa huyu ndiye aliyeamriwa na Mungu awe mhukumu wa wahai na wafu. Huyo manabii wote humshuhudia, ya kwamba kwa jina lake kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi.

WIMBO WA KATIKATI. 
Zab. 118:1-2, 16-17, 22-23. 
1.Aleluya.
            Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema
  kwa maana fadhili zake ni za milele.
           Israeli na aseme sasa,
    Ya kwamba fadhili zake ni za milele.

K. siku hii ndiyo aliyoifanya Bwana, Tutashangilia na kuifurahia.

2. Mkono wa kuume wa Bwana umetukuzwa;
                   Mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu.
     Sitakufa bali nitaishi,
                   Nami nitayasimulia matendo ya Bwana.
(K)
3. Jiwe walilolikataa waashi
                Limekuwa jiwe kuu la Pembeni.
     Neno hili limetoka kwa Bwana,
                Nalo ni ajabu machoni petu (K)

read more....
SOMO  2: Kol. 3:1-4
 Mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu, Kristo aliko, ameketi mkono wa kuume wa Mungu. Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi. Kwa maana mlikufa, na uhai wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu. Kristo atakapofunuliwa, aliye uhai wetu, ndipo na ninyi mtafunuliwa pamoja naye katika utukufu.

  INJILI.Yn. 20:1-9.
Somo katika Injili ilivyoandikwa na Yohane.
  Hata siku ya kwanza ya juma Mariamu Magdalena alikwenda kaburini alfajiri, kungali giza bado; akaliona lile jiwe limeondolewa kaburini. Basi akaenda mbio, akafika kwa Simoni Petro na kwa yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, akawaambia, wamemwondoa Bwana kaburuni, wala hatujui walipomweka. Basi Petro akatoka, na yule mwanafunzi mwingine , wakashika njia kwenda kaburini wakaenda mbio wote wawili; na yule mwanafunzi wengine akaenda mbio upesi kuliko Petro, akawa wa kwanza wa kufika kaburini. Akainama na kuchungulia, akaviona vitambaa vya sanda vimelala; lakini hakuingia. Basi akaja Simoni Petro akimfuata, akaingia ndani ya kaburi; akavitazama vitambaa vilivyolala; ile leso iliyokuwako kichwani pake; haikulala pamoja na vitambaa, bali imezogwazogwa mbali mahali pa peke yake. Basi ndipo alipoingia naye yule mwanafunzi mwingine aliyekuwa wa kwanza wa kufika kaburini, akaona na kuamini. kwa maana hawajalifahamu bado andiko, ya kwamba imempasa kufufuka  .

No comments:

Post a Comment

NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR