Monday, February 24, 2014

Waraka kuhusu Elimu Katoliki wazinduliwa mjini Vatican



Majiundo ya majadiliano ya kitamaduni katika shule za Kikatoliki: ili kuishi kwa pamoja utamaduni wa upendo. Ni hati iliyowasilishwa kwa waandishi wa habari mjini Vatican na Viongozi wakuu wa Baraza la Kipapa la Elimu Katoliki, chini ya uongozi wa Kardinali Zenon Grocholewski

Ni hati ambayo imepitishwa na Baba Mtakatifu Francisko hapo tarehe 28 Oktoba 2013, kama kumbu kumbu ya miaka 48 tangu Mababa wa Mtaguso mkuu wa Pili wa Vatican walipochapisha hati kuhusu elimu inayojulikana kama "Gravissimum Educationis". Hii ni hati muhimu sana kuwahi kutolewa baada ya Mtaguso mkuu wa Pili wa Vatican.

Kardinali Grocholewski anasema, mwaka 2015, Kanisa litafanya Jubilee ya Miaka 50 tangu hati juu ya Elimu ilipochapishwa na Mababa wa Mtaguso mkuu wa Pili wa vatican. Kanisa Katoliki limekuwa ni mdau mkubwa katika sekta ya elimu kwani kuna zaidi ya vijana billioni moja wanaopata elimu kutoka katika: shule na taasisi za elimu zinazosimamiwa na kuendeshwa na Kanisa Katoliki. Kuna waalimu na wafanyakazi millioni 58 ambao wameajiriwa kwenye shule na taasisi hizi.

Takwimu zinaonesha kwamba, katika kipindi cha Mwaka 2008 hadi mwaka 2011 kumekuwepo na ongezeko kubwa la wanafunzi wanaosoma katika shule na taasisi za Kanisa Katoliki sehemu mbali mbali za dunia. Idadi hii imepungua Barani Ulaya, lakini imeongezeka Barani Afrika, Asia na Oceania. Idadi ya wanafunzi wanaosoma kwenye shule na taasisi za Kanisa katika nchi changa ingeweza kuongezeka, lakini kuna mambo kadhaa ambayo bado yanakwamisha jitihada hizi.

Baadhi ya sababu hizi ni vita, kinzani na majanga asilia. Kuna uhaba mkubwa wa waalimu duniani na kwamba, kuna upungufu wa waalimu millioni 1.7, ili kufikia lengo la kuwa na waalimu wenye sifa na ubora unaotakiwa na UNICEF. Hali hii ni mbaya zaidi Barani Afrika, kwani takwimu zinaonesha kwamba, kuna mwalimu mmoja kwa wanafunzi mia moja!

Baraza la Kipapa la Elimu Katoliki limeendelea kusaidia kutoa utambulisho wa shule na taasisi zinazoendeshwa na kumilikiwa na Kanisa Katoliki. Kanisa linatambua kwamba, shule na taasisi hizi ni mahali pa ushuhuda wa imani unaowashirikisha, waamini walei pamoja na watawa ambao kwa kiasi kikubwa wanatekeleza utume wao kwenye sekta ya elimu.

Hati hii mpya anasema Kardinali Zenon Grocholewski inagusa kwa karibu zaidi changamoto mbali mbali za mwingiliano wa kitamaduni unaojitokeza kutokana na utandawazi na maendeleo sayansi na teknolojia. Walengwa wakuu wa hati hii ni wazazi na walezi we nye dhamana ya malezi na majiundo kwa watoto wao; waalimu, majaalimu na wafanyakazi ambao kwa pamoja wanaunda Jumuiya ya walezi.

Hati hii ni msaada mkubwa kwa Tume za Mabaraza ya Maaskofu kuhusu elimu pamoja na wadau mbali mbali wanaojihusisha na sekta ya elimu. Hii ni nyenzo ya majadiliano ya kitamaduni inataka kutoa kipaumbele cha kwanza kwa binadamu; uhuru wa kidini kwa kuzingatia utambulisho wa Kanisa Katoliki. Neno msingi ni majadiliano!

Lengo ni kuendeleza mchakato wa majadiliano ya kitamaduni katika sekta ya elimu, ili kujenga na kuimarisha utamaduni wa upendo, dhamana inayotekelezwa na Kanisa katoliki katika sekta ya elimu na kama sehemu ya utangazaji wa Injili ya Furaha.

Askofu mkuu Angelo Vincenzo Zani, Katibu mkuu wa Baraza la Kipapa la elimu anasema, tema ya majadiliano ni sehemu ya mchakato wa utume unaofanywa na Mama Kanisa katika sekta ya elimu. Hii ni changamoto iliyotolewa na Makardinali kunako Mwaka 2008 kwa kuhamasisha Kanisa kushirikiana na wadau mbali mbali katika sekta ya elimu, ili kuchangia maboresho ya elimu duniani. Kunako mwaka 2008, wawakilishi kutoka dini na madhehebu mbali mbali walichangia kuhusu umuhimu wa elimu katika mwingiliano wa tamaduni.

Baraza likaanza kazi yake kwa baraka na utashi wa Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI kunako mwaka 2011 muswada wa hati hii, ukapitishwa na wajumbe wa Baraza la Kipapa la elimu. Mang'amuzi ya majadiliano ya kitamaduni ni jambo ambalo limeonesha mafanikio makubwa sehemu mbali mbali za dunia.

Kunako Mwaka 2015 Kanisa litaadhimisha Jubilee ya Miaka 50 tangu Mtaguso mkuu wa Pili wa Vatican ulipochapisha Waraka kuhusu elimu. Mwaka huu pia Kanisa litaadhimisha Jubilee ya Miaka 25 tangu Katiba kuhusu elimu ilipochapishwa na kufanya rejea kuhusu vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu zinazomilikiwa na kusimamiwa na Kanisa Katoliki.

Friday, February 14, 2014

MPANGO KAZI WA VIWAWA PAROKIA YA BOKO 2014


UTANGULIZI
Kwa mwaka 2013, Vijana Parokia ya Boko tulifanikiwa kuyafanikisha matukio yote tuliyokuwa tumejipanga.
Pamoja na ufanisi huo yapo mengi ambayo yalishindwa kufanikiwa kwa asilimia zote na hii nikutokana na hali mbaya ya uchumi kwa Vijana wetu, na chama chetu kwa ujumla.
Kwa Mwaka 2014, Halmashauri ya VIWAWA Parokia imeridhia kupunguza baadhi ya matukio, ili kuweza kuleta ufanisi zaidi.
Kutokana na kutokuwepo kwa mashindo ya Vijana ya Dekania (dekania Cup) na  ya Jimbo (Pengo Cup), Uongozi wa Parokia umeona pia ni vyema kutoa mashindano ya Paroko Cup kwa Msimu huu.
MATUKIO YA MWAKA 2014
1.      Tutakuwa na  Mafungo ya Vijana wote wa Parokia yatakayo fanyika mwanzo wa kipindi cha kwaresima, na Mafungo haya hatafanyikia Mlango wa Imani Bagamoyo. Lengo la mafungo haya ni kuwafanya vijana waweze kuanza kutafakari safari ya Ukombozi wa Mwanadamu kwa Mateso, Kifo na Ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristo.
2.      Hija ya Vijana jimbo kuu la Dar es salaam itafanyikia Parokia kwetu Juma la nne la kwaresima siku ya Jumamosi.
3.      Siku ya JUMATATU YA PASAKA VIJANA WETU WOTE WA PAROKIA watakutana pamoja kwa ajili ya kusheherekea Ufufuko wake Bwana, hii ikiwa ni pamoja na kushirikishana mambo mbali mbali ya kimaisha.
4.      Mwanzo wa mwezi wa saba tutakuwa na ziara ya UINJILISHAJI JIMBO LA MBULU; Licha ya kwamba mwaka jana tulifanya ziara katika Jimbo hili kwa kutembelea Parokia tatu, bado changamoto za Kiimani ni kubwa sana ambapo sasa jamii ya kule inahitaji elimu zaidi juu ya mambo ya kiimani.
Hivyo kwa mwaka huu tunaenda na ujumbe wa IMANI MSINGI WA KANISA, na kuelimisha kwa kina zaidi juu utume wetu,
Tunatarajia kutembelea Jumla ya parokia nne, kwa ziara hii wenyeji wetu ni Parokia ya Dareda, zaidi ya hayo pia tutapata nafasi ya kutembelea mbuga ya wanyama ya Ngorongoro
5.      Tamasha la Vijana; huu ni utamaduni wetu wa kila mwaka, tamasha la mwaka huu litafanyika mwezi wa nane na litakuwa na semina, michezo ya ndani ambayo ni Maigizo, Ngoma, Kwaya, Nyimbo, Vichekesho na Show mbali mbali, tamasha hili linatarajiwa kufanyika kwa muda wa siku mbili(ijumaa jioni hadi Jumapili baada ya Misa).
6.      Kongamano la Ujirani Mwema (Parokia ya Bunju na Boko) halmashauri ya Viwawa Parokia inatarajia kuandaa kongamano la Ujirani mwema kwa Vijana na Viongozi wa Halmashauri ya Walei wa Parokia hizi, Kongamano hili litafanyika mwezi wa kumi na moja.
7.      Mwisho wa mwaka tunatarajia kuwa na semina ya siku moja kwa vijana wote; Lengo ni kuwakumbusha vijana wajibu wao katika kanisa na jamii kwa jumla.
NB: LIPA ADA YA CHAMA KWA MAENDELEO YA CHAMA CHETU, PIA UNAWEZA KULIPIA ADA ZA USHIRIKI YA MATUKIO YOTE YA VIWAWA KWA MWAKA 2014 KATIKA ACCOUNT YETU YA CRDB TAWI LA TEGETA.
ADA KWA MWEZI NI SHS 2000/= NA KWA MWAKA NI TSHS 24,000/= KWA KILA KIJANA.
ADA ZA USHIRIKI WA MATUKIO YOTE YA MWAKA NI TSHS 276,000/=
ACCCOUNT  NAME:VIWAWA PAROKIA YA BOKO
 ACCCOUNT  NO: 01524526820100


RATIBA HII YAWEZA KUBADILIKI KWA SABABU AMBAZO ZITAKUWA NJE YA UWEZO WETU, MATUKIO HAYA YAKIGONGANA NAYA PAROKIA YAKO ONYESHA UTII, FUATA YA PAROKIA.


TAREHE
TUKIO
WAHUSIKA
MAHALI
19/01/2014
MKUTANO MKUU
VIONGOZI WA VIGANGO, KANDA NA JUMUIYA
BOKO
08/03/2014
MAFUNGO
VIJANA WOTE
BAGAMOYO
16/03/2014
KIKAO CHA HALMASHAURI
VIONGOZI WA VIGANGO
BOKO
29/03/2014
HIJA
VIJANA WOTE
PAROKIANI-BOKO
5-6/04/2014
MAFUNGO
VIONGOZI WA PAROKIA, VIGANGO NA JUMUIYA
CONSOLATA – BUNJU-KIDEKANIA
13/04/2014
MISA YA MATAWI

VIJANA WOTE
DONBOSCO UPANGA
19/04/2014
MATENDO YA HURUMA
VIJANA WOTE
KIJIJI CHA FURAHA MBURAHATI –KIJIMBO
21/04/2014
GET TOGETHER
VIJANA WOTE

01/05/2014
SOMO WA VIWAWA (MT. YOSEPH)
VIJANA WOTE
DONBOSCO –UPANGA-KIJIMBO
11/05/2014
KIKAO CHA HALMASHAURI
VIONGOZI WA VIGANGO
 RAFAEL
08/06/2014
MKUTANO MKUU
VIONGOZI WA VIGANGO, KANDA NA JUMUIYA
BOKO
28-29/06/2014
KONGAMANO LA VIJANA JIMBO
VIJANA WOTE
SEKONDARI YA LOYOLA
01-07/07/2014
ZIARA YA UINJILISHAJI
VIJANA WOTE
JIMBO LA MBULU
20/07/2014
KIKAO CHA HALMASHAURI
VIONGOZI WOTE WA VIGANGO
MBWENI
15-17/08/2014
TAMASHA LA VIJANA
VIJANA WOTE
BOKO
23/08/2014
MAFUNGO
VIJANA  WOTE
BAGAMOYO-KIDEKANIA
21/09/2014
KIKAO CHA HALMASHAURI
VIONGOZI WOTE WA VIGANGO
RAFAEL
01-06/10/2014
KONGAMANO LA VIJANA KITAIFA
VIJANA WOTE
JIMBO LA NJOMBE(KITAIFA)
19/10/2014
KIKAO CHA HALMASHAURI
VIONGOZI WOTE WA VIGANGO
BOKO
15/11/2014
UJIRANI MWEMA
VIJANA BOKO NA BUNJU
BOKO
06/12/2014
SEMINA
VIJANA WOTE

13/12/2014
SEMINA
VIJANA WOTE
ST. GASPER – MBEZI-KIDEKANIA




18/01/2015
MKUTANO MKUU
VIONGOZI WA PAROKIA, VIGANGO NA JUMUIYA
BOKO








NCHI YANGU FAHARI YANGU TOUR